Ninaamini kuna kanuni za siri tena rahisi zinazoratibu mambo haya ya Ulimwengu hasa Teknolojia

Ninaamini kuna kanuni za siri tena rahisi zinazoratibu mambo haya ya Ulimwengu hasa Teknolojia

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Baada ya salamu naomba kushare nanyi jambo hili ambalo nimekuwa nikilitafakari kwa siku nyingi sana.

Kuhusu mambo ya kilimwengu hasa haya mambo ya sayansi na technolojia.tukiangalia namna tunavyopata picha katika tv kupitia ving'amuzi mbalimbali na sauti na watu tukawaona live pale kwenye screen, naamini fika kuna kanuni za kilimwengu ambazo zinaongoza haya mambo bado hatujazijua vizuri

Ni jambo kubwa sana kuona tukio la kigoma live ukiwa pale gongo la mboto ukiangalia television.lakini leo tunaona na ni kweli.

Tunaongea na mtu akiwa mbali kabisa kupitia simu na bado tunasikiana,hili linafikirisha sana hawa waliogundua walitumia fika akili zao

Kinachonifanya nione kuwa kuna kanuni za asili zinaendesha haya mambo ni kwa sababu zifuataza.

1.Wote tumekuja duniani tumekuta kanuni zipo tayari tokea hapo zamani tulichofanya ni kutumia hizo kanuni na sio kuzianzisha.

Mfano kanuni ya third law of motion hii ilikuepo tangu na tangu hata kabla ya isaack hajazaliwa,kazaliwa kaikuta kabisa hii kanuni akaanza kufanya mambo yake kupitia hii kanuni.
Na kanuniz zingine nyingi sana.

Mfano mzuri ni kanuni ya kusafirisha mawimbi ya sauti kutoka kwenye simu yangu kuja kwenye simu yako ukiwa mbali.

Ninaamini kuna kanuni ya asili ambayo hao waliotengeneza simu wameikutawao wakaunda vifaa tu na kuacha kanuni za asili zifanye kazi yake.

Siamini kama wao ndo wanasafirisha hizo sauti kutoka kwa mtu kwemda kwa mtu,bali kanuni za asili ndo zinafanya mambo hayo.

Hata katika mambo mbalimbali ya kusafirisha picha kutoka kigoma live kuja dar tukaona kwemye tv naamini kuna kanuni za asili zinazoongoza haya mambo.

Ninaamini kanuni hizo sio kwamba zimejificha,zipo ila tunaweza kuzipata kupitia matendo yetu ya kawaida ya kila siku tukatumia kanuni hizo kufanya matendo makubwa zaidi.

Mfano mimi naamini kuwa mtoto analijua jina lake kwa sababu ya kuitwa mara nyingi jina hilo na watu wakimuangalia yeye,kupitia kanini hiyo ya marudio ya sauti mtoto anajua kuwa hapa anaitwaax yeye na hilo ndio jina lake.

Hivyo kupitia kanuni hii ya asili ya marudio,mtoto mdogo ukimuita jina lake mara 1000 kwa siku kwa muda wa mwaka mmoja.

Na mtoto mwingine kwa siku ukamuita jina lake mara 1 kwa siku kwa muda wa mwaka,basi huyo wa mara 1000 atajua mapeema kuwa hilo ni jina lake na huyu wa mara 1 atachelewa kujua jina lake.

Hii ina maana ya kuwa kutumia kanuni hii ya asili ya marudio tunaweza kumpa jina paka,au mbwa au hata panya unaemfuga kwa kurudiarudia kumuita jina hilo.

Sio kwamba wanaowapa majina wanyama kuwa wao wamesababisha na wanauwezo hapana,bali walitumia kanuni ya asili ya marudio ambayo wameikuta duniani kufanya mambo yao ambayo yanategemea kanuni hizo.

Je, una mawazo yeyote juu ya hili suala ?

Karibu
 
Kanuni za kisayansi (scientific laws) hazikuwepo bali zimevumbuliwa na wanasayansi.

