Ninapitia msongo mkali wa mawazo baada ya kusimamishwa kazi kisa vyeti feki. Naomba ushauri niweze kujikwamua

Ninapitia msongo mkali wa mawazo baada ya kusimamishwa kazi kisa vyeti feki. Naomba ushauri niweze kujikwamua

Pole sana dearest......

Maybe naomba niulize umesema una dip ya education na ulitumia majina ya mtu hapo imekaaje au ndo ile unauziwa jina kuanza form one? Km hukufanya vzr ? Nieleweshe
Asante sana kipenzi.
Hapana, ni kwamba niliuziwa cheti cha mtu aliyemaliza form 4 nikaenda nacho kusomea ualimu ngazi ya certificate na diploma kwa kutumia jina lake.
Kipindi hiko mimi nilikuwa nimemaliza kidato cha nne miaka kama 3 iliyopita na cheti changu kilichomwa moto na msichana wetu wa kazi.
Hivo nilipanda na jina lake mpaka kufikia ngazi ya diploma (katika kujiendeleza) ndipo nikatumbuliwa hukohuko.
 
Pole sana Miss Natafutwa nashindwa hata namna ya ku kushauri. Lakini zingatia sana kuwa ni mtu wa shukrani kwa kila jambo.

Maisha siku zote hayawezi kwenda vile unavyotarajia. Nakumbuka habari ya Dada wa Mariah Carey alipata mpaka ugonjwa wa ukimwi kwa sababu ya changamoto kama ulizo nazo wewe lengo ni kupambana na haya haya maisha.

Pole sana endelea kuwa na uvumilivu.
 
Habari wana Jf kwa ujumla.
Sina muda mrefu tangu nijiunge na jumuia hii chini ya kaka Max.

Ni hivi, napitia msongo mkali sana wa mawazo yaani nikisema ni mkali namaanisha.

First of all nilikuwa muajiriwa serikalini na likapita suala la vyeti feki hapo nilikuwa natumia cheti cha mtu na kazi ikawa ndio basi.
Sababu nilipoteza wazazi ikabidi ile akiba niliyojiwekea kipindi nafanya kazi niitumie kwa ajili ya kumsomesha mdogo wangu ambae niliachiwa na wazazi pamoja na kununua kiwanja tu.

Hali ikazidi kuwa mbaya zaidi, ikabidi niingie kwenye kazi ya kujiuza.
Nilichokuwa nafanya ni kumuandalia mdogo wangu sare za shule na pesa ya matumizi usiku ili hata kama nitarudi asubuhi au kama sitarudi kabisa basi apate kujiandaa na kwenda shule (shule na nyumbani ni kama km 1 tu) mwenyewe.
Nilifanya hiyo kazi kwa miaka 6, nikapata pesa na kuanza ujenzi wa nyumba yangu ya kuishi pamoja na mdogo wangu.

Shida imeanza tena, nyumba haijakamilika na pesa zote nimemaliza na mdogo wangu mwaka huu anaingia kidato cha 3.
Sitaki tena kurudi kule nilipotoka (kujiuza).
Nahitaji mdogo wangu akue bila kujua nafanya nini.
Pia nahitaji kumalizia nyumba

Kama kuna mtu ana uhitaji wa mtu wa kufanya kazi naomba nipewe ajira.
1. Nina diploma ya Education niliyoipata pale UDSM kabla sijatumbuliwa.

2. Nina uzoefu katika kulea watoto na pia ninajua sana upishi (nilisomea hotel management kabla sijaenda kusomea ualimu)
Umri wangu ni miaka 42 na niko Morogoro.
Asanteni.
Rais Samia aliwapa kiinua migongo wafanya kazi feki,wewe hukupewa? Kama ulifanya kazi Kwa miaka SITA namimi ulilipwa zaidi ya 10M ulipeleka wapi?

Si kweli uyasemayo hapa
 
Habari wana Jf kwa ujumla.
Sina muda mrefu tangu nijiunge na jumuia hii chini ya kaka Max.

Ni hivi, napitia msongo mkali sana wa mawazo yaani nikisema ni mkali namaanisha.

