Nini chanzo cha nyumba nyingi zinazojengewa Tanzania kubaki mapagala yaliyogeuka magofu?

Nini chanzo cha nyumba nyingi zinazojengewa Tanzania kubaki mapagala yaliyogeuka magofu?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Katika mambo huwa yananishangaza na kunifikirisha sehemu mbalimbali za nchi hii ni uwepo wa majengo mengi ya nyumba za watu walionza kujenga kubaki bila kumaliziwa(mapagala) kwa muda mrefu sana na hatimaye kugeuka magofu.

Tatizo huwa ni nini?

Ni ujenzi wa kukurupuka?

Ujenzi bila kuwa na taarifa muhimu za kutosha? (Ile mtu anaambiwa ukipiga mahesabu sana hutajenga, we anza tu)

Kwa nini mtu anapoona amefikia mahali pumzi katika ujenzi imekata na hakuna dalili ya kuendelea muda mrefu ujao asiliuze tu jengo(pagala) lake na hiyo pesa akaitumia kujaribu kufanya mambo mengine?

Nachelea kusema sekta ya real estate Tanzania inaweza kuwa chanzo cha umasikini mkubwa kwa raia wengi wenye kipato cha kawaida waliojaribu kujiingiza katika hii sekta

Ni hasara kubwa sana kuwa na pagala lililogeuka gofu.
 
Si uokote tu
All the best
Katika mambo huwa yananishangaza na kunifikirisha sehemu mbalimbali za nchi hii ni uwepo wa majengo mengi ya nyumba za watu walionza kujenga kubaki bila kumaliziwa(mapagala) kwa muda mrefu sana na hatimaye kugeuka magofu...
Sababu kuu ni pesa kukata katikati ya ujenzi na mtu kukosa mifereji ya kumuingizia pesa ili aendelee na ujenzi wake .
 
Wenye mapagala yao wakali, hawataki yaguswe kabisa!
Mkuu tusijisahaulishe uhalisia wa Mtanzania na mishahara ya mhindi. Kupata tu kiwanja ni shughuli, kama kapambana kafika lenta ni sawa tu nyumba ikae hata miaka 7 mpaka apate ela ya bati au pension yake imalizie maana akiuza akafanya mambo mengine nje ya ujenzi uzee ukifika akastaafu asiweze kulipa tena kodi nani atampokea? Unless bei anayouzia imsaidie kupata au kujenga nyumba ingine.
 
Mkuu tusijisahaulishe uhalisia wa Mtanzania na mishahara ya mhindi. Kupata tu kiwanja ni shughuli, kama kapambana kafika lenta ni sawa tu nyumba ikae hata miaka 7 mpaka apate ela ya bati au pension yake imalizie maana akiuza akafanya mambo mengine nje ya ujenzi uzee ukifika akastaafu asiweze kulipa tena kodi nani atampokea? Unless bei anayouzia imsaidie kupata au kujenga nyumba ingine.
Uza pagala fanya biashara, fuga, lima nunua hisa za UTT Amis au weka fixed deposits n.k badala ya kusubiria uzeeni uje umalizie pagala
 
Inategemea na aina ya kisababishi cha kuwepo kwa mapagala hayo, mfano:-​
  • Wengine walikuwa wanajenga bila familia zao kujua, umauti ukamkuta na jengo likawa halina mmiliki na kutokuendelezwa.​
  • Wengine wakati wanaanza ujenzi walikuwa karibu na eneo husika, baada ya kuhama kutokana na mambo ya kikazi n.k akawa mbali na eneo husika na kushindwa kuendeleza​
  • Wengine wamefikia hatua fulani ya ujenzi, wakakutana na changamoto za ugonjwa, kazi, familia n.k na kushindwa kuendeleza.​
  • Wengine wanakuwa wamepata zuio kutoka mamlaka husika wasiendelee na ujenzi​
Kwa mazingira hayo, mapagala yatapungua kutokana na aina ya kisababishi cha kuwepo kwa mapagala hayo.​
 
Kwa mimi niliyejenga nyumba yangu ya kuishi for almost 13 years naweza kusema kikubwa kinatukwamisha wengi ni hatuna elimu juu ya ujenzi na pia hatupendi kuwatumia wataalamu wa ujenzi eg:Qs‘s,architects etc.

Kuokoteza ramani kwa sababu mjomba au rafiki aliijenga wakati mwengine kuongeza hata vitu ambavyo wao hawakuviweka husababisha ongezeko la gharama mwisho mjenzi kukata tamaa,kwa opti ya kusema mtu auze tukumbuke maskini hana cha kumiliki kinachomfaa kama nyumba hata kama haijakamilika kwake bora iwepo.
 
Kwa mimi niliyejenga nyumba yangu ya kuishi for almost 13 years naweza kusema kikubwa kinatukwamisha wengi ni hatuna elimu juu ya ujenzi na pia hatupendi kuwatumia wataalamu wa ujenzi eg:Qs‘s,architects etc.

Kuokoteza ramani kwa sababu mjomba au rafiki aliijenga wakati mwengine kuongeza hata vitu ambavyo wao hawakuviweka husababisha ongezeko la gharama mwisho mjenzi kukata tamaa,kwa opti ya kusema mtu auze tukumbuke maskini hana cha kumiliki kinachomfaa kama nyumba hata kama haijakamilika kwake bora iwepo.
Miaka 13 hiyo ni nyumba ya kawaida ya kuishi au kasri! Bila shaka itakuwa bonge la mjengo.
 
Tanzania wanatamani kujenga nyumba expensive as if ni kitu cha milele na hatimaye hujikuta wanashindwa kumalizia. Tujifunze kwa wakenya ase huwa wanajenga very simple houses
Hapana mkuu kusema tujifunze kwa Wakenya kuhusu suala la ujenzi napingana na wewe hao jamaa kuna vya kuiga kutoka kwao siyo issue ya makazi.

Muhimu Watanzania tuujue umuhimu wa kutumia wataalamu ujenzi,nimejifunza kitu ktk angle hii ukitaka ufanikiwe kwa wakati onana na hawa watu ni gharama ndiyo lakini utakapomtumia mtu huyu vipo vitu vingi atakufumbua macho kabla hujaenda kukwamia kwenye lintel,
 
Back
Top Bottom