Ninachoshindwa kuelewa ni kwamba Tanzania wanataka madereva wa Tanzania wasipimwe wanapoingia Kenya au hata wakiwa positive waingie?

Ninachoshindwa kuelewa ni kwamba Tanzania wanataka madereva wa Tanzania wasipimwe wanapoingia Kenya au hata wakiwa positive waingie?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Hizi bifu na Kenya sasa naona kama ni utoto na nashangaa inafikia hata viongozi wetu wa ngazi ya mkoa wanahemuka na maamuzi bila kufikiria kumaliza mambo kidiplomasia. Hawa viongozi wanadhani wanamfurahisha Magufuli lakini ukweli ni kwamba wanamdhalilsha Magufuli na Tanzania kwa ujumla.

Ona kwamba tumekuwa na migogoro mipakani sio na Kenya tu, bali na Rwanda na Zambia pia. Hiyo ni dalili kwamba sisi ndio wenye tatizo. Ukiona kila siku wewe tu ndio unagombana na jirani zako, tatizo sio jirani, ni wewe!

Kwanza kabisa tuelewe kwamba nchi hizi jirani, japo sisi hatukuweka lockdown, wao waliweka. Sasa hatuwezi kuwalazimisha wasiwe na lockdown kwa Watanzania kwa kuwa sisi huku kwetu hakuna - huko ni kukosa si tu busara bali akili pia. Kwa mfano, Kenya wana lockdown kiasi kwamba hata kusafiri kati ya jimbo na jimbo, mfano, Nairobi na Mombasa, hairuhusiwi isipokuwa kwa vibali maalum.

Sasa sis tunachotaka kwa Wakenya au Rwanda au Zambia ni nini hasa? Tunataka madereva wetu wasipimwe wanapoingia kwenye hizo nchi? Au tunataka madereva wetu hata wakipimwa wakaonwa wana Corona waruhusiwe tu kuingia kwa kuwa kwetu hakuna lockdown?

Ona kwamba madereva wetu wanasema hawaviamini vipimo vya Kenya. Kenya watafanyaje vipimo vya udanganyifu kwa madereva ambao wanapeleka bidhaa kwao? Hiyo ni akili kweli kudhani mtu unaemplekea bidhaa kama chakula nk akukomoe kwa kukufanyia kipimo cha uongo? Tanzania tunataka tuamini vipimo vipi, maana hata vya kwetu tulisema vinasema mapapai yana Corona ni vipimo feki. Kama ni hivyo tupimwe madereva wetu mipakani basi ili wanapopimwa upande wa Kenya tuweze kubisha kisayansi kuwa upande wetu tumewapima wakaonekana negative.

Vitu vingine tusijifanye kuwa wajuaji na kukorofishana na jirani zetu pasipo sababu. Hatuwezi kuwalazimisha wasiwe na restrictions za Corona kwa kuwa sisi hatuna. Kama sisi hatuna restriction basi ni sawa madereva wao kuingia kwetu bila kupimwa, lakini hatuwezi kudai kuwa na madeeva wetu waingie kwao bila kupimwa!

KUmbuka kwamba madereva wa Kenya wakitoka Tanzania wanaporudi kwao wanawekwa quarantine - sasa kama wanafanya hivyo kwa madereva Wakenya, kwa nini tuone sio sawa wakisema madereva wa Tanzania wawekwe quarantine?

Ona pia thread hii:

Tunaweza kuona tuna msimamo imara suala la Corona lakini mwishoni gharama yake inaweza kuwa Tanzania kukosa heshima na kupoteza urafiki na nchi jirani
 
Tatizo nadhani linakuja hapa.

Nafunga mpaka upande mmoja, bila kuingia mezani na jirani ili kujua ni hatua gani tuchukue kwa pamoja kuweka mambo sawa.

Unaweza kuwa upo sawa kulinda wananchi wako, ila jirani nae anaweza kuja hoja yake.

Kwa hivyo ilipaswa wawasiliane kwanza wahusika.

Ukiacha kila mtu afanye kivyake ndio hii mikorogano tunayoshuhudia leo hii.
 
Endelea kujiuliza zaidi,ni hivi, watanzania hawana shida na kupimwa.,ispokuwa wakenya wanatumia mwanya huo kutuhujumu kiuchumi ,sasa acha mbwai na iwe.mbwai,hongera zake RC Shigela

Sent using Jamii Forums mobile app
Jibu kwanza. Mimi naona Tanzania tunatia aibu sasa. Mara Rwanda, mara Uganda, mara Zambia, mara Kenya. Hivi tuna akili gani sisi? KIla jirani tunagombana nae?
 
Kila mtu akae kwake, mizigo ifaulishwe mpakani, hakutakuwa tena na malalamiko ya nchi moja inaambukiza nchi nyingine.
 
Tatizo nadhani linakuja hapa.

Nafunga mpaka upande mmoja, bila kuingia mezani na jirani ili kujua ni hatua gani tuchukue kwa pamoja kuweka mambo sawa.

Unaweza kuwa upo sawa kulinda wananchi wako, ila jirani nae anaweza kuja hoja yake.

Kwa hivyo ilipaswa wawasiliane kwanza wahusika.

Ukiacha kila mtu afanye kivyake ndio hii mikorogano tunayoshuhudia leo hii.
Mkuu, kumbuka walipotualika tukae mezani tupange mkakati pamoja tuliwatolea nje. Sasa wanaweka uratibu kwenye nchi zao tunakuja juu. Kama huo sio uendawazimu wa viongozi wetu ni nini hasa? Vitu vingine bwana ni sisi tuna matatizo!
 
Vitu vingine tusijifanyw kuwa wajuaji na kukorofishana na jirani zetu pasipo sababu. Hatuwezi kuwalazimisha wasiwe na restrictions za Corona kwa kuwa sisi hatuna.
TZ tunataka na majirani wawe kama sisis bila strict observances /restrictions. hata watu wakiwa positive waachwe waingie, ni coronavirus ni mafuta yatayeyuka
 
Hapa kuna " bifu" kubwa sana,ni vyema ili bifu likashughulikiwa mapema kabla alijaleta majanga makubwa zaidi.

There's no truth in this world.
 
Halafu huyu Mkuu wa Mkoa wa Tanga anasema eti anashangaa Rais wa Kenya anaitwa Uhuru lakini hawaruhusu Wakenya kuwa huru na Corona, wakati wa kwetu anaitwa Magufuli lakini kawaondolea Watanzania makufuli ya Corona. Hivi kama huu si utaahira ni nini basi?

Na huyu ndio tumeona ana akili ya kuwa Mkuu wa Mkoa anaongea utumbo kama huu halafu anajisifia mimi ni mkuu wa mkoa lazima nilinde maslahi ya Tanzania?

Kwa point kama hizo hafai hata kuwa Balozi wa nyumba kumi.
 
Endelea kujiuliza zaidi,ni hivi, watanzania hawana shida na kupimwa.,ispokuwa wakenya wanatumia mwanya huo kutuhujumu kiuchumi ,sasa acha mbwai na iwe.mbwai,hongera zake RC Shigela

Sent using Jamii Forums mobile app
Tafadhali mkuu,hebu rudia tena kusoma labda utamuelewa mtoa mada.maana naona kama umepanic
 
Back
Top Bottom