Nini chanzo cha ongezeko la tuhuma za ndugu kurogana na kukwamishana?

Nini chanzo cha ongezeko la tuhuma za ndugu kurogana na kukwamishana?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Uchawi upo. Jambo la ajabu kwa sasa nimepata kesi zaidi ya tano ndugu kurogana.

Yaani kuna moja mama hataki kuona vijana wa kike na wa kiume wa wanatoboa.

Ndugu wanafichana mambo na kila mmoja anamuangalia mwenzake kama kihatarishi. Dada mmoja ameniambia Alfajiri anaona anakabwa na Mama yake mdogo, huku akimwambia lazima tukukwamishe tu utake usitake.

Mwingine mtu mzima hata kwenye msiba aliingia kimafia kwa hofu ndugu zake wamemuwekea mtego kwenye vyakula vya msibani wamuue. Yeye ndiye amesaomesha na kusomeshea watoto wao.

Kuna mmoja aliona kwenye ndoto ndugu anamletea zawadi ya chakula, hakumkuta akampa mwingine huyo aliyekila alikutwa amekufa kimazingara makaburini siku kadhaa. Hicho alichokiona kikatokea hivyohivyo.

Mwingine alitafuta mtoto wa ndugu yake anapofanyia kazi, akalazimisha kumpa pesa ya noti 10K, kumbe ile pesa ilikuwa imefanyiwa namna ili jamaa afukuzwe na kufirisika. Mama mwenye nyumba wa huyo jamaa usiku akaona tukio lote ndotoni. Asubuhi akaja kumuhadithia kila kitu wakati hakuwepo na hamjui huyo aliyetoa ile pesa. Akamwambia umewakosea nini ndugu zako mbona wanakutafuta sana. Jamaa akawa analia tu kwa uchungu.

Maisha ni vita vya kiroho. Muamini Mungu, usiamini ndugu, marafiki na watu wanaosema ni wa karibu kwako. Wengine wamwkusogelea ili wakujue vizuri wakikushambulia wafumue hadi mizizi.

Tumia Muda mwingi kwenye sala, kazi, na familia yako, ndugu chagua wale mnaoendana wengine wapende sio lazima wakujue sana.

Ni hayo tu

Mtumishi
Matunduizi.
 
Uongezekaji wa tuhuma za ndugu kurogana na kukwamishana ni suala tata lenye mizizi mingi na linaweza kutokea kwa sababu mbalimbali.
Mfano angalia video hii HAPA

Ni muhimu kutambua kuwa kila familia ina changamoto zake na sababu zinazoweza kusababisha migogoro kati ya ndugu ni za kipekee.

Baadhi ya sababu zinazoweza kuchangia kuongezeka kwa migogoro kati ya ndugu ni hizi HAPA

Urithi: Migogoro mingi ya kifamilia hutokea pale kunapokuwa na mizozo kuhusu urithi, hasa pale kunapokuwa na mali nyingi au kuna kutoelewana kuhusu jinsi mali hiyo inapaswa kugawanywa.

Biashara ya familia: Wakati ndugu wanashiriki biashara pamoja, kunaweza kutokea tofauti za maoni kuhusu uendeshaji wa biashara, ugawaji wa faida, na uongozi.
Ushawishi wa nje: Marafiki, majirani, au hata vyombo vya habari vinaweza kuathiri uhusiano wa kifamilia na kusababisha migogoro.
Mabadiliko ya kijamii na kiuchumi Mabadiliko ya haraka katika jamii, kama vile miji kukua na kuongezeka kwa utajiri, yanaweza kusababisha mabadiliko katika maadili na mitazamo ya watu, na hivyo kusababisha migogoro katika familia.
Ukosefu wa mawasiliano: Kutokuwa na mawasiliano ya wazi na ya mara kwa mara kati ya ndugu kunaweza kusababisha kutoelewana na kuchukiana.
Pia angalia HAPA
Masuala ya kisaikolojia: Matico ya kisaikolojia ya mtu binafsi, kama vile wivu, chuki, au uchungu, yanaweza kuathiri uhusiano na ndugu.
Kujua zaidi bonyeza HAPA

.
 
Mambo ya uchawi husikika kwa maskini walala hoi na makabwela, Hasa waafrika.

Utajiri wa kishetani husikika tu kwa waafrika pangu pakavu tia mchuzi.

