Nina Tshs. 45 milioni, Nifanye biashara gani?

Nina Tshs. 45 milioni, Nifanye biashara gani?

sikuwa na mpango wa kuingia humu leo lakini nimevutiwa na kushawishiwa na juhudi zako na wife wako..kwanza labda nikuulize unaishi wapi ili angalau hata mtu akitaka kukushauri kuhusu hiyo miradi mingine labda direction inaweza kusaidia..

pili kwa maelezo yako na msisitizo ulioweka kuwa lazima ifanyike maeneo ya nyumbani, mi nakushauri uendelee na hiyo hiyo baishara ya kuku, wala usiogope wala usitishike na hizo changamoto..

ila nikuullize jambo moja umeshafanya physical survey/search ya soko wewe mwenyewe? achana na media tembelea soko hilo la kuku/mayai na uone mwenyewe, au zungumza na wafugaji wakupe data za ukweli na pia unapokuwa sokoni utajifunza mbinu za kukabiliana na changamoto nyingi, mfano ikibidi unaweza kupunguza bei kidogo ili uatract wateja zaidi ilimradi tu kuhakikisha hakuna hasara..

hii biashara ya kuku ni nzuri we endelea na plan yako, na hongera kwa mafanikio
 
ni nzuri ukitafuta hizi biashara za kuwa wakala au msambazaji kwa kampuni mbalimbali za hapa nchini na nje ya nchi,na unaweza kupata taarifa hzo za kampuni zinazotafuta agent/distributors hapa www.mpakasi.com kuna fursa mbalimbali za kibiashara
 
Jikite katika kilimo,ufugaji..viwe vya kitaalamu zaidi,utaona matokeo makubwa na ya faida kubwa.

Ila usimamizi muhimu juu ya hayo nakufuata ushauri wa wataalamu.
Au Invest katikia Biashara za Nafaka fulani fulani.

Note.
 
Nawashukuru sana wadau mliokwisha changia mada hii na wale watakaoendelea kuchangia. Mwisho wa siku nitachuja mawazo yenu mliyoyatoa kwa nia njema na kwa umakini na hatimae kuibuka na maamuzi muafaka. Kwa pamoja tutajenga.
 
wewe sio mwenzetu kabisa,yani mshahara wako umaweza uka-save? Kabla sijachangia ebu tuambie kwa mwezi unapokea sh ngapi kama salary?
 
Kwa kuwa unataka mradi ufanyikie nyumbani kwako basi fuga nguruwe kama imani inaruhusu.
 
wewe sio mwenzetu kabisa,yani mshahara wako umaweza uka-save? Kabla sijachangia ebu tuambie kwa mwezi unapokea sh ngapi kama salary?

Ndugu yangu kuhusu kuweka hadharani kiasi cha mshahara wangu sidhani kama kutakusaidia chochote. Kwa hiyo sitakutajia. Naomba ushauri wako u base zaidi kwenye facts nilizokwisha ziweka hapa kama walivyofanya wana JF wengine waliokutangulia kuchangia mada hii. Nakutakia wikiendi njema.
 
Nyaka-One nimerudi tena kutoa ushauri mwingine mdogo na muhimu

Kwakuwa unahitaji project ambayo ni home based na Kwakuwa nyumbani pa kuishi hapapaswi kuwa na commercial scenes or environment hivyo basi unahitaji biashara ambayo the eyes of the regulators are very far or a business that is not easily regulated .... you can imagine the TRA on your foot steps

bado nasisitiza poultry venture itakuwa profitable and yes very lucrative .... hutapata adha ya kusumbuliwa na hawa watu Wa TRA, municipal licenses, TFDA and other regulators

apart from all your family will be guaranteed at least food supply for most of the daily life from the produce of poultry venture

I am in with experience and I started small but now its far from being a home based venture

all the best
 
Last edited by a moderator:
Bluetooth,
Ushauri wako kwenye mada hii hautapotea bure. Nakushukuru.
 
nilikuwekea wazo juu ya ufugaji wa kienyeji ila ile post siioni..
fuga kuku wa kienyeji pure Kisha nunua incubator utotoleshe kuku wakifika miezi 4-5 unachinja na kuuza katika hotels pia unafungua points ambazo utakua unauzia..kadri mzunguko utakavyokuwa mkubwa utaweza pia kuanza kusupply vifaranga wa kienyeji.
pia waweza kufuga bata nao wanafaida.
 
Jenga nyumba za kupanga au kuuza... there is no risk of losing all your money.
 
nilikuwekea wazo juu ya ufugaji wa kienyeji ila ile post siioni..
fuga kuku wa kienyeji pure Kisha nunua incubator utotoleshe kuku wakifika miezi 4-5 unachinja na kuuza katika hotels pia unafungua points ambazo utakua unauzia..kadri mzunguko utakavyokuwa mkubwa utaweza pia kuanza kusupply vifaranga wa kienyeji.
pia waweza kufuga bata nao wanafaida.

Thanks mkuu. Kutokana na mawazo ya wengi hapa naona wana support wazo la ufugaji nililokuwa nalo awali. Naona kuna haja ya kufanya thorough market survey kuhusu hili.
 
Bulldog na Primking: Nitafanyia kazi ushauri wenu kwa kufuatilia pale DSE.

Bwana Mapesa: You have a splendid idea. Nitalifanyia kazi wazo lako. Je una hint yoyote kuhusu minimum package ya vifaa vinavyotakiwa kwa ajili ya car wash na gharama zake (kwa hiyo minimum package)?

