Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kila siku ninapoamka nakuzitizama siasa zetu, huwa najiuliza swali moja kama kweli kama taifa bado tunahitaji kuendelea kuwa na wanasiasa wa aina hii tuliyonayo. Kiuhalisia kila kitu Tanzania kimesimama au kinasuasua lakini hakuna anayeonyesha kustuka badala yake wanasiasa wetu wametingwa na mazingaombwe yao dhidi ya watu wanaowaongoza.
Wanasiasa wetu wameweka mfumo wa kuaminiwa wao zaidi kuliko Mitizamo, Falsafa au Itikadi wanazozisimamia. Rahisi sana kumshambulia Mbowe, Kikwete, Lipumba au mwingine yeyote yule kibinafsi kuliko kushambulia vile wanavyoviamini kwa kuwa havipo!!
Wanasiasa wetu kwa vitendo vyao si waliberali, si wajamaa, wala si mabepari, bali ni vinyonga wanaobadilika kutokana na wapi walipo na wapi wanaposema au kutenda wayatendayo. Siasa zinazoendeshwa na watu wasiofahamika misimamo yao kwa dhahiri ni siasa za watapihatima na wala haziwezi kujenga nchi. Wafuasi wao ni wafuasi wa umaarufu wa mtu unaoweza kuwa umesababishwa na kitu chochote kile hata nje ya siasa, na wafuasi hao huwa hawalindi kile huyo shujaa wao anachokiamini bali wanalinda yule wanayemuani hata kama hawajui shujaa wao huyo anasimamia nini.
Huwa najiuliza kama kuna mahali hawa "Mashujaa" wameshawahi kusema ni nini wanakisimamia kwenye nyanja ya Elimu, Afya,Sera za Kimataifa, Ajira, Ardhi, Kilimo au hata biashara. Na mara zote malumbano yao hujikita kwenye matukio na wala si kwenye hoja yakinifu muktadha wa maendeleo ya nchi yetu. Nikifika hapa huwa nagundua kwamba kumbe nchi yetu inaendeshwa kwa kudra za mwenyezimungu na hali hiyo itadumu kwa miaka mingi ijayo.
Hizi ni siasa uchwara!!
Wanasiasa wetu wameweka mfumo wa kuaminiwa wao zaidi kuliko Mitizamo, Falsafa au Itikadi wanazozisimamia. Rahisi sana kumshambulia Mbowe, Kikwete, Lipumba au mwingine yeyote yule kibinafsi kuliko kushambulia vile wanavyoviamini kwa kuwa havipo!!
Wanasiasa wetu kwa vitendo vyao si waliberali, si wajamaa, wala si mabepari, bali ni vinyonga wanaobadilika kutokana na wapi walipo na wapi wanaposema au kutenda wayatendayo. Siasa zinazoendeshwa na watu wasiofahamika misimamo yao kwa dhahiri ni siasa za watapihatima na wala haziwezi kujenga nchi. Wafuasi wao ni wafuasi wa umaarufu wa mtu unaoweza kuwa umesababishwa na kitu chochote kile hata nje ya siasa, na wafuasi hao huwa hawalindi kile huyo shujaa wao anachokiamini bali wanalinda yule wanayemuani hata kama hawajui shujaa wao huyo anasimamia nini.
Huwa najiuliza kama kuna mahali hawa "Mashujaa" wameshawahi kusema ni nini wanakisimamia kwenye nyanja ya Elimu, Afya,Sera za Kimataifa, Ajira, Ardhi, Kilimo au hata biashara. Na mara zote malumbano yao hujikita kwenye matukio na wala si kwenye hoja yakinifu muktadha wa maendeleo ya nchi yetu. Nikifika hapa huwa nagundua kwamba kumbe nchi yetu inaendeshwa kwa kudra za mwenyezimungu na hali hiyo itadumu kwa miaka mingi ijayo.
Hizi ni siasa uchwara!!