Nina mtaji wa milioni 6 nataka nianze biashara ya bodaboda

Nina mtaji wa milioni 6 nataka nianze biashara ya bodaboda

Nimejichanga nimefanikiwa kupata mtaji wa milion 6, nataka ninunue pikipiki 3 moja yangu na nyingne niwape vijana.

Kama unafahamu changamoto au ushauri tafadhali sema.
Changamoto ni hii best hao unaowapa unawaamini
 
Zote zina hela hila toyo ni [emoji91]

Hesabu kidogo hivi hizo za abilia utoka kwa foreni tena mpaka ijae kwa nauli ya jero kila abilia amabapo ikijaa jumla aifiki ata elfu nne net

Sasa toyo zinatoka muda wowote na mara nyingi ubeba mzigo mkubwa na kupeleka sehemu za mbali kidogo yaani pesa ya toyo kwa siku ni kubwa mara nne au sita ya pesa ya bajaji ya abilia.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Sikujua hili mm hua naona wamepaki wanapigwa upepo na toyo zao.
Ok ,toyo wanhoo mpya inaenda sh?

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
 
Bodaboda wapuuzi sana yalinikuta mimi.

Mungu ana nguvu sana, sisemi kwa ubaya ila Mungu fundi sana

Dogo alinidhurumu pesa zangu karibia 1M, nikachukua chombo changu tukaandikishana kwamba atanilipa ila akagoma, baada ya wiki akapata chombo kingine akaingia road Fuso ikapita nae pale pale bwana akatwaa.

Msidhurumu watu, ukidhurumu mtu anakuwa anaugulia kimya kimya Mungu anaweza kuyaona maumivu yake
Karma at work
 
Nimejichanga nimefanikiwa kupata mtaji wa milion 6, nataka ninunue pikipiki 3 moja yangu na nyingne niwape vijana.

Kama unafahamu changamoto au ushauri tafadhali sema.

Hongera sana mkuu. Kukusanya 6m si jambo dogo.

Kwanza nikuambie kila biashara ina changamoto zake, juhudi yako ndio itakufanya uone matunda ya biashara.

Achana na biashara za bahati nasibu, kama unaishi Dar tafuta boda boda moja tu kwanza halafu njoo nikupe mikate na vitafunwa (mimi ninayo Bakery) then wewe tafuta masoko yako zungusha mzigo masaa manne asubuhi na masaa manne jioni. Kulala na Laki moja kwa siku ni jambo la kawaida.

Nimesema uanze wewe kwanza na ukishazimudi changamoto zake ndio uwanunulie vijana wengine unaowaamini nao wabebe mikate.

Achana na kubeba abiria huko ndiko risk nyingi zilikojificha.


MCHANGANUO KIDOGO TU KUHUSU HILI:

1. Mkate kiwandani utachukua kwa Sh. 690-700 kwa kila mkate (Hii ni ile inayouzwa Sh. 1000-1200 dukani)

2. Utapeleka kwenye maduka na unaweza kuuza kwa Sh. 850-900 kutegemeana na maeneo. (mfano Tabata utauza 900, Temeke utauza 850)

3. Mtu wa dukani atauza Tsh. 1000-1200/=

4. Let say utapata wastani wa Sh. 150 kwa kila mkate mmoja utakaouza.

5. Jiwekee malengo ya kuuza Pc 500 asubuhi na PC 500 jioni. (kwa kuanza unaweza usifikishe lakin ukishalizoea soko hii ni averahe ya maduka 50 tu ya Mangi)

6. Hapo utakuwa na 150*500 =75,000/= per shift. Ukifanya Shift mbili unakuwa Tsh. 150,000/= per day. Tumia 50,000 kujiendesha na 100,000/= ishi nayo kama faida. Utakuja kunishukuru.

7. Kabla ya kufanya maamuzi, tafuta wale jamaa wa pikipiki wanaosambaza mikate ufanye upelelezi utaelewa nimi nasema.

CHANGAMOTO ZAKE

1. Kupata wateja- Hii utaitatua kwa kuanza kazi mapema ili usikute wenzako wamepita

2. Mtaji wa kuanzia - Kununulia mikate (Hii tukiweka terms sawa maweza kuwa nakupa mzigo wa malikauli unaleta pesa ukirudi)

3. Upatikanaji wa Mikate- Lazima uwe na kiwanda cha uhakika ili soko lako likuamini. Hapa unaeza kuja PM tuyajenge nikupe uhakika wa kupata mzigo


Baada ya wewe kufanikiwa unaweza sasa ku-husisha vijana wako wengine mkawa mnakipiga pamoja.

Nakutakia kila la Kheri.
 
Tupe details kuhusu hii biashahara

A, mtaji kiasi gani wa kuanzia?

B,biashara ipo mfumo gani ni udalali au unafungua frame kabisa kwa ajili ya wanunuzi?