Huwezi kusikia Forbes wametoa orodha ya matajiri ambao vyanzo vyao vya mapato ni uchawi au ushirikina.

Ila utasikia investments, real estates na makampuni makubwa ya kibiashara.
 
Uongezekaji wa tuhuma za ndugu kurogana na kukwamishana ni suala tata lenye mizizi mingi na linaweza kutokea kwa sababu mbalimbali.
Mfano angalia video hii HAPA

Ni muhimu kutambua kuwa kila familia ina changamoto zake na sababu zinazoweza kusababisha migogoro kati ya ndugu ni za kipekee.

Baadhi ya sababu zinazoweza kuchangia kuongezeka kwa migogoro kati ya ndugu ni hizi HAPA

Urithi: Migogoro mingi ya kifamilia hutokea pale kunapokuwa na mizozo kuhusu urithi, hasa pale kunapokuwa na mali nyingi au kuna kutoelewana kuhusu jinsi mali hiyo inapaswa kugawanywa.

Biashara ya familia: Wakati ndugu wanashiriki biashara pamoja, kunaweza kutokea tofauti za maoni kuhusu uendeshaji wa biashara, ugawaji wa faida, na uongozi.
Ushawishi wa nje: Marafiki, majirani, au hata vyombo vya habari vinaweza kuathiri uhusiano wa kifamilia na kusababisha migogoro.
Mabadiliko ya kijamii na kiuchumi Mabadiliko ya haraka katika jamii, kama vile miji kukua na kuongezeka kwa utajiri, yanaweza kusababisha mabadiliko katika maadili na mitazamo ya watu, na hivyo kusababisha migogoro katika familia.
Ukosefu wa mawasiliano: Kutokuwa na mawasiliano ya wazi na ya mara kwa mara kati ya ndugu kunaweza kusababisha kutoelewana na kuchukiana.
Pia angalia HAPA
Masuala ya kisaikolojia: Matico ya kisaikolojia ya mtu binafsi, kama vile wivu, chuki, au uchungu, yanaweza kuathiri uhusiano na ndugu.
Kujua zaidi bonyeza HAPA

.
Asqnte.
 
Mambo ya uchawi husikika kwa maskini walala hoi na makabwela, Hasa waafrika.

Utajiri wa kishetani husikika tu kwa waafrika pangu pakavu tia mchuzi.

Huwezi kusikia Forbes wametoa orodha ya matajiri ambao vyanzo vyao vya mapato ni uchawi au ushirikina.

Ila utasikia investments, real estates na makampuni makubwa ya kibiashara.
Kutoka katika level ya chini kabisa kwenda kwenye level za forbies kuna vikwazo vingi. Hatua ya kwanza kabisa ni kukwepa masikini wenzako hata kama ni wazazi wanaoamini unatakiwa kufa masikini kama wao.
Wako tayari kufanya chochote kuhakikisha hauwazidi.
Ikiwezekana hama hata mkoa.
 
Uchawi upo. Jambo la ajabu kwa sasa nimepata kesi zaidi ya tano ndugu kurogana.

Yaani kuna moja mama hataki kuona vijana wa kike na wa kiume wa wanatoboa.

Ndugu wanafichana mambo na kila mmoja anamuangalia mwenzake kama kihatarishi. Dada mmoja ameniambia Alfajiri anaona anakabwa na Mama yake mdogo, huku akimwambia lazima tukukwamishe tu utake usitake.

Mwingine mtu mzima hata kwenye msiba aliingia kimafia kwa hofu ndugu zake wamemuwekea mtego kwenye vyakula vya msibani wamuue. Yeye ndiye amesaomesha na kusomeshea watoto wao.

Kuna mmoja aliona kwenye ndoto ndugu anamletea zawadi ya chakula, hakumkuta akampa mwingine huyo aliyekila alikutwa amekufa kimazingara makaburini siku kadhaa. Hicho alichokiona kikatokea hivyohivyo.

Mwingine alitafuta mtoto wa ndugu yake anapofanyia kazi, akalazimisha kumpa pesa ya noti 10K, kumbe ile pesa ilikuwa imefanyiwa namna ili jamaa afukuzwe na kufirisika. Mama mwenye nyumba wa huyo jamaa usiku akaona tukio lote ndotoni. Asubuhi akaja kumuhadithia kila kitu wakati hakuwepo na hamjui huyo aliyetoa ile pesa. Akamwambia umewakosea nini ndugu zako mbona wanakutafuta sana. Jamaa akawa analia tu kwa uchungu.

