Ndugu wachangiaji wote wa hii thread niseme tu kwamba nawashukuru sana kwa mawazo yenu mliyoyatoa. Pamoja na kwamba mawazo yalitofautiana kutokana na mtazamo wa kila mchangiaji lakini naamini kuwa yote yalikuwa na mwelekeo wa kujenga na wala si kubomoa.
Kimsingi ni kwamba baada ya kusoma michango mbalimbali iliyotolewa nimeona kwamba sehemu kubwa ya mawazo yaliyotolewa yana support wazo langu nililokuwa nalo awali la ufugaji. Hii ndugu wadau ni kutokaa na Terms of Reference nilizokuwa nimeziweka kwenye topic husika na pia urahisi wa management ya project husika na pia ukubwa wa eneo nililonalo nyumbani ambalo badala ya kuwa idle na unprodroductive sasa litatumika katika uzalishaji. Wakati huo wanangu wadogo nilio nao nyumbani naamini kuna kitu watakuwa wanajifunza kwenye hii project. Possibly one day they'll be able to take a leaf out my book and eventually embark on smilar projects. Huwezi jua mipango ya Mungu.
Kuna wachangiaji wengine wanasema siyo kila siku ku copy na ku paste projects. Mimi nasema ni kweli si vizuri ku copy na ku paste kila siku. Lakini mbona hata kwenye ku copy na ku paste huko huko mtu anaweza akafanya hivi lakini akabadili font na font size na hata arrengement ya text husika na ikavutia msomaji kuliko ilivyokuwa awali. Hapa namaaisha kwamba mtu anaweza akacopy kitu lakini akaja na strategy tofauti na kule aliko copy.
Mfano nilipoanza biashara ya pharmacy nilikumbana na critics wengi tu. Na madai yakawa haya haya ya kuwa biashara ya pharmacy ni ya ku copy na ku paste. Mmoja wa critics hao akajana wazo la treasury bills and bonds. Lakini nika opt kufungua pharmacy ambayo within a few years ikaweza kuzaa pharmacy nyingine na mambo mengine kadhaa mazuri tu. Na hizi hizi ndizo zimenifikisha hii leo ninapokuja na hoja ya kuomba ushauri ili nilicho save niweze kuinvest tena katika mradi mwingine.
Lakini pia hata mtu unapoingia kwenye issue ya treasury bills and bonds haimaanishi kuwa wewe umeepuka swala la ku copy na ku paste. Wapo walioanza biashara hiyo wakafanikiwa na hadi kukuvutia na wewe kuingia huko.
Kitu kingine kama haujapata idea mpya na fursa zingine zenye faida na mtaji vipo je ukae tu ukisubiri upate idea yako mpya hadi lini ndugu zangu?
Kwa hiyo kutokana na michango yenu ya mawazo kwa sasa nafanyia kazi wazo la ufugaji kwa undani zaidi ikiwa ni pamoja na utotoleshaji na pia na products zingine zinazohusiana na ufugaji kwa ujumla. Nawashukuru sana na hamu yangu ni kuona mnabarikiwa sana.
Kwa niaba ya wachangiaji wote nasema hivi... 'Tumepokea shukurani zako' lakini mkuu siku hizi shukurani inaambatanishwa na maji ya kunywa. Kama hutojali nikutumie m-pesa yangu.
Sasa wewe unafikiri ukinunua hizo treasury bills wangapi watakuiga? niliwahi kusoma makala sijui ni kitabu kile sehemu fulani nkilionesha kwamba marekani ili matajiri waweze kukupa start up and whatever inabidi hiyo biashara yako isiwe rahisi kuigezeka au kuigwa i.e. coca cola naskia formula jamaa wamekaa nayo mpaka leo aiseee ndo mana pepsi na coca cola aka coke zina ladha tofauti...plus kua mwanziishi wa kitu inakufanya kama uwe pioneer wa hicho kitu aiseee yani kama vile una cruise control but you dont control the cruise...!!!! whatever that means...Mkuu hata ukaanzisha biashara mpya leo, watu wataiga tu. Kuiga ni kuzuri coz inafanya wazalishaji kuwa wengi na bidhaa kupatikana kwa wingi sokoni. Ushindani unaleta ahueni kwa mlaji.
Nyaka-One nimerudi tena kutoa ushauri mwingine mdogo na muhimu
Kwakuwa unahitaji project ambayo ni home based na Kwakuwa nyumbani pa kuishi hapapaswi kuwa na commercial scenes or environment hivyo basi unahitaji biashara ambayo the eyes of the regulators are very far or a business that is not easily regulated .... you can imagine the TRA on your foot steps
bado nasisitiza poultry venture itakuwa profitable and yes very lucrative .... hutapata adha ya kusumbuliwa na hawa watu Wa TRA, municipal licenses, TFDA and other regulators
apart from all your family will be guaranteed at least food supply for most of the daily life from the produce of poultry venture
I am in with experience and I started small but now its far from being a home based venture
all the best
mimi kwa muono wangu, wazo la ufugaji ndo ungestick nalo bila kuogpa ila ukatafuta njia ya kupunguza gharama. mfano gharama kubwa iko kwenye chakula kwa huo mtaji ungeweza nunua mashine ya kutengeneza chakula cha kuku kingine ukawa unauza na kilichibaki ukawapa kuku.
pia ili kupunguza gharama ya kununua vifaranga, unaweza unaweza fuga kuku wa mayai, wengi ambapo baadhi ya mayai ungeweza tumia kutotoleshea vifaranga mengine ukawa unauza hapo unakuwa umeua ndege wawili kwa wakati moja sabab hutakuwa na gharama ya kununua vifaranga kwa 1500 we unajiuzia yaan kwa sh 100 na kutotolesha ambapo huwez fikisha hata 1000 ukiwa unazalisha chakula chako.
pia ukiwa na incubator yako unaweza kuwa unachukua mayai ya wateja wengine na kuwatotoleshea kwa 300. hapo gharama ya umeme inajilipa yenyewe.
pia ungeweza funga solar ili kuweza endeshea incubator yako au mabanda ya kuku wako ili kuepukana na bili za umeme.
ukishindwa kabisa ninunulie tractor mie hata used nijiendee msumbiji nikalime baada ya miez nane nikupe twice ya hizo. serious