JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Kwa nyakati tofauti kumekuwa na Viongozi walionukuliwa wakisema "Nchi hii imechezewa sana, Nchi iligeuzwa Shamba la Bibi lakini wahusika hawatajwi. Wapo waliowahi kutoa kauli za Vitisho ikiwemo Unanijua Mimi ni Nani?" na wengine waliwahi kutuhumiwa kutumia Mamlaka yao kuvunja Sheria za nchi hadharani
Je, unadhani mambo hayo yanasababishwa na nini na kwanini hakuna Uwajibishwaji wa wazi kwa wahusika?
Jiunge nasi katika Mjadala utakaojadili Chimbuko la Matumizi Mabaya ya Madaraka, ungana nasi leo Juni 6, 2024 Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2:00 Usiku kupitia #XSpaces ya JamiiForums
Link ya Mjadala jamii.app/JFMadaraka
=======
Mjadala umeanza kwa muongoza mjadala, Ipyana Gwaselya kumkaribisha Tito Magoti baada ya kuufungua.
Tito Magoti(Mtetezi wa haki za Kibinadamu): Mada ni pana, nitaangazia kwa upande niliouchagua, matumizi mabaya ya madaraka kwa viongozi wa Umma. Kumekuwa na matumizi mabaya ya madaraka kwa muda mrefu kwasababu ya kukosekana uwajibikaji. Imeonekana na kawaida kukiuka miiko ya maadili bila kuwajibishwa na mhusika akaendelea na uongozi.
Tuna mifumo butu, bunge ni kama halipo, hatuoni chachu ya Bunge kusimamia uwajibikaji hata tukitazama ripoti za CAG.
Utamaduni huu umekuwa kama sehemu ya utamaduni wa uongozi wetu(matumizi mabaya ya madaraka).
Ipyana Gwaselya: Kuna viongozi waliwahi kutuhumiwa kwa matumizi ya madaraka nchini na Je waliwajibishwa inavyopaswa?
Eugine Kabendera: Nawapongeza Jamii kwa kuendesha mijadala hii. Nawakumbuka haraka haraka Basil Mramba na mwenzake ambao walipewa adhabu ya kufagia lakini hatujawahi kuona hukumu kama ya jana aliyefungwa miaka 7 kwa kutapeli milioni nne za Ridhwani Kikwete.
Napenda nimguse leo Paul Makonda, hali aliyokuwa nayo miaka 10 iliyopita na leo ni vitu viwili tofauti, unaweza ukajiuliza huyu mtu ana biashara gani!
Chimbuko
Namna na jinsi viongozi hawa wanavyopatikana. Binadamu tuna tamaa hatukatai lakini sheria na hukumu zake ziko vipi? Kama adhabu ni kwenda kufagia Palestina! Sheria zimekuwa bubu na butu.
Viongozi lazima wawe na shughuli za kufanya.
Ipyana Gwaselya: Sheria za Tanzania zina Nguvu ya kupambana na matumizi mabaya ya madaraka
Thomas: Mimi naweza kusema Sheria za kuwafuatilia wanaofanya Madudu zipo ili Changamoto ni pale ambapo hatua zikichukuliwa Wananchi hawapati Taarifa
Kila Mwaka tuna tukio la Ripoti za CAG na huwa anasema kwenye Ripoti iliyopita ni mambo mangapi yalishughulikiwa. Shida hatufanyi 'publication' ya hatua zilizochukuliwa
Mara nyingi hatua tunaona zinachukuliwa kwa Viongozi wa nafasi za Uteuzi kwasababu Ajira ya Mtumishi wa Umma kuna process ndefu ya kumuondoa
Ili kuweka public trust, hatua zozote zikichukuliwa visisubiri ripoti ya CAG ya mwakani.
Abdul Nondo: Matumizi mabaya ya madaraka ni kutumia cheo vibaya kuumiza watu kukidhi matakwa yake. Hautoi huduma, fedha za kutoa huduma unazitumia kwa maslahi binafsi.
Tatizo kubwa ninaloliona kama chanzo cha Matumizi mabaya ya Madaraka ni kutokuwa na Mifumo Imara ya Utaasisi kama Katiba Imara, Tamaduni Imara na Sheria imara. Viongozi wanatumia utashi wao badala ya kutumia Utaratibu
Sheria zetu zina mianya mingi zinazofanya viongozi kuongoza kwa utashi wao.
Huwezi kuzungumza matumizi mabaya bila kuongelea upatikaji wa viongozi. Kiongozi wa kumteua mtu kwasababu tu ni kada, ndugu. Hawi royal kwa wananchi bali kwa aliyemteua.