Maisha ni vita vya kiroho. Muamini Mungu, usiamini ndugu, marafiki na watu wanaosema ni wa karibu kwako. Wengine wamwkusogelea ili wakujue vizuri wakikushambulia wafumue hadi mizizi.

Tumia Muda mwingi kwenye sala, kazi, na familia yako, ndugu chagua wale mnaoendana wengine wapende sio lazima wakujue sana.

Ni hayo tu

Mtumishi
Matunduizi.
Uchawi ni nini?

Unahakikishaje huo unaofikiri ni uchawi, ni uchawi kweli, na si kitu kingine usichokielewa tu?
 
Sababu nyingine, watu wengi kwa kujua au kutojua wamerithishwa mikoba ya wazee. Sasa wale wazee wanamaelekezo pia wanataka kurithisha mindset zao kwa vitukuu japo wamekufa. Kama wao waliona umasikini na hali nguvu ndio ufahari huyo mwenye mikoba atasimamia hilo kwa hali na mali. Atakuwa agent wa kukwamisha kila anayefurukuta ili awafurahishe wazee na mizimu.

Mnyororo wa mduara wa umasikini wa familia haukatwi kwa msumeno wa mbao. Inahitajika mikakati mikali sana.
 
Uchawi haupo wacha kupoteza muda wako...Fanya kazi...kushindwa kwako kimaisha usitafute kichaka cha uchawi kujifichia humo...tatua changamoto zako....tumia akili .

Uchawi haupo, haujawai kuwepo na hautokaa kuwepo
 
Mojawapo ya malengo ya milenia, Millennium Development Goals( MDG)

Kutokomeza umasikini uliokithiri kwa kipare to eradicate extremely poverty.

Matokeo ya MDGs yanaonyesha umasikini au poverty ni mtambuka sana kuanzia mentality, utamaduni, Mila, Imani, desturi, itikadi n.k.

Uchawi na ushirikina umetawala fikra na mawazo ya jamii masikini.
 
Uchawi upo. Jambo la ajabu kwa sasa nimepata kesi zaidi ya tano ndugu kurogana.

Yaani kuna moja mama hataki kuona vijana wa kike na wa kiume wa wanatoboa.

Ndugu wanafichana mambo na kila mmoja anamuangalia mwenzake kama kihatarishi. Dada mmoja ameniambia Alfajiri anaona anakabwa na Mama yake mdogo, huku akimwambia lazima tukukwamishe tu utake usitake.

Mwingine mtu mzima hata kwenye msiba aliingia kimafia kwa hofu ndugu zake wamemuwekea mtego kwenye vyakula vya msibani wamuue. Yeye ndiye amesaomesha na kusomeshea watoto wao.

Kuna mmoja aliona kwenye ndoto ndugu anamletea zawadi ya chakula, hakumkuta akampa mwingine huyo aliyekila alikutwa amekufa kimazingara makaburini siku kadhaa. Hicho alichokiona kikatokea hivyohivyo.

Mwingine alitafuta mtoto wa ndugu yake anapofanyia kazi, akalazimisha kumpa pesa ya noti 10K, kumbe ile pesa ilikuwa imefanyiwa namna ili jamaa afukuzwe na kufirisika. Mama mwenye nyumba wa huyo jamaa usiku akaona tukio lote ndotoni. Asubuhi akaja kumuhadithia kila kitu wakati hakuwepo na hamjui huyo aliyetoa ile pesa. Akamwambia umewakosea nini ndugu zako mbona wanakutafuta sana. Jamaa akawa analia tu kwa uchungu.

Maisha ni vita vya kiroho. Muamini Mungu, usiamini ndugu, marafiki na watu wanaosema ni wa karibu kwako. Wengine wamwkusogelea ili wakujue vizuri wakikushambulia wafumue hadi mizizi.

Tumia Muda mwingi kwenye sala, kazi, na familia yako, ndugu chagua wale mnaoendana wengine wapende sio lazima wakujue sana.

Ni hayo tu

Mtumishi
Matunduizi.
Ukiona Ukoo/Familia Ina Umasikini ndani yake, na Waliotoboa wanahesabika Tena wametoboa Kwa mbinde, na inawabidi kama Wajitenge hivi na Familia ili wa survive... MEANS KUNA UCHAWI KWENYE FAMILIA....!
 
Back
Top Bottom