Ninaomba tafsiri ya ndoto hii

Ninaomba tafsiri ya ndoto hii

Mama Mwana

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2023
Posts
2,435
Reaction score
7,784
Hamjambo,

Usiku wa kuamkia leo nimeota nipo kwenye mji mwingine, ni kama "lost city" ambapo hakuna mtu lakini majengo yake ni makasri, kama yale kwenye filamu za katuni, mfano jengo la Disneyland.

Nimeota hayo majengo ni chakavu, na nje kuna sanamu za farasi aliyepandwa na mtu akiwa amenyanyua miguu ya mbele kana kwamba anakwenda mbio. Ni kama kuna anayenikaribisha lakini simwoni, nikajiuliza, hapa ni wapi? Nafanya nini hapa? Kwa nini niko hapa?

Nilipoangalia juu, nikaona mbingu ni kama kioo, na ndani yake kuna buibui mkubwa mfano wa nyumba, akitembea na vitu vya ajabuajabu. Nilihisi kuchanganyikiwa. Hayo yote yalikuwa ndotoni, lakini kiuhalisia nilikuwa naweweseka. Mtu niliyelala naye ndiye aliyeniambia leo usiku nimeota na kuweweseka sana.

Nimejaribu kutafakari maana yake, kwani ndoto zangu zimekuwa zikihusiana na matukio ya kweli. Kuna kitu kinaniambia natakiwa kuelewa maana yake. Je, kuna yeyote anayeweza kunisaidia tafsiri ya ndoto hii?
 
Roho yako ( nakosa lugha nzuri ya kumtumia ) moja huna nguvu za rohoni, na mbili roho yako inaweza kusafiri from one location to another. Roho yako imesafikiri na kuingia kwenye territory ambayo inaweza ( ina atahri kwenye roho yako ). Roho yako imejikuta Kuta hapo kwasababu inatanga Tanga na imeingia kwenye territory ambayo sio safe kwako
 
Hii ndoto ni genuine kabisa,haina maana yoyote.

Chukulia tu ni kwamba ulichoka vizuri na umelala vyema,ni sawa na ungeota umeenda kuvuna mahindi halafu akatokea samaki mkubwa anapiga ngoma kisha wamama wanacheza wakimtupia punje za mchele.
 
Ukiiota usiwaze sana andika chini unayokumbuka kisha omba muendelezo
 
Duh ndoto moja ya karama sana naona mwili wako hujaguswa kabisa na wabaya.
Elewa hivi ni ndoto kubwa mno na haifai hata kuwaambia watu..
Nashindwa namna ya kukueleza..ishia kuelewa hivo.
sasa unanitishia au unanipa taarifa?
 
Ndoto ni nadhani inayo kosa uhalisia, ndoto na imani za kidini hamna tofauti.
Chukulia kawaida tu focus kwenye mambo mengine ya uhalisia .
sawa, kwa sababu mm n miongoni mwa watu ambao mostly ndoto tunazoota huwa hivohivo au kuna taarifa flan au msg naletewa sasa bora iwe kweli lakini kwa hilo kasri farasi na huyo buibui juu sjui ngoja nipuuzie
 
Hii ndoto ni genuine kabisa,haina maana yoyote.

Chukulia tu ni kwamba ulichoka vizuri na umelala vyema,ni sawa na ungeota umeenda kuvuna mahindi halafu akatokea samaki mkubwa anapiga ngoma kisha wamama wanacheza wakimtupia punje za mchele.
sawa
 
Roho yako ( nakosa lugha nzuri ya kumtumia ) moja huna nguvu za rohoni, na mbili roho yako inaweza kusafiri from one location to another. Roho yako imesafikiri na kuingia kwenye territory ambayo inaweza ( ina atahri kwenye roho yako ). Roho yako imejikuta Kuta hapo kwasababu inatanga Tanga na imeingia kwenye territory ambayo sio safe kwako
ungejua hata namna ya kutoka nje ya mwili sjui namna gan inafanywa inakosaje utulivu? mh haya
 
ungejua hata namna ya kutoka nje ya mwili sjui namna gan inafanywa inakosaje utulivu? mh haya
Ipo hivi, unapolala, mwili una zima na roho inakuwa active. Roho inapokuwa na nguvu inakuwa na control na mazingira na roho ikiwa Haina nguvu inakuwa haina control na mazingira, kuna Ile MTU kupitia ulimwengu wa ndoto anaitwa na wachawi au roho ovu unakuta anaenda, na kuna Ile MTU anaitwa na roho ovu ila haendi.. ndio kama wewe Sasa hapo.. umeenda sehemu ambayo haitakiwi huende.. maana yake roho yako Haina nguvu.. sio swala unajua kutoka mwilini au hujui.. kitendo Cha kulala huwa kinafanya hilo by default.. ila uki mature ku exercise rohoni inaweza ukawa unafanya utakapo
 
Hamjambo,

Usiku wa kuamkia leo nimeota nipo kwenye mji mwingine, ni kama "lost city" ambapo hakuna mtu lakini majengo yake ni makasri, kama yale kwenye filamu za katuni, mfano jengo la Disneyland.

Nimeota hayo majengo ni chakavu, na nje kuna sanamu za farasi aliyepandwa na mtu akiwa amenyanyua miguu ya mbele kana kwamba anakwenda mbio. Ni kama kuna anayenikaribisha lakini simwoni, nikajiuliza, hapa ni wapi? Nafanya nini hapa? Kwa nini niko hapa?

Nilipoangalia juu, nikaona mbingu ni kama kioo, na ndani yake kuna buibui mkubwa mfano wa nyumba, akitembea na vitu vya ajabuajabu. Nilihisi kuchanganyikiwa. Hayo yote yalikuwa ndotoni, lakini kiuhalisia nilikuwa naweweseka. Mtu niliyelala naye ndiye aliyeniambia leo usiku nimeota na kuweweseka sana.

Nimejaribu kutafakari maana yake, kwani ndoto zangu zimekuwa zikihusiana na matukio ya kweli. Kuna kitu kinaniambia natakiwa kuelewa maana yake. Je, kuna yeyote anayeweza kunisaidia tafsiri ya ndoto hii?
Tafuta mtumishi wa Yesu Kristo mweleze akufanyie maombi inaonekana nafasi yako inatekwa kichawi na kupitishwa kwenye mashimo ya uharibifu. Hasa ni chini ya maji kwenye miji ya kipepo. Fanya ukombozi haraka kwani mambo haya yanaweza kuambatana na anguko kiuchumi, na mambo yako mengine.
 
Back
Top Bottom