Kanuni zote za kisayansi; The Laws of Motion (Isaac Newton), Hooke's Law (Robert Hooke), Laws of Planetary Motion (Johannes Kepler), Ohm's Law (Georg Ohm) n.k. zimetokana na majaribio na tafiti za kisayansi zinazohusu masuala yaliyopo na yanayoonekana.

Kwa ujumla, kanuni za kisayansi ni maelezo ya kisayansi kuhusiana na masuala pamoja na matukio mbalimbali yanayoonekana katika mazingira ya asili.

Isaac Newton, wakati anatoa machapisho ya kazi zake kama vile Principia, alizitumia kanuni kadha wa kadha kueleza na kufafanua miendo ya vitu mbalimbali katika mazingira yetu ya kawaida (Newton's Laws of Motion).

Maana yake ni kuwa, mazingira ya asili na miendo ya vitu mbalimbali ilikuwepo hapo kabla lakini hakukuwa na ufafanuzi wa kisayansi kuhusiana na kufanyika kwa masuala hayo kabla ya Newton kuwepo. Hali kadhalika kwa kanuni nyinginezo.
 
Kanuni za kisayansi (scientific laws) hazikuwepo bali zimevumbuliwa na wanasayansi.

Kanuni zote za kisayansi; The Laws of Motion (Isaac Newton), Hooke's Law (Robert Hooke), Laws of Planetary Motion (Johannes Kepler), Ohm's Law (Georg Ohm) n.k. zimetokana na majaribio na tafiti za kisayansi zinazohusu masuala yaliyopo na yanayoonekana.

Kwa ujumla, kanuni za kisayansi ni maelezo ya kisayansi kuhusiana na masuala pamoja na matukio mbalimbali yanayoonekana katika mazingira ya asili.

Isaac Newton, wakati anatoa machapisho ya kazi zake kama vile Principia, alizitumia kanuni kadha wa kadha kueleza na kufafanua miendo ya vitu mbalimbali katika mazingira yetu ya kawaida (Newton's Laws of Motion).

Maana yake ni kuwa, mazingira ya asili na miendo ya vitu mbalimbali ilikuwepo hapo kabla lakini hakukuwa na ufafanuzi wa kisayansi kuhusiana na kufanyika kwa masuala hayo kabla ya Newton kuwepo. Hali kadhalika kwa kanuni nyinginezo.
Hata ufafanuzi wa kisayansi pia kuna mambo haujafafanua.

Tumekubaliana kuwa matukio ama sheria za asili zipo tokea zamani kabla ya hao wanasayansi kuwepo,na ndio maana wameweza kutoa ufafanuzi kwa sababu wanatolea ifafanuzi juu ya jambo ambalo wamelikuta.

Lakini ufafanuzi huo umeishia sehemu haujafika moja kwa moja na kutosheleza.

Mfano..

Sayansi inaweza kueleza kuwa kitu kurudi chini ukirusha ni gravitational force.

Lakini kwa nini kirudi chini kisiende kulia au kushoto au mbele au nyuma n.k

Hapo ni kuwa sayansi haiwezi kutoa majawabu nyooofu.

Nakubali kuwa wamezitungia ufafanuzi kanuni za asili na tunashukiru kwa mchango wao huu..
 
Kanuni za kisayansi (scientific laws) hazikuwepo bali zimevumbuliwa na wanasayansi.

Kanuni zote za kisayansi; The Laws of Motion (Isaac Newton), Hooke's Law (Robert Hooke), Laws of Planetary Motion (Johannes Kepler), Ohm's Law (Georg Ohm) n.k. zimetokana na majaribio na tafiti za kisayansi zinazohusu masuala yaliyopo na yanayoonekana.

Kwa ujumla, kanuni za kisayansi ni maelezo ya kisayansi kuhusiana na masuala pamoja na matukio mbalimbali yanayoonekana katika mazingira ya asili.

Isaac Newton, wakati anatoa machapisho ya kazi zake kama vile Principia, alizitumia kanuni kadha wa kadha kueleza na kufafanua miendo ya vitu mbalimbali katika mazingira yetu ya kawaida (Newton's Laws of Motion).