Zumbemkuu: ushauri wa kununua viwanja pia naupokea. Ahsante.

Bluetooth: Pia nakushukuru. Bado hatujakatia tamaa wazo tulilokuwa nalo awali kuhusu ufugaji. Ni kwa sababu tu nimeona ni busara kupata mawazo mbadala.

Delzzy: Wazo lako la kufungua decent restaurant huko Mbeya kimsingi siyo baya. Tatizo ninalo liona ni management yake ukizingatia kuwa mimi makazi yangu ni huku Dar na itakuwa shida kusimamia biashara ya mgahawa kwa kutumia remote. Ila ahsante sana kwa wazo lako.

Nawashukuru sana nyote mliokwisha toa mawazo yenu na mnaoendelea kutafakari nini cha kunishauri kuhusu ombi langu.
Mkuu kuna rafiki yangu anafanya hiyo biashara najaribu kuwasiliana nae ntakurudia hapahapa.Shukran
 
Wana JF,

Poleni na majukumu mliyonayo.

Ni kwamba mimi ninaishi Dar es Salaam. Umbali kutoka yalipo makazi yangu hadi city centre ni wastani wa kilometer 18. Nimeajiriwa sehemu ambako kwa maisha yetu ya kitanzania nadiriki kusema kwamba mshahara si mbaya kivile. Kutokana na ajira hii niliyonayo nimeweza kujenga nyumba ya kisasa kiasi fulani na pia kufungua miradi kadhaa hapa hapa jijini.Kwa kiasi kikubwa hii miradi inasimamiwa na mke wangu akisaidiwa na watu wengine tuliowaajiri.

Sasa kutokana na faida iliyopatikana kutokana na miradi hii ambayo imedumu kwa muda wa miaka minne napia saving yangu inayotokana na ajira yangu tuliweza kugawa hiyo faida katika mafungu makubwa mawili. Fungu la kwanza ikiwa ni kukuza mtaji kwa kila mradi uliopo na fungu la pili likiwa ni kufungua mradi mwingine mpya ambapo tuliutengea jumla ya Tshs. 45,000,000/=. Mradi huo mpya tulilenga kuufanyia nyumbani ili kuwa na usimamizi wa karibu (kwa maana ya kuuona kila siku) lakini usiohitaji uwepo wa mimi na mke wangu muda wote (kati ya saa moja na nusu asubuhi na saa kumi jioni)

Baada ya kutenga kiasi hicho chapesa tulifanya investment portfolio analysis na tukaona kwamba tungeweza kuwekeza pesa hiyo kwenye mradi wa ufugaji wa kuku wa kisasa wa mayai (2,000),kuku wa kienyeji (2,000) na pia kanga (1,000) na pia kununua vifaa mbalimbali kwa ajili ya ufugaji huo kama incubator, generator, n.k. Maamuzi ya kufanya mradi huo pamoja na factors zingine yalizingatia taarifa tulizokuwa nazo kuhusu faida nzuri ya ufugaji huo na pia eneo tulilo nalo nyumbani ambalo ni mita za mraba 2,600 na liko liko fenced.

Sasa taarifa nilizo nazo hivi karibuni soko la mazao ya ufugaji huu hasa kwa upande wa mayai ya kuku wa kisasa siyo zuri kutokana na uingizwaji wa mayai kutoka nchi jirani ambayo uuzwa kwa bei ya chini ukilinganisha na bei ya wafugaji wa hapa Dar. Pia gharama za ufugaji wa hao kuku na kanga kuonekana kuwa kubwa kulinganisha na hali ya soko kwa sasa. Hali hii imetufanya tusite kuwekeza kwenye mradi huu wa ufugaji (kwa ujumla wake) kwa sasa ili kuepuka hasara ambayo inaonekana kuwa wazi kwa macho ya haraka haraka.

Sasa ndugu zangu nikaona si vibaya kuja hapa JF ili ikiwezekana basi kupata ushauri wa mawazo mbadala ambayo tutayafanyia kazi na kuweza kuwekeza kiasi hicho cha pesa lakini wakatiwa kutoa ushauri naomba mzingatie kwamba mradi huo mpya unatakiwa ufanyikie katika eneo la nyumbani ninapoishi.

Natanguliza shukurani zangu kwenu wana JF.

Mkuu chukua 15m jenga mabwawa matano ya samaki aina ya perege/sato. Baada ya miez 4 unaanza kula faida kiulaini. Hii biashara haina competitors wengi. Kwa ushauri mwingine wa kibiashara unipe laki 7 kama consultation fee. Kila la heri.
 
kuna bank unaweka hela kwenye fixed deposit account na kisha unachukua 90% ya hiyo hela kuendelea na uwekezaji. kama utaweka mil 100 utapata mil 12 kwa mwaka. na mil 90 unaichukua kama mkopo unafanya biashara nyingine. PM Mimi.
Huo mkopo si utakuwa na interest na inaweza kuwa zaidi ya mil 12 kwa mwaka?
 
Watanzania hua hatunaga idea mpya ni zile zile kila siku fuga kuku,duka la hardware...kuna uzi ulikuwepo humu unazungumzia kununua treasury bills, bonds, kama vipi jaribu hayo mambo huo uzi wafuga kuku wote waliukimbia sio kwamba nabeza kufuga kuku lakini ni muda sasa biashara zibadilike sasa sio zile zile za photocopy..Over...
 
Back
Top Bottom