Ninachoshindwa kuelewa ni kwamba Tanzania wanataka madereva wa Tanzania wasipimwe wanapoingia Kenya au hata wakiwa positive waingie?

Mkuu mbona hiyo ni simple logic, kama hutaki mi nifike kwako basi we usije kwangu

MONEY STOP NONSENSE
Huo ndio utoto ninaosema tunao, sisi na viongozi wetu. Na Kenya hawajasema msiende kwao, wamesema msiingie kwao ikiwa mtapimwa mkaonekana mna Corona. Mnachokataa hapa ni kwamba hamtaki mpimwe kwa kuwa sisi hatuwapimi madereva wao. Sasa tusilazimishe utaratibu wetu uwe wao.
 
Ungefanya research kwanza kabla ya kuandika huu uzi ungekuwa umefanya la maana. Acha kudandia gari kwa mbele. Nenda horohoro ukaangalie hali ilivyo ujue undani wa hili swala.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na wewe uko Horohoro sivyo ndio maana unajua unachosema? Ila naona umesema nenda Horohoro, sio njoo!
 
wewe ujaelewa.hii ni vita ya kiuchumi kwa kusingizia corona.
embu fatilia kwa kina utafahamu tu.
na unaona ni tanzania tu ni kwa sababu tanzania ni chem chem ya neema inanyeshea nchi zoote za jirani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tupe sababu za kisayansi mmefanya nini hadi kufikia mkataa kuwa vipimo vya Kenya haviaminiki. Na haviaminiki kwa Watanzania pekee?

kuna wale madereeva walipimwa uganda wakakutwa hwana then same same people wakapima kenya wakakuta wanaoa: i think kuna battle apa sio siri
 
wewe ujaelewa.hii ni vita ya kiuchumi kwa kusingizia corona.
embu fatilia kwa kina utafahamu tu.
na unaona ni tanzania tu ni kwa sababu tanzania ni chem chem ya neema inanyeshea nchi zoote za jirani

Sent using Jamii Forums mobile app

hata marekani saaahv anamshtumu china na yeye china anasema marekani anahusika kutengeneza hiki kirusi, cha ajabu sisi tunajua kwamba huu ugonjwa umetokea wuhan kwenye soko la wanyama kumbe kuna vita ingine chini kwa chini
 
Mkuu JF wakati fulani ilikuwa na watu kama wewe na ilifurahisha kujadili mada.Tulikwa hata na mawaziri tukaongea mambo ya msingi kwa nchi yetu. Kisha wakaingia wana JF yeboyebo mambo yakaharibika! Utagundua kuwa kuna wana JF wengine waliamua kujitoa kwa sababu ya huu uvamizi.
 
Bora shule zifunguliwe,kaa kimya kuficha upumbafu wako.
 
Tunafunga mipaka kwa gari zote kutoka kenya kuepuka korona... Sasa sijui unataka nini? Unaumia nini? Walipotuzuia wao si mlisema wapo sahihi wanalinda nchi yao? Kwahyo sie tusilinde yetu?

Dunia ya leo ukimwaga ugali watu wanamwaga mboga, sasa tuone nani atataka tukae chini wayamalize.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii hali isiposuluhishwa haraka kwa njia za kidiplomasia, EAC ina hatari ya kuvunjika.. na kuja kuungana tena itachukua Muda sana.

MÊmENtO HoMO
 
Sasa povu la nini, wamefunga mipaka nasi tumefunga... Gari za zambia, ugandq, vongo nk ruksa. Kasoro kenya hatuwataki sababu ya korona nini shida yako? Inauma ehee!!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee inasikikitisha sana, badala ya watu hawajadili hoja hata wakatae tu, Ila wanatukana..@moderator sijui nao vip
 
Kwanini waweke lockdown?,hii Ni dharau kwa umoja wa East Africa,ilitakiwa tuwe na msimamo mmoja tu,,msimamo wa Tanzania ndio sahihi hakuna lockdown,full stop,,kwahiyo madereva wetu wasipimwe na mtu,kwanza vipimo Ni fake,😔😔
 
Mkuu

Wakwetu Katk hili hatak kukaamezani na yeyote.. Wamemtafta Sana lkn Hataki

Sent from my TECNO_W4 using JamiiForums mobile app
 
Si mliitwa kwenye kikao cha EAC Mkaingia mitini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…