Nina wapenzi wawili nimuoe nani kati yao?

Alikuwa anatafuta support ila kaambulia spana za utosi! Mwanamke wa kuoa ni A huyo B ni wa kuendelea kumchakata kwa siri kama hataki ampige chini tu 😂😂😂 ila mke ni A
 
Binafsi nakushauri uwe na A kwasababu zifuatazo,moja mnajuana vizuri,maana miaka mi5 inatosha kufahamiana,pili ni mnyenyekevu,nasema hv maana umeeleza kuwa tangu huna kitu mpaka leo mpo nae so kwako hajafwata faida za kibnafsi,pia napenda nikukumbushe kuwa utu wa mtu hautegemei kabila lake,halafu uache kuwanyanyapa watu wenye ulemavu,yangu n hayo mkuu.
 
Huyu jamaa mwehu kweli yani wanaume wanakataaga pepo wenyewe wanakimbilia moto wa duniani 😂😂😂
 
Makurubembe yanakutia spana hadi unarudisha majeshi nyuma😅 ukipata mwanamke anayekupenda unakituliza
 
Atalia na kusaga meno,, anatupa dhahabu kwa vipande vya chupa
 
Unataka kuuvaa mkenge kwa kumuoa B pamoja na kuwa maelewano yenu ni dhaifu. Mguu mfupi uliridhika nao kwa miaka mitano ya kuwa pamoja lakini sasa unauona ni tatizo. Ukiamua kumtelekeza huyo A kwa visingizio visivyo na kichwa wala miguu Mwenyezi Mungu amlipie kwa kumpotezea muda wake.
 
Pole sana.. Mwanaume unatakiwa uwe na msimamo... A ni best
 
Umeyumba tena umeyumba vibaya mno. Unalo litafuta utalipata muda si mrefu.

Eti anachechemea shame on you!!
 
Kakaa huyo dada uliyeanzanye mbali usimwache, kwanza inaonekana ni mwanamke mwenye bahati na pia mwenye kukuvumilia!!

ushauri wangu usimwache huyu dada kisa ulemavu wake.

akikulilia huta kaa hufike popote! ( miaka mitano mtoto wawatu umemchakata, umembinuabinua afu unata umwache).

kaka ni laana iwe juu yako na sio sii juu ya watoto wetu.
 
Ila mademu wa Chuo si wakuwawekee plan kabisaaaa

Wale wasnge ni wa kupelekea moto halafu unalala mbereeeee
 
Wakilingana umri mke stawahi kuzeeka akizaa bana. At least kuwe na age difference
Hahahahahah mke akizeeka haina shida hamna ambaye hataazeeka hio tabia ya age difference ndio mnakuja kutesa wazee na michepuko yenu viben 10 bora wote damu zipoe pamoja sio mmoja damu baridi mwengine bado ana joto!
 
Makurubembe yanakutia spana hadi unarudisha majeshi nyuma😅 ukipata mwanamke anayekupenda unakituliza
kweli mkuu yaani nimepata bahati ya kua na msichana mtulivu sana sana Katika kizazi hiki ni wachache sana Kuna muda hua najaribu kutest mizinga ya nyuki hua naambulia manundu natoka nduki
Vi slay kwini hivi havifai dadeq!
😂😂😂
 
Unamkataa A kisa anachechemea, unaoa B anakuja pata ajali miguu yote inakatwaa... Cjui utaacha pia???
 

I insist,

The 3 F’s of dating.

- Fossil. - Be older.

- Fortunes. - Be wealthier.

- Fitness. Be fitter.

The Fossils calculator:

  • Divide your age by 2
  • Add 7 or 8 or 9 or 10
  • That should be her age.

Be patient. Don't rush.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…