Ninamuhitaji mwanaume (hiv+)

Ninamuhitaji mwanaume (hiv+)

Wengi wanakutakia mafanikio hata mimi nakutakia ufanikiwe, Allal akufanyie wepesi.
 
life is an interesting safari utapata tu unachohitaji.kila la kheri
 
Salam wana JF. Mimi ni mwanamke mwenye umri miaka 48 ambaye naishi na VVU natafuta mwanaume wa kuishi nae au kufunga ndoa, kama yupo tayari. Awe na umri kuanzia miaka 50-55, kwa ufupi nilikuwa na mume ambae nilimuamini na kumpenda sana yeye ni mfanyabiashara nje na ndani ya nchi baada ya miaka 4 alianza mabadiliko ya kutowasiliana tena na mimi. Mwaka uliofuta nilipata mchumba na tulihitaji kufunga ndoa nikaona niende ANGAZA kuangalia afya yangu lakini haikuwa siku nzuri kwangu kwani nilijikuta nimeshapata maambukizo sikuwa na jinsi. Nilimuomba Mungu katika sala zangu anisaidie na kunitia nguvu katika maisha yangu ya upweke. Kwa vile nimezoea kuwa na mwenzangu kuishi peke yangu ni vigumu kwangu, nami naomba kujitokeza mimi nipo katika ukweli (serious) na tutalindana.
i wish you all the best and don't forget to pray to Jesus because through him everything is possible as Jesus say if you ask anything in my name,i will do it John 14:14
 
Kila mtu anastahili kuwa na furaha...kuwa hiv+ siyo mwisho wa dunia. Nimefurah kuwa unatafuta mwenza muendeleze gurudumu la maisha...keep the spirit mpenz....all the best.....
 
Sweety mpendwa.... Engeza imani na dose za " Astagh FirruLLaah " full time muradi wako utajibiwa. AMIN pamoja
 
Pole sana Sweet Juma, naheshimu mawazo yako lakini ningependa kukupa ushauri, ''Kwa kuwa wewe umejieleza kwa kina, basi ungetoa nafasi kwa mwanaume yeyote mwenye HIV na asie na HIV ilimladi atimize vigezo vingine. Mapenzi yana nguvu kushinda nguvu uzijuazo, pengine bahati yako ipo kwa asie na maambukizi.'' Elimu juu ya VVU kwa kiasi kikubwa imesaidia jamii kuondokana na fikra potofu.
 
Hata asiye Muathrika anaweza akakuoa Tu, kwani Kuna DisCordant Couple kama 5% mke Mwathrka bur dume mzima au vise versa, mhimu Jipange tu utampata
 
Hongera sana mama kwa moyo wako mwema wakuto kuambiza wengine na kutafuta mme mwenye hali inayo lingana na wewe. kwa sababu wewe ni mwema mungu atakupa mme mwema.ukiwa mkweli utaijua kweli na utampata mtu mkweli na utakuwa huru na utapata mafanikio makubwa . hata kama umepata maambukizi malengo yako ya kumpata mme bora yatatimia na furaha yako itaongezeka zaidi.
 
unadhani wewe ni fundi sana wa kutukana,ewe kibwengo?...chunga domo lako bana.

ujumbe umekufikia,ingekuwa vema ukatembea ktk maneno yako,tafadhari tu usilete dhihaka kwa mdada wa watu anachohitaji ni faraja ktk hali aliyonayo na siyo kuleta masihara
 
Mungu akusaidie upate hitaji la moyo wako, najua wahusika kulingana na vigezo vyako wapo wengi na huenda umekwishapokea PM.

All the best Sweety Juma
 
Last edited by a moderator:
endelea kumuomba mungu atakupa ukitakacho usijali na pole sanaaaaaaaaah!
 
Back
Top Bottom