Maana yake ni kuwa, mazingira ya asili na miendo ya vitu mbalimbali ilikuwepo hapo kabla lakini hakukuwa na ufafanuzi wa kisayansi kuhusiana na kufanyika kwa masuala hayo kabla ya Newton kuwepo. Hali kadhalika kwa kanuni nyinginezo.
The sama kwamba wao wameelezea matokeo juu ya kitu fulani na sio kwamba wao ndo wanasababisha matokeo hayo na kuyacontrol
 
Mkuu umepinga umezunguuka lakini mwisho umeangukia kwenye key concept ya mtoa Mada.
Wewe umenielewa mkuu.

Oengine jamaa hakuelewa.

Yaani wanasayansi kazi yao ni kutunga maelezo juu ya matukio ambayo wameyakuta.

Kwa maana maelezo yao yanafuata mtiririko wa matukio waliyoyakuta,na sio matukio hayo yafuate maelezo ya hawa wana sayansi
 
This means kwamba maajabu bado yapo as long as Jesus yupo
 
Baada ya salamu naomba kushare nanyi jambo hili ambalo nimekuwa nikilitafakari kwa siku nyingi sana.

Kuhusu mambo ya kilimwengu hasa haya mambo ya sayansi na technolojia.tukiangalia namna tunavyopata picha katika tv kupitia ving'amuzi mbalimbali na sauti na watu tukawaona live pale kwenye screen, naamini fika kuna kanuni za kilimwengu ambazo zinaongoza haya mambo bado hatujazijua vizuri

Ni jambo kubwa sana kuona tukio la kigoma live ukiwa pale gongo la mboto ukiangalia television.lakini leo tunaona na ni kweli.

Tunaongea na mtu akiwa mbali kabisa kupitia simu na bado tunasikiana,hili linafikirisha sana hawa waliogundua walitumia fika akili zao

Kinachonifanya nione kuwa kuna kanuni za asili zinaendesha haya mambo ni kwa sababu zifuataza.

1.Wote tumekuja duniani tumekuta kanuni zipo tayari tokea hapo zamani tulichofanya ni kutumia hizo kanuni na sio kuzianzisha.

Mfano kanuni ya third law of motion hii ilikuepo tangu na tangu hata kabla ya isaack hajazaliwa,kazaliwa kaikuta kabisa hii kanuni akaanza kufanya mambo yake kupitia hii kanuni.
Na kanuniz zingine nyingi sana.

Mfano mzuri ni kanuni ya kusafirisha mawimbi ya sauti kutoka kwenye simu yangu kuja kwenye simu yako ukiwa mbali.

Ninaamini kuna kanuni ya asili ambayo hao waliotengeneza simu wameikutawao wakaunda vifaa tu na kuacha kanuni za asili zifanye kazi yake.

Siamini kama wao ndo wanasafirisha hizo sauti kutoka kwa mtu kwemda kwa mtu,bali kanuni za asili ndo zinafanya mambo hayo.

Hata katika mambo mbalimbali ya kusafirisha picha kutoka kigoma live kuja dar tukaona kwemye tv naamini kuna kanuni za asili zinazoongoza haya mambo.

Ninaamini kanuni hizo sio kwamba zimejificha,zipo ila tunaweza kuzipata kupitia matendo yetu ya kawaida ya kila siku tukatumia kanuni hizo kufanya matendo makubwa zaidi.

Mfano mimi naamini kuwa mtoto analijua jina lake kwa sababu ya kuitwa mara nyingi jina hilo na watu wakimuangalia yeye,kupitia kanini hiyo ya marudio ya sauti mtoto anajua kuwa hapa anaitwaax yeye na hilo ndio jina lake.

Hivyo kupitia kanuni hii ya asili ya marudio,mtoto mdogo ukimuita jina lake mara 1000 kwa siku kwa muda wa mwaka mmoja.

Na mtoto mwingine kwa siku ukamuita jina lake mara 1 kwa siku kwa muda wa mwaka,basi huyo wa mara 1000 atajua mapeema kuwa hilo ni jina lake na huyu wa mara 1 atachelewa kujua jina lake.

Hii ina maana ya kuwa kutumia kanuni hii ya asili ya marudio tunaweza kumpa jina paka,au mbwa au hata panya unaemfuga kwa kurudiarudia kumuita jina hilo.