C, changamoto ya upatikanaji mafuta, changamoto ya usafirishaji na kwa wanunuzi

D,faida inapatikanaje, mf lita moja itakupa faida ya kiasi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Dm Mkuu tuongee kuhusu hili
 
Njoo tuingie mkataba apa iyo ela yote ambayo unayo kisha niambie unataka boda walejeshe sh ngap kwa siku iyo pesa nitakuwa mi nakurejeshea na kwa muda ambao hao boda wangerejesha mkuu namaanisha njoo tuingie mkataba kwenye biashara yangu alafu niwe nakurejeshea izo pesa za pik pik 3 ambazo boda wengekuwa wanakurejeshea kwa siku mi nitakuwa nakurejeshea kaka kama uko serious plz njoo pm usifanye biashara ya kununua pik pik utalia mno broo nakusisitiza tena

Kama uko bize basi njoo tufanye mkataba unipe izo pesa na niwe nakurejeshea marejesho ambayo boda wengekulejeshea kwa siku plz kama uko interested njoo pm tuingie mkataba nitakuwa narejesha izo pesa ambazo hao boda wangekurejeshea per day na kwa duration iyo iyo ambayo ungewapa boda
 
PPi
Nimejichanga nimefanikiwa k Kkupata mtaji wa milion 6, nataka ninunue pikipiki 3 moja yangu na nyingne niwape vijana.

Kama unafahamu changamoto au ushauri tafadhali semaboda
Biashara ya boda inalipa sana sio Siri lakini inabidi upate dereva anayejielewa na anapassion ya iyo KAZI Kuna aina mbili za biashara ya boda Kuna mkataba na Kuna ya kipande.
MKATABA.
IPO Ivi Kwa siku elfu 12 Kwa dar es salaam. Baada ya miezi 12 kijana anachukua pikipiki mnaachana ambapo unakua umepata million 4 laki 3 na ishirini hapo boda boxer mpya million mbili na laki 6 kwaio faida ya million Moja na laki Saba na ishirini.
hii faida yake ni nzuri sana. Na watu wengi hufanya hii.

KIPANDE.
Kwa siku ni elf kumi lakini pikipiki inakua ya kwako mda wote. Na service unafanya wewe Kama za engine oil n.k hii hesabu zake ni million 3 na laki 6. Kwa mwaka. Hapo ukinununua used million 1 na laki 3 au 4 boxer mpya. Kwaio unaweza Kuta ndani ya miaka miwili unakua na boda 2 au 3 Kama ukiwa serious.
CHANGAMOTO.
Ajali nje nje
marejesho kutofika Kwa wakati kutokana na uaminifu.
matumizi mabaya ya chombo dereva uyo.
ila hakuna biashara ambayo Haina changamoto kikubwa ni kupambana.
NO RISK NO GAIN.






Nimejichanga nimefanikiwa kupata mtaji wa milion 6, nataka ninunue pikipiki 3 moja yangu na nyingne niwape vijana.

Kama unafahamu ctafadhWoto au ushauri tafadhali sema.

Nimejichanga nimefanikiwa kupata mtaji wa milion 6, nataka ninunue pikipiki 3 moja yangu na nyingne niwape vijana.

Kama unafahamu changamoto au ushauri tafadhali sema.

Ata ukimpa kijanaa
BIASHARA YA USAFIRISHAJI VYOMBO VYA MOTO INAHITAJI UWE SERIOUS I MEAN SIO KUCHEKA CHEKA. NA INAHITAJI RISKY YA HALI YA JUU.
BODA BODA Inalipa sana ukipata vijana waadilifu na wachapakazi na wenye nidhamu.
Kinachotakiwa kutoka kwako ni consistency bila kukata tamaa na uchapa KAZI. kanuni namba Moja usifanye BIASHARA bila kumuamini mtu. M nakutakia Kila la kheri Mungu akutangulie katika safari Yako ya mafanikio
 
Biashara ya boda boda ni nzuri kama utaendesha mwenyewe,japo siku hizi imekua biashara ngumu kiasi maana abiria hawapandi mtu wasie mjua.

binafsi hata mimi sipandi tu boda boda ilimradi nimepanda,hivyo ili uanze ona matunda ya hii biashara itakubidi uchaji solar sana kijiweni wakati wenzio unawaona wanatoka na kuingia.

ukizoeleka biashara utapga sana ila hapo mpaka uzoeleke sasa (maji umeyaita mma)

Kwa mtaji huo nakushauri kitu ambacho vijana wengi wanakichukulia poa mno mwisho wake wanawaza mabiashara yasio na future ya kueleweka.

Binafsi siwezi fanya biashara ya boda,ila mkuu nakushauri kwa mtaji huo Hebu kaa chini tafuta location nzuri chukua frem kisha fungua DUKA LA MANGI.

duka la vitu vya majumbani tunapenda kusema dukani kwa mangi,Mkuu nakuhakikishia hili duka ukiweza litunisha mtaji kama ulionao ukajaza mazaga zaga yote na mkawa wawili (wewe na waifu) waifu mchana yote anatoka saa 8:00 usiku,wewe unaingia muda huo hadi majogoooo, BABA BABA BABA mchawi lazima uitwe braza.


