Nina siku ya nne sijaenda haja kubwa

Nina siku ya nne sijaenda haja kubwa

Nyankuru Wankuru

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2018
Posts
1,199
Reaction score
1,346
Watalaam wa lishe na wale wa afya ya mfumo wa chakula naomba mnisaidie kuhusiana na hili.

Yaani leo ni siku ya NNE sijaenda haja kubwa.

Sasa sijajua tatizo ni nini, nikawa na hypothesize labda nameza chakula bila kutafuna.

Mimi nimeoa ila my wife yuko mkoa mwingine kikazi na Mimi niko mkoa mwingine kikazi, so niko sawa sawa na bachala hivi.

Cha ajabu ninapoenda kwa my wife choo kwa siku huwa napata mara mbili tena cha maana kweli kweli.

Sasa ninaporudi geto geto choo kubwa inakuwa taabu kuipata kwa wakati.

Labda ni vyakula nilivyokula kwa mama ntirie yawezekana kilikuwa na amira.

Yaani naonekana Nina kitambi kikubwa , sasa sijui dawa ya kwenda haja kwa kila siku

Naomba kujua dawa ya kufanya niende haja kubwa kwa wakati

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ya ukwaju nilikua sihifahamu.
Ila mapapai Nina uhakika, Kwani naifahamu..
 
Aisee fanya upate hicho choo,
kikizidi kujikusanya huko halafu kisitoke utalia kilio cha aina zote.....halafu ukifika hiyo stage ukienda hospitali kuna dawa watakuwekea huko nyuma, usiombe ufike hiyo hatua....ina fedhehesha sana.
 
Huna haja ya kwenda hospitali. Anza utaratibu wa kunywa chai ya maziwa asubuhi na ndizi mbivu 3-4. Achana na chapati, vitumbua na maandazi kwa asubuhi.

Pata lunch kama kawaida.... ila punguza kiasi cha wanga na ongeza mboga za majani na matunda katika mlo wako.

Kunywa maji ya kutosha. Utaona tofauti baada ya muda mfupi sana.
 
Mkuu.. Swali la kichokozi. Hiyo avatar yako .... Je, inaakisi chochote kwa uzito pia ulionao? Kwa uzi huu... Hio avatar inasema mengi kwa sie tunaosoma kwa kutumia picha[emoji38][emoji2956][emoji2]
 
Una utamaduni wa kula vyakula vya aina gani kwanza tuanzie hapo
 
Back
Top Bottom