Sio kwamba wanaowapa majina wanyama kuwa wao wamesababisha na wanauwezo hapana,bali walitumia kanuni ya asili ya marudio ambayo wameikuta duniani kufanya mambo yao ambayo yanategemea kanuni hizo.

Je, una mawazo yeyote juu ya hili suala ?

Karibu
Mbona kawaida, kuna laws of nature zipo tu, ni kuzifuata kutengeneza vitu.
 
Mkuu umepinga umezunguuka lakini mwisho umeangukia kwenye key concept ya mtoa Mada.
Mtoa mada amesema kuwa kanuni kama Third Law of Motion ilikuwepo kabla ya Newton. Mimi nimepinga na nimesema kuwa haikuwepo kabla ya Newton maana Newton ndiye aliyeivumbua.

Mtoa mada anachanganya kati ya kanuni za kisayansi (scientific laws) na matukio ya asili (natural phenomena). Kanuni za kisayansi zimevumbuliwa na wanasayansi ili kuyaelezea matukio ya asili. Kanuni hizo hazikuwepo hapo kabla.
 
Maana yake ni kuwa, mazingira ya asili na miendo ya vitu mbalimbali ilikuwepo hapo kabla lakini hakukuwa na ufafanuzi wa kisayansi kuhusiana na kufanyika kwa masuala hayo kabla ya Newton kuwepo. Hali kadhalika kwa kanuni nyinginezo.
Na hiki ndicho alicholenga mleta mada
 
Na hiki ndicho alicholenga mleta mada
Kanuni zimevumbuliwa na wanaadamu,mfano kanuni ya aerodynamics inayotumika kutengeneza Ndege,watu wa kwanza kutengeneza Ndege,Wright brothers waliweza kwa majaribio Mengi sana,baadae wengine wakaisoma,wakaangalia Ndege/,birds wanavyoweza kuruka,shape ya mabawa yao,na wao wanatengeneza Ndege yenye muundo huo,na kwa kutumia kanuni kadhaa,wakajua wakitengeneza bawa lenye shape fulani,Ndege inaweza kuruka,
Kanuni ya action and reaction,ingetumika pia kutengeneza rockets,Bunduki,mizinga,kwa ku study ulimwengu na majaribio kadhaa ya nguvu za asili zilizopo ulimwenguni,mwanadamu aliweza kutengeneza kanuni ambazo zikitumika,zinaleta matokeo yaliyatarajiwa,
Mfano ukizungusha sumaku karibu na coil ya waya,unatengeneza umeme,
 
Kwa mfano swala la Time machine......ili kuweza kutravel through time....
 
Concorde ilikuwa inafika Marekani kabla haijaondoka Ulaya [Local time departure: saa nane mchana; Local Time arrival: Saa tano asubuhi, same day].
 
Alichokosea mleta mada ni kuchanganya matukio ya asili na kanuni za kisayansi. Hivyo ni vitu viwili tofauti.
Kanuni za kisayansi ni maelezo tu ambayo yanafuata matukio ya asili.

Mfano newton third law of motion ni kanuni ya kisayansi ambayo imefuata matukio ya asili ambayo yakamfanya bwana newton ahitimishe kwa kusema kwamba "for every action there is an equal and opposite reaction.

nadhani mkuu wewe ndio hujanielewa.

wanasaysnsi wanayatafakari matukio ya asili then ndio huyatungia kanuni kupitia matukio hayo akbayo wameyakuta hapa ulimwenguni.
 
Kanuni za kisayansi (scientific laws) hazikuwepo bali zimevumbuliwa na wanasayansi.
HAPANA. KANUNI HIZI ZILIKUWEPO KABLA, VINGINEVYO WALIOZIVUMBUA WASINGEWEZA KUZIVUMBUA KAMA ZISINGEKUWEPO KABLA
ZILIKUWEPO ILA ZILIKUWA HAZIJULIKANI RASMI
NATURAL LAWS ZINA EXIST BILA KUJALI KUWA WEWE UNAZIJUA AU HUZIJUI
 
Back
Top Bottom