Duka la mangi ni biashara bomba sana yenye Future inayoeleweka,unapokua na mtaji mkubwa biashara ya Mangi inakupa more income ila boda boda hata ujambe uharishe hutokaa hata siku 1 ulaze faida LAKI ng'ooo utachora chini.

DUKA LA MANGI uwezo wa kulaza faida zaidi ya 100k per day kila siku biashara ikija changanyia mwendo wa 360km/hr boss kama nakuona hivi utavyokuja nishukuru badae.

Achana na ma idea ya vijana sijui boda boda,sijui toyo,sijui bolt,nk (sidharau hizi idea zao) lakini future yahizo biashara zao ni inaonekana kabisa, binafsi mimi sasa hivi huwezi niambia nifungue biashara ambayo nikiiangalia baada ya 5yrs haitoweza nipa 500k per day, sifungui mimi biashara.

Biashara zenye COSTANT INCOME sizitaki na wala siziwezi,napenda duka la mangi maana the more the capital the more the income the more the customer,nk

DUKA la Mangi ni biashara ambayo kijana yeyote anaetafuta maisha na amedhamiria kupambana na ana mtaji basi simshauri mara mbili namwambia tu mara 1 Asijifikirie aifanye bila kusita sita.

Duka la mangi linauza vingi brooo,kuna mchele,unga,sabuni,wine zote,vinywaji vyote yani unakusanya unakusanya hadi ukija jumlisha faida unasema Asante BABA wewe ni mkuu.

Mama yangu alikua akimiliki duka la mangi ezi hizo,ilikua ukiingia dukani chini sakafuni kuna coin kama zote zimedondoka,huwa haziokotwi dukani kuna coin nikawa najiuliza kwann mama anaacha pesa chini? nikienda dukani kwake najifanya viatu vinanibana nikiwa pale nnje nakunywa soda navua viatu then natafuta namna yyte ile niingie dukani,napita kukanyaga maeneo yenye coin nazifinya na kidole cha mguu naziinua natia mfukoni...

Mpaka nitoke dukani mfukoni nishamake hadi buku, (buku enzi zetu wazee sio masihara)

Leo nimekua ndio naelewa kwanini duka la mangi lina pesa,kwann mama alikua haokoti coin zikidondoka,mkuu duka ya mangi ina pesa kuliko watu wafikiriavyo.

Nafanya biashara nyingi ila mwaka Huu biashara yangu kubwa ninayoenda ifungua ni DUKA LA MANGI brother penye asali washirikshe na wengine,ifanye hii biashara ina faida nyingi sana sana sana.
Excellent
Kwa wastani duka hili linahitaji kianzio cha shiringi ngapi
 
Nimejichanga nimefanikiwa kupata mtaji wa milion 6, nataka ninunue pikipiki 3 moja yangu na nyingne niwape vijana.

Kama unafahamu changamoto au ushauri tafadhali sema.
Subira
 
PPi

Biashara ya boda inalipa sana sio Siri lakini inabidi upate dereva anayejielewa na anapassion ya iyo KAZI Kuna aina mbili za biashara ya boda Kuna mkataba na Kuna ya kipande.
MKATABA.
IPO Ivi Kwa siku elfu 12 Kwa dar es salaam. Baada ya miezi 12 kijana anachukua pikipiki mnaachana ambapo unakua umepata million 4 laki 3 na ishirini hapo boda boxer mpya million mbili na laki 6 kwaio faida ya million Moja na laki Saba na ishirini.
hii faida yake ni nzuri sana. Na watu wengi hufanya hii.

KIPANDE.
Kwa siku ni elf kumi lakini pikipiki inakua ya kwako mda wote. Na service unafanya wewe Kama za engine oil n.k hii hesabu zake ni million 3 na laki 6. Kwa mwaka. Hapo ukinununua used million 1 na laki 3 au 4 boxer mpya. Kwaio unaweza Kuta ndani ya miaka miwili unakua na boda 2 au 3 Kama ukiwa serious.
CHANGAMOTO.
Ajali nje nje
marejesho kutofika Kwa wakati kutokana na uaminifu.
matumizi mabaya ya chombo dereva uyo.
ila hakuna biashara ambayo Haina changamoto kikubwa ni kupambana.
NO RISK NO GAIN.











BIASHARA YA USAFIRISHAJI VYOMBO VYA MOTO INAHITAJI UWE SERIOUS I MEAN SIO KUCHEKA CHEKA. NA INAHITAJI RISKY YA HALI YA JUU.
BODA BODA Inalipa sana ukipata vijana waadilifu na wachapakazi na wenye nidhamu.
Kinachotakiwa kutoka kwako ni consistency bila kukata tamaa na uchapa KAZI. kanuni namba Moja usifanye BIASHARA bila kumuamini mtu. M nakutakia Kila la kheri Mungu akutangulie katika safari Yako ya mafanikio

Ndugu unafanya hii bishara
 
Back
Top Bottom