Ninaogopa endapo Othman Masoud na Ismail Jussa wataamua kumjibu Tundu Lissu wa CHADEMA kuhusu Katiba ya JMT ya 1977 na Katiba ya Zanzibar ya 1984!

Kwanini hizo zote hazikuweza kuwashwishi wenye madaraka kuunda Muungano wa Seriali 3

..mabadiliko yanaweza yasi-guarantee Ccm kuendelea kuwa madarakani, au yanaweza kupunguza nguvu yao kwa kiwango kikubwa.

..binafsi naamini kuna mambo Ccm hawataki yaangaliwe, au yashughulikiwe, na mtawala asiyetokana na chamaa chao.

..kwa hiyo huenda Ccm ikang'ang'ania serikali mbili, na katiba ya 1977, kwa muda mrefu mpaka pale pressure itakapokuwa kubwa kupita kiasi.
 
Huu muungano hauna maana.
 
Hatuutaki muungano!!
 
Ndani ya katiba pendekezwa kuna muungano wa serikali tatu?
 
Hao wananchi wengi unaowaongelea hapa wanaopenda huu Muungano umewapata wapi au kwa takwimu gani? Kwa upande wa Tanganyika hakuna mwananchi wa kawaida anayeweza kueleza faida ama binafsi au ya kitaifa inayomnufaisha yeye zaidi ya viongozi na chama cha tawala. Huko zanzibz ndiko usithubutu kuuliza faida kwao hawataki kabisa.

Ccm na serikali waruhusu uamuzi wa kura ya maoni juu kuendelea kwa Muungano huu au muundo wa Muungano halafu ndipo utakuwa na uhalali wa kuwasemea hao wananchi.
 
Ndani ya katiba pendekezwa kuna muungano wa serikali tatu?

..kuna serikali 2.

..ni dhana potofu kusema Ukawa walikwamisha mchakato wa katiba.

..ukawa hawakuwa na wajumbe wa kutosha ktk bunge maalum kuweza kukwamisha mchakato.

..vikao vya bunge maalum viliendelea mpaka zoezi la kuandika katiba pendekezwa lilipokamilika.

..inastaajabisha kwamba Ccm wameachana na katiba pendekezwa ambayo waliiunga mkono.
 
Siasa zetu zina ujinga, uongo, ujuha, upumbavu na mengine yanayofanana na hayo. Tunajenga jamii na taifa la namna gani?
Lazima lifanyike jambo ili tuwe na watu wakweli, waadilifu na wenye weledi kwenye siasa kwa mustakabali mwema wa jamii na taifa kwa ujumla.
Na hii ndiyo kazi ya kipaumbele kwa TISS. Au nao ni kama habari ya yai na kuku.
 
Muungano haufi ila watu waachwe waujadili kwa kina, hayo machache tu aliyoyaibua Lissu yamewaamsha wengi - yaani ni kama kachoma kuni mbichi ndani ya shimo..
Muungano unaolindwa na viongoz wachache wa ccm utakufa tu one day,huu muungano ni fake na haujawah kupata baraka za wananchi kupitia kura ya maoni,ni muungano wa Nyerere na Karume
 
umejuaje kama alishindwa kumshauri Mwenyekiti? Mtu akishauriwa anaweza kuupokea ushauri au la, kwa hivyo hiyo imebaki kama ni theory tu, na hasa kwamba uamuzi siyo wa mtu mmoja peke yake hata kama alikuwa Waziri.
 
Jibu sasa wewe hapo
 
Yeye mwenyewe hajui anafanya nini na anatakiwa kufanya nini
 
Huo muungano ni wa viongozi wa ccm. Hauna chochote cha maana kwa wananchi wa kawaida

Muungano ulianzishwa kwa ombi la Wamarekani, kwa faida walizozijua wao.

Mzee Henry Kissinger, ambaye alishiriki kuutengeneza huu Muungano, bado yupo hai, wataalam wa Hostoria, kaongeani naye, akawape ABC ya Muungano.

Kwa sasa muundo w Muungano urekebishwe ili uwe na tija kwa pande husika. Hofu waliyokuwa nayo Wamarekani wakati ule, sidhani kama bado ipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…