Ninatamani kula wakati wote na huwa napata njaa masaa machache tu baada ya kula, nina tatizo gani?

Jaribu kula chakula chako kwa kubalance ...yaani protein +wanga +fat(unsaturated fatty)...kwa luga nyepe asubuhi kula vizuri kama mfalme...Protein za kutosha na wanga kiasi na fatty ..mfano...Maharage + chapati+ parachichi au mtindi....hapo una protein + wanga +fatty...kula Mara kula kwa kubalance chakula hii itakusaidia kukaa masaa sita au nane bila kula baadala ya mawili ya sasa...
 
Kisukari!!!??? Hicho sikinawapata wazee Walevi??
Mimi sio mzee na wala sinywi pombe
Kaka hizo kisukari zipo aina mbili ... Hazina uhusiano sana na ulevi wala aging ... Sometimes ni urithi na lifestyle yako tu... Kama ni mnene kupindukia jua upo hatarini bosd kacheki faster
 
Reactions: Paa
Sina bro, labda itakua ni hali ya kawaida kwa binadamu ambaye hana matatizo katika mwili wake
Ningependa kufahamu menyu yako ikoje... Ahsubuhi unakula chakula gani... Mchana na jioni.... Nataka nikusaidie katika upangiliaji wa vyakula boss
 
Reactions: Paa
Shukrani, nitafanyia kazi nione
 
Unafanya kazi ngumu? Kama ndivyo kula tu
Sifanyi kazi ngumu. Nashinda kwenye kompyuta siku nzima...nafanya kazi za kushunghulisha ubongo sana kuliko manual works
 
Kapime KIWANGO CHA SUKARI MWILINI ASUBUHI KABLA HUJALA NA MASAA 2 BAADA YA KULA
Nilipima kabla ya kula, dokta akaniambia niko sawa, sijajaribu kupima baada ya kula
 
Kaka hizo kisukari zipo aina mbili ... Hazina uhusiano sana na ulevi wala aging ... Sometimes ni urithi na lifestyle yako tu... Kama ni mnene kupindukia jua upo hatarini bosd kacheki faster
Mimi sio mnene, naa nina simple life style...sina stress hata kijiko
 
Ningependa kufahamu menyu yako ikoje... Ahsubuhi unakula chakula gani... Mchana na jioni.... Nataka nikusaidie katika upangiliaji wa vyakula boss
Asubuhi nakulaga chai ya maziwa na vitafunio kama ndizi zilizoiva zile za kuchoma kwa mafuta, sambusa, maandazi, bagia....sometimes supu ya kuku au ngombe ....chapati ..uji wa ulezi mara chache.
Pi huwa nakula mihogo/ viazi

Mchana nakula ugali/wali + maharage na dagaa+nyama+mboga za majani matunda...nyanya chungu...bamia

Usiku nakulaga mtindi na chakula chochote ila sio ugali na juice ya matunda

Wapi niongeze au kupunguza??
 
Unakula sana vitu vya sukari hiyo insulin inakufanya hivyo acha kabisa kula wanga anza kula vitu vya mafuta utakula Mara moja kwa siku na afya yako itakuwa makini
 
Reactions: Paa
Mimi Niko tofauti na wew kidogo ! Aisee nikipiga Soda aisee naweza nikahisi Njaa Siku nzima maana ntakuwa nakula baada ya Muda kidogo Njaaa
Kapime sukari na insulin we utakuwa nazo nyingi na uache kunywa vitu vya sukari
 
Reactions: Paa
Unakula sana vitu vya sukari hiyo insulin inakufanya hivyo acha kabisa kula wanga anza kula vitu vya mafuta utakula Mara moja kwa siku na afya yako itakuwa makini
Nile vyakula gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…