Nina upungufu wa nguvu za kike, waungwana nisaidieni!

Ntigy

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2014
Posts
489
Reaction score
267
Wahenga walisema "Mficha uchi hazai".
Jamani nisaidieni,mwenzenu sina hamu kabisa ya kufanya mapenzi. Hata niandaliwe vip au nijiandae kisaikolojia namna gani nabaki mkavu na sifurahii tendo la ndoa hata kidogo.

Sio mpenzi wa picha za ngono, sio mlevi wala mvuta sigara, nakula vizuri, sina msongo wa mawazo, vipimo vinaonesha homoni ziko sawa lakini tatizo limekuwa sugu siku hadi siku. Nilienda hospitali sikupata msaada zaidi ya kushauriwa kutumia K-Y gel.

Ndugu zangu kama kuna anayejua matibabu au suluhisho la tatizo hili anisaidie kwani hii hali inanitesa sana. Asanteni!

======

MREJESHO: UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIKE.
 
Una mpenzi?
 
Usikute unatoa nyuma, maana ukitoa nyuma hisia za mbele zinahamia nyuma huku mbele kukipoteza mawasiliano.

Pili usikute umekeketwa

Tatu usikute unayefanya nae ngono huna hisia nae za kimapenzi.
Mwisho km yote hayo huna kasoro nayo, majaaliwa kesho kazini nitawauliza madaktari wazoefu na specialist kwenye magonjwa ya uzazi then nitakuletea majibu.

Pia ningependa kujua hilo tatizo limekuanza lini??
 
Sijawahi kuliwa nyuma,sijakeketwa nampenda sana mpenzi wangu lakini hali ndo hiyo.
 
Tatizo la muda mrefu sasa,yapata miaka 3 tangu lianze ila lilianza kidogo kidogo mpaka sasa limekuwa sugu.
Okay

Kwavile hormone levels ziko normal, it sounds like a deeper issue. Ina maana ni psychological

Nimeona umemjibu mtu kuwa una mpenzi na unampenda, kwa hiyo nitaasume huna any relationship problems
Ila kama unastress na unafanya vitu vinavyo kufanya uwe unachoka, pia inaweza kuchangia hali hiyo

Kitu kingine ni depression

Pia dawa za kuzuia mimba zinaweza kusababisha hiyo hali

Ushauri wangu ni kama unatumia dawa za kuzuia mimba, basi punguza na muwe mnatumia condom
Pia nenda kaonane na psychologists na halafu ukafanye vipimo vingine zaidi ili kujua kama kuna underlying medical conditions
 
Asante kwa mchango wako wa mawazo. Nina muda mwingi wa kupumzika na sijawahi kutumia dawa za uzazi wa mpango.
 
Swali hili linahusiana nini na tatizo lake,?
sijakulupuka kumuuliza hilo swali kwa bahati mbaya au nzuri mimi huwa sipendi kuwakwaza watu

Huyu dada najaribu kumuuliza maswali ili nione tatizo lake ni swala la psychology au ni suala la homoni.

Kwa hiyo kuwa mpole tu mimi sio chizi kumuuliza hilo swali
 
Tafuta supplements zinazoitwa Horny goat weed.Kisha utaleta mrejesho baada ya matumizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…