CHANZO
Busha (Hydrocele or hydrocoele) husababishwa na uwepo wa majimaji flani kwenye vifuko vya korodani. Hali hii husababishwa na minyoo aina ya filaria (wuchereria bancrofti, brugia malayi na brugia timori) ambao huziba mfumo wa lymph unaorudisha lymph kwenye mfumo wa damu hivyo kusababisha kimiminika hicho kiitwacho lymph kujikusanya kwenye vifuko hivyo, minyoo hii ya filaria huenezwa na mbu aina ya anopheles, aedes na mansonia ambao huahamisha minyoo kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mtu mzima.
TIBA:
Dawa aina ya Ivermectin au Oral diethylcarbamazine ukichanganya na antibiotics mf: doxycycline ili kuua symbiotic bacteria wanaoambatana na minyoo hiyo pia excision Surgery (upasuaji wa kuondoa busha) kwa kesi sugu.
KINGA:
Kinga ni kuzuia maambukizi kutoka kwa vectors ambao ni mbu kwa kutumia dawa za kuua wadudu na njia nyinginezo kama matumizi ya vyandarua vyenye dawa.