Ninamjibu Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu kuhusu kuwapongeza viongozi wa Tanga kwa kutogombana

Ninamjibu Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu kuhusu kuwapongeza viongozi wa Tanga kwa kutogombana

Standards Person

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2021
Posts
672
Reaction score
860
Bila kuwachosha wanajukwaa nitaandika kwa kifupi sana. Juzi waziri wa Tamisemi na mbunge wa Tanga alikuepo jimboni kwake. Kupitia mitandao ya kijamii nimeona eti akiwapongeza viongozi Tanga kwasababu hawagombani.

Naomba nimwambie hawagombani kwasababu lao ni moja (kuinyonya Tanga). Unadhani mtu kama Anthony Mtaka au Yule RC Mwanza, Geita, ambae hajulikani kwani hatatui kero za wananchi. Au Takukuru waliolala wakati mji unafwonzwa? Halafu eti mbunge kabisa unasifiatu kutogombana.

Ummy anajua kabisa kwamba mkurugenzi anaingilia michakato ya ujenzi na anatuhumiwa kwa rushwa. Anajua wapo watumishi waliofukuzwa kazi na wake zao wanachukuliwa hapo halmashauri. Anaijua tuhuma ya rushwa ya ngono anajua watumishi waadilifu walivyonyanyasika.

Ndani ya halmashauri kama sio mpigaji unaambiwa kabisa kwa usalama wako hama ukikataa utatengenezewa zengwe ufukuzwe kazi. Ummy anajua bali anajitoa ufahamu. Ninaomba sana kwa Mungu Mh. Rais amuondoe Ummy kwenye uwaziri maana anafanya upendeleo anaondoa wakurugenzi wa halmashauri nyingine halafu kwake kumeoza.

Amewaondoa kazini kwa hoja kwamba wananchi wamelalamika. Atupe utaratibu wa kulalamika kama ni barua tuandike kwa katibu mkuu au popote.

Ummy anajua watu wameporwa viwanja na wengine maboma yao. Watu wameingiza maji na wanalipia lakini kiwanja kinauzwa kuna kesi za ardhi lukuki leo unawachekea chekeatu, kwanini? Ni ubabe wao au aliwatuma? Ummy hana huruma na wananchi wake. Wenye huruma na wananchi akina Sele Bosi hawatakiwi ndani ya halmashauri na wakamfanyia fitna asiingie kwenye umeya.

Ummy anawatetea kwa kua anaona wamemuweka ninamwambia kama Mungu akimtia tamaa ya kuomba tena ubunge hawatakuepo hao hapo ndio ataelewa kama dunia duara. Atawafuata wamsaidie kampeni? Hakuna kiongozi yoyote kutoka tanga atakae mlalamikia mkurugenzi aliepo kwani lao nimoja.

Ummy aondolewe kwenye uwaziri kwa maendeleo ya wanatanga maana anafanya upendeleo.
 
Kwani yeye ummy anasemaje
Anataka waendelee kuchapa kazi hivyohivyo. Wazidi kupendana. Yeye kwake anaona kuelewana ndio kunaleta maendeleo. Hajajua kama urafiki mwingine hauna afya kwa taifa. Hajui kwamba tege wafananao huruka pamoja. Hata yeye anafanana nao ndio maana wanaelewana. Akivuliwa uwaziri atahaha sana na akili itamkaa sawa
 
Anataka waendelee kuchapa kazi hivyohivyo. Wazidi kupendana. Yeye kwake anaona kuelewana ndio kunaleta maendeleo. Hajajua kama urafiki mwingine hauna afya kwa taifa. Hajui kwamba tege wafananao huruka pamoja. Hata yeye anafanana nao ndio maana wanaelewana. Akivuliwa uwaziri atahaha sana na akili itamkaa sawa
🙏🙏🙏
 
.... Anajua wapo watumishi waliofukuzwa kazi na wake zao wanachukuliwa hapo halmashauri. Anaijua tuhuma ya rushwa ya ngono anajua watumishi waadilifu walivyonyanyasika.
Wacha watu wapenziane buana.... si tunaambiwa tanga ndio mapenzi yalikozaliwa!?
Au nakosea ndugu yangu

Ummy aondolewe kwenye uwaziri kwa maendeleo ya wanatanga maana anafanya upendeleo.
Hili sahau kabisa mkuu
 
Asipotenda haki ataondolewa,aendekee kujitia uziwi na upofu. Kama mtangulizi wake alielezwa akawa anachekea wazembe akaharibu yeye aachwe kawa nani? Asipotenda haki hapo hatadumu hakika nakuambia.
 
Tatizo ni kwamba nguzo za mawaziri sita wanao tegemewa na utawaala wa Mama na ummy yumo.....hapo ungelalamikiwa mfumo mzima wa ccm wa kuteua ma waziri, kinacho hitajika ni professional ministers kwenye wizara husiku sio kuteua wanasiasa watii wa chama.
 
Tatizo ni kwamba nguzo za mawaziri sita wanao tegemewa na utawaala wa Mama na ummy yumo, hapo ungelalamikiwa mfumo mzima wa ccm wa kuteua ma waziri, kinacho hitajika ni professional ministers kwenye wizara husiku sio kuteua wanasiasa watii wa chama.
Wapo waliokua wameaminiwa kuliko hata yeye. Walikuepo akina Kitwanga,Muhongo,Ngeleja,Makamba,Nchimbi nk huyo yupoyupo kwa kubebwatu hata jukwaani hamna kitu.

Hawezi kuifikia imani ya Mh. Lowassa huyo ndani ya ccm hata kwa theluthi.

Ninasema ataondoka Tamisemi na atakua muuliza maswali na mchangiaji kama huamini utaiona nguvu ya Mungu. Hawezi kuungana na mkandamizaji halafu akabarikiwa. Mama yetu nae hataki unafiki na tuone muda utasemaje.
 
Watu walishalalamika sana. Hata hapa jukwaani alishaandikiwa Jafo uozo unaofanywa na viongozi ikiwemo kulinda wezi na kunyanyasa watumishi waadilifu.

Mkurugenzi huyo alishalalamikiwa hata kwenye vyombo vya habari kwa Lemutuz pia wanaharakati walienda. Jafo alimlinda huyo mbadhirifu na mnyanyasaji.

Waitara pia aliambiwa kwa kuandikiwa barua lakini wote hawakuchukua hatua. Tanga niyamkurugenzi haina mwenyewe
 
Ummy ni kama mama kilango tu, akiwa mkuu wa mkoa wa SHINYANGA alidai mkoa wake hauna wafanyakazi hewa kumbe wapo kibao. Hawa mawazir wanashida Sana.
Alikua wakwanza kutangaza kwamba Shinyanga haina mtumishi hewa hata mmoja,hayati akamzingua. Kweli wamekua sawasawa nae yatamkuta
 
Back
Top Bottom