Habari wana Jf kwa ujumla.
Sina muda mrefu tangu nijiunge na jumuia hii chini ya kaka Max.
Ni hivi, napitia msongo mkali sana wa mawazo yaani nikisema ni mkali namaanisha.
First of all nilikuwa muajiriwa serikalini na likapita suala la vyeti feki hapo nilikuwa natumia cheti cha mtu na kazi ikawa ndio basi.
Sababu nilipoteza wazazi ikabidi ile akiba niliyojiwekea kipindi nafanya kazi niitumie kwa ajili ya kumsomesha mdogo wangu ambae niliachiwa na wazazi pamoja na kununua kiwanja tu. Hali ikazidi kuwa mbaya zaidi, ikabidi niingie kwenye kazi ya kujiuza.
Nilichokuwa nafanya ni kumuandalia mdogo wangu sare za shule na pesa ya matumizi usiku ili hata kama nitarudi asubuhi au kama sitarudi kabisa basi apate kujiandaa na kwenda shule (shule na nyumbani ni kama km 1 tu) mwenyewe.
Nilifanya hiyo kazi kwa miaka 6, nikapata pesa na kuanza ujenzi wa nyumba yangu ya kuishi pamoja na mdogo wangu.
Shida imeanza tena, nyumba haijakamilika na pesa zote nimemaliza na mdogo wangu mwaka huu anaingia kidato cha 3.
Sitaki tena kurudi kule nilipotoka (kujiuza). Nahitaji mdogo wangu akue bila kujua nafanya nini. Pia nahitaji kumalizia nyumba
Kama kuna mtu ana uhitaji wa mtu wa kufanya kazi naomba nipewe ajira.
1. Nina diploma ya Education niliyoipata pale UDSM kabla sijatumbuliwa.
2. Nina uzoefu katika kulea watoto na pia ninajua sana upishi (nilisomea hotel management kabla sijaenda kusomea ualimu), Umri wangu ni miaka 42 na niko Morogoro.
Asanteni.
Umenikumbusha mbali saana.
Nimewahi kuishi morogoro miaka hiyo, siku moja Kuna kaka angu alikuwa anatokea Kagera ikabidi anipigie simu na kuniambia kuwa watalala morogoro kwahiyo niende msamvu kumsalimia maana ni muda mrefu tumepotezana.
Ikabidi nitoke chuko kwenye saa 4 hivi nikaenda msamvu, miaka hiyo kabla ya stend mpya mle ndani mlikuwa na Giza tu.
Ikabidi nijitembeze huku nje Kuna sehem flani yalikuwa yanapaki malori.
Aisee nikaenda sehem flani hivi ndo nikakuta wadada wanajiuza, nilikuwa sijawahi kuona hii kitu,ikabidi niende Kwa Mmoja hivi nikamsalimia nikumuuliza akaniambia ndio Yuko kwenye biashara.
Nikaanza kuchezea maziwa aisee alisukuma mkono akaniambia mpaka tuelewane kwanza.
Nikatoka kidog nikatokea sehem nyingine dah nilikuta Kuna gari ndogo la kifahari limepak alafu Kuna madada wawili wanakimbilia dirishani wamevaa madela aiseee, sikuamini kabisa mwili wangu ulijaa ganzi.
Baadae nikasema ngoja nitoke hapa isije nikaingia na kitu kibaya.
Ikabidi nipite kwenye uchochoro flani wa malori aaah bahati mbaya nikakutana na Teja ana kisu alafu akanipa mkwara alivoona natetemeka akaingiza mfukoni akachukua simu yangu.
Na akawa anataka na chenji nilizorudishiwa kwenye daladala duh.
***************************************
Stori yako inaumiza saana ila naomba usirudi kwenye kujiuza naamini mungu atakusimamia huyo ndugu yako atasoma na atamaliza.
Kama unaweza jaribu kuwatafuta watu ambao unaamin wanaweza kukusaidia walau kumsomesha mdog wako tu.
Huku ukiendelea kuangalia namna nyingine yakujikwamua