Ningekuwa Dkt. Bashiru ningeamua tu kujiuzulu

Ningekuwa Dkt. Bashiru ningeamua tu kujiuzulu

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Busara na msimamo ndio jambo la msingi sana kwa mwanadamu anayejitambua, kujiamini na kujipanga kwa kesho yake.

Ajali ya kisiasa aliyoipata Dr. Bashiru ni pigo kubwa kwake na kwa watu waliokuwa wanamuamini. Bashiru ametupwa nje ya ulingo wa utawala wa siasa za CCM na sasa anakwenda kutumika kama kitambaa cha kufutia vumbi cha watawala ndani ya Bunge. Legacy yake imefutwa ndani ya muda mfupi sana.

Dr. Bashiru ni msomi mzuri na mwalimu wa chuo kikuu. Kazi ya kufundisha ndio kazi aliyoipenda na kuifurahia zaidi katika maisha yake. Huu ndio wakati wake wa kurejea Chuo kikuu kufundisha.

Akutukanae huwa hakuchagulii tusi, CCM na serikali yake hawamuhitaji tena Bashiru na huenda hawakuwahi kumhitaji kabisa (ni Magufuli yeye mwenyewe ndio alimhitaji Bashiru), walichomfanyia Bashiru kinatosha, akiendelea kuwa mbishi na mkaidi kikubwa na kibaya zaidi kitafuata.

Njia bora kwa Bashiru kwa sasa ni kuwakwepa wabaya wake na kukaa kimya. Ubunge wa kupewa haiwezi kumfanya kukaa kimya, ni ubunge wa kitumwa, atapikiwa majungu na kuzushiwa kila mbaya na wanaCCM wenzake.

Majuto ni mjukuu.
 
Ni kawaida ya kenge kutosikia maumivu hadi pale anaposikia damu zinamvuja ndiyo anajua kuwa ameumia.

Mwache aendelee na tamaa ya madaraka huku akizidi kuporomoka
 
Sasa Mimi naona Bashiru Hana tamaa ya madaraka Ila wanaompa madaraka labda ndio wanatamani awe na madaraka.
Hajawahi Kuomba kazi yoyote katika kazi alizozifanya hizi kubwa zaidi ya kuteuliwa kwamba waliomteua ndio waliona anafaa sio yeye aliona anafaa.
Sasa hapo kosa lake ni nini na hata hajawahi kugombea nafasi yoyote kabisa Kati ya hizo alizozishika.
 
Ili zahabu iwe zahabu lazima ipite kwenye moto.

For Bashiru, the future is bright.
 
Kuna external force imempiga bashiru TKO, Wastaafu wabaya sana tena nahisi kuna underway plan itamtoa Ulingoni, Huyu mtaalam arudi tu kula vumbi la Chaki, Mwisho wake kisiasa umekuwa worse sana, Shida ya watu wa ule ukanda hawapendi kuwa loyal kwa mwanamke ata awe boss wake, We unajua Mzee baba kangata shuka afu unaanza Figisu, Ofisi ya makamu wa rais ina facilities nyingi sana na ina watu kila point Pengine ni superior ofisi ikitoka ya Namba moja, Mama kanyagia apo apo tuna imani na wewe sana
 
Unamshauri ajiuzulu halafu arudi Udsm kupiga chaki! Bora afedheheke tu na huo ubunge wake wa kuteuliwa. Ila siyo kurudia hiyo kazi ngumu na isiyo na maslahi yoyote yale! ya ualimu.
 
Kuna external force imempiga bashiru TKO, Wastaafu wabaya sana tena nahisi kuna underway plan itamtoa Ulingoni, Huyu mtaalam arudi tu kula vumbi la Chaki, Mwisho wake kisiasa umekuwa worse sana, Shida ya watu wa ule ukanda hawapendi kuwa loyal kwa mwanamke ata awe boss wake, We unajua Mzee baba kangata shuka afu unaanza Figisu, Ofisi ya makamu wa rais ina facilities nyingi sana na ina watu kila point Pengine ni superior ofisi ikitoka ya Namba moja, Mama kanyagia apo apo tuna imani na wewe sana
Bashiru is underdog on Building the national.
Jizi la kura
Idiot
Negative conscience
 
Unamshauri ajiuzulu halafu arudi Udsm kupiga chaki! Bora afedheheke tu na huo ubunge wake wa kuteuliwa. Ila siyo kurudia hiyo kazi ngumu na isiyo na maslahi yoyote yale! ya ualimu.
Huyo Kakulwa kaiba sana hela
Ndo maana pale kwao Bukoba katelelo Rulongo Bukoba vijijini alikuwa anaabudiwa mwizi hafai
 
Unamshauri ajiuzulu halafu arudi Udsm kupiga chaki! Bora afedheheke tu na huo ubunge wake wa kuteuliwa. Ila siyo kurudia hiyo kazi ngumu na isiyo na maslahi yoyote yale! ya ualimu.
Huo ubunge amepewa kama mtego au kongwa la utumwa. Amekuwa demotion na kuzawadiwa ubunge wa viti maalum!
Ni vyema akarejea zake kwenye kupiga chaki zake pale UDSM, akafanya kile anachokiamini na kukipenda katika maisha yake kuliko huu utumwa wa siasa za kimalaya ndani ya CCM.
 
Sasa Mimi naona Bashiru Hana tamaa ya madaraka Ila wanaompa madaraka labda ndio wanatamani awe na madaraka.
Hajawahi Kuomba kazi yoyote katika kazi alizozifanya hizi kubwa zaidi ya kuteuliwa kwamba waliomteua ndio waliona anafaa sio yeye aliona anafaa.
Sasa hapo kosa lake ni nini na hata hajawahi kugombea nafasi yoyote kabisa Kati ya hizo alizozishika.
Utajuaje kama alifanya mafrekechee ili ateuliwe huwezi jua siri za mtu wala akiwazacho
 
Sasa Mimi naona Bashiru Hana tamaa ya madaraka Ila wanaompa madaraka labda ndio wanatamani awe na madaraka.
Hajawahi Kuomba kazi yoyote katika kazi alizozifanya hizi kubwa zaidi ya kuteuliwa kwamba waliomteua ndio waliona anafaa sio yeye aliona anafaa.
Sasa hapo kosa lake ni nini na hata hajawahi kugombea nafasi yoyote kabisa Kati ya hizo alizozishika.
Na yeye anapewa madaraka asiyoyataka na kuyapokea tu?
Sasa huu ndio wakati wake wa kuonyesha msimamo, aachane na siasa uchwara za CCM, asisubiri mpaka siku apopolewe mawe na makada wa CCM. Hawamtaki na hawampendi.
 
Back
Top Bottom