habari zenu wana jukwaa, ni imani yangu kwamba mu wazima wa afya!
mwenzenu nimekumbwa na tatizo la muda mrefu sana toka mwaka 2004 nikiwa darasa la sita, nimekuwa nakosa hamu ya chakula kabisa, ama hata pale ninapokula, basi nakula kidogo saaana na endapo nikijilazimisha kula, huwa najisikia kutapika!
ndugu zangu, tatizo hili limenisumbua sana, nimezunguka baadhi ya hospitali hapa jijini na nimepewa ushauri na tiba za kitaalamu, lakini naona mambo ni yale yale tu hamna mabadiliko! yani kula kwangu imekuwa nafikia kipindi naweza kaa kuanzia asubuhi mpaka hata jioni ndio nakumbuka kula, tena napo kidogo tu!
naombeni ushauri wenu ndugu zangu na tiba mbadala ili nisije zidisha tatizo!