First of all nilikuwa muajiriwa serikalini na likapita suala la vyeti feki hapo nilikuwa natumia cheti cha mtu na kazi ikawa ndio basi.
Sababu nilipoteza wazazi ikabidi ile akiba niliyojiwekea kipindi nafanya kazi niitumie kwa ajili ya kumsomesha mdogo wangu ambae niliachiwa na wazazi pamoja na kununua kiwanja tu.

Hali ikazidi kuwa mbaya zaidi, ikabidi niingie kwenye kazi ya kujiuza.
Nilichokuwa nafanya ni kumuandalia mdogo wangu sare za shule na pesa ya matumizi usiku ili hata kama nitarudi asubuhi au kama sitarudi kabisa basi apate kujiandaa na kwenda shule (shule na nyumbani ni kama km 1 tu) mwenyewe.
Nilifanya hiyo kazi kwa miaka 6, nikapata pesa na kuanza ujenzi wa nyumba yangu ya kuishi pamoja na mdogo wangu.

Shida imeanza tena, nyumba haijakamilika na pesa zote nimemaliza na mdogo wangu mwaka huu anaingia kidato cha 3.
Sitaki tena kurudi kule nilipotoka (kujiuza).
Nahitaji mdogo wangu akue bila kujua nafanya nini.
Pia nahitaji kumalizia nyumba

Kama kuna mtu ana uhitaji wa mtu wa kufanya kazi naomba nipewe ajira.
1. Nina diploma ya Education niliyoipata pale UDSM kabla sijatumbuliwa.

2. Nina uzoefu katika kulea watoto na pia ninajua sana upishi (nilisomea hotel management kabla sijaenda kusomea ualimu)
Umri wangu ni miaka 42 na niko Morogoro.
Asanteni.
Mungu akufungulie milango ya mibaraka 🙏
 
Ndugu yangu ninakuombea mungu ni mwema sana najua unapitia changamoto kali sana ningekuwa na uwezi ningekusaidia mpendwa lakini ndio ivyo ila nina Imani jamiiforum ni uwanja mpana sana nina Imani utapata msaada kupitia jukwaa ili watu watakushika mkono🙏🏽
Asante sana mpendwa, nashukuru sana.
Nina imani wenye uhitaji watanisikia na kunishika mkono.
Nashukuru sana.
Ni changamoto tu za dunia, nina imani zina mwisho.
Asante sana
 
Asante sana kipenzi.
Hapana, ni kwamba niliuziwa cheti cha mtu aliyemaliza form 4 nikaenda nacho kusomea ualimu ngazi ya certificate na diploma kwa kutumia jina lake.
Kipindi hiko mimi nilikuwa nimemaliza kidato cha nne miaka kama 3 iliyopita na cheti changu kilichomwa moto na msichana wetu wa kazi.
Hivo nilipanda na jina lake mpaka kufikia ngazi ya diploma (katika kujiendeleza) ndipo nikatumbuliwa hukohuko.
Huu ni uongo.

Kwanza, kinachomata haswa ni index number ya kidato cha nne. Cheti huwa ni nyongeza tu baadae, hapa nazungumzia katika mchakato wa kuomba vyuo, nk.

Lakini pia, ukichoma cheti ama kukipoteza kwa bahati mbaya, utaratibu upo very clear. Omba loss report, andika barua kwenda NECTA, watakutengenezea cheti kingine.

Kudai ulitumia cheti cha mtu kwa sababu chako ulichoma ni upuuzi usio na mantiki.
 
Kwa nini uliacha kujiuza?

Je, ulipata hela za kutosha au ni vipi?

Kwa uamuzi wako wa kuweka kila kitu hapa, ukisema uliwahi kujiuza NA SASA HUTAKI TENA KUJIUZA, umeamua kutafuta kazi.

Huoni kama waajiri wako wanaweza kukusumbua?(Maana past yako inajulikana)

Je huoni kama watu watakutafuta wakiwa na lengo Lao la kificho, wakijaribu kukushawishi kwa hiyo kazi?

Dada, ulikua unajiuza, na kwa bandiko lako hili, muda si mrefu utarudi katika kujiuza hata kama hupendi. Maana hakuna namna, hakuna mwanaume atakutafuta akusaidie kazi tu peke yake behind atakua na interest zake na hiyo ni kwa sababu umewapa past yako.
 
Back
Top Bottom