Polisi anapofanya Mauaji kwa Raia kunatakiwa kuwe na Chombo tofauti na Polisi wenyewe ambacho kitafanya Uchunguzi na kuleta Uwajibikaji kwa wahusika
Katiba Imara ndio itakayofanya Viongozi walioko Madaraka wajione kwamba wao ni Agent na kumpa Madaraka Mwananchi
Tusipotambua Power ya Mwananchi hawa Viongozi wataendelea kuwa hivi walivyo
Kamala Dickson: Kuna mambo ambayo ni Mtambuka. Mfano kwenye kipindi fulani kuanzia kwa JK Taasisi zilikuwa na Uhai na unaona hata Watu ambao imezalisha kwa ajili ya Uwajibikaji
Ukiangalia Vyombo vya Habari kipindi hicho unaona kulikuwa na Jicho la Uwajibikaji ambao ulitokana na Watendaji kuanzia Mwandishi mpaka kwa Mlaji
Tumeona Wakurugenzi fulani ambao baada ya CAG kutoa Ripoti wamehamishwa Vituo badala ya kuchukuliwa hatua. Kama Wewe umeteuliwa na unataka kumuwajibusha mwenzio ambaye naye ameteuliwa halafu kahamishwa Kituo inakuwa ngumu kumchukulia hatua.
Tito Magoti: Sheria zetu zipo lakini zinajitegemeza kwa Viongozi wa Kisiasa hasa Rais, Uwajibikaji nao umetegemea neno la Rais, akitia neno utaona Mawaziri na kila Mtu anahangaika kuonesha kwamba anafuatilia
Niambie ni Polisi gani ambaye anaweza kwenda kumkamata Mkuu wa Wilaya au Kiongozi yeyote Mwanadamizi wa Serikali?
Lakini Mimi nikiandika hapa hata Tweet nitachukuliwa kwasababu Sheria zetu zinabagua na Usawa mbele ya Sheria ulishakufa muda mrefu kwenye Nchi yetu.
Tunasikia skendo mbalimbali Mikoani kwamba huyu kaiba hiki au kafanya hivi lakini watasubiria mpaka Waziri Mkuu aende kutembelea hilo eneo
Watu wanapakatwa na kurudishwa Ofisini utadhani hawajawahi kufanya Matukio yoyote. Nani asiyejua kwamba Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliwahi kuvamia Kituo cha Habari akiwa na Silaha, pia ameshatoa kauli nyingi mbaya mbaya dhidi ya Watu lakini leo hii amerudi Ofisini
Tulihitaji uthibitisho gani kujua kwamba huyu Mtu hafai kushika Madaraka.
Niambie ni skendo gani kubwa ambayo ilishughulikiwa mpaka ikaacha historia. Mwenzangu amesema hapa Watu walifanya makosa halafu wakapewa adhabu ya kwenda kufagia Hospital ya Palestina, haya ni Maigizo
Askari walimuua Mwanafunzi wa NIT, Akwilina halafu wakaenda wakafungua kesi ila Mwendesha Mashtaka anakuja anaifuta kwamba hana nia ya kuendelea na hiyo kesi.
Kuna Polisi wana kesi kule Mtwara ila inazungushwa tu ila ifike mahali Watu tusahau. Tunaishi kama vile tupo Gheto.
Onesmo Mushi: Kuna kitu huwa tunakiangalia vibaya nacho ni tafsiri ya Madaraka, inaaminika wenye nguvu katika Nchi ndio wanaokuwa na nafasi ya kuiweka Serikali madarakani wakati kwa uhalisia ni Wananchi ndio wanaoiweka madarakani.
Kwa bahati mbaya Wananchi tumeruhusu viongozi na Taasisi zao kuchukua madaraka na maamuzi yetu, pia sisi Wananchi, tumeruhusu Serikali ituongoze kwa imani na siyo kwa kuchambua sera za kiongozi.
Eugene Kabendera: Umma wa Watanzania hauwezi kuufananisha na Umma wa Jamii nyingine kama vile ilivyo nchi kadhaa, sisi ni Watu wa kuvumilia na kumuachia Mungu, tunatakiwa kutoka huko na kuzungumza
Mfano mtu anaweza kukukanyaga kwenye Daladala na ukavumilia, unafika unapokwenda ndio unazungumza, unatakiwa kusema kuanzia mapema kuwa unaumia
Je, unadhani mambo hayo yanasababishwa na nini na kwanini hakuna Uwajibishwaji wa wazi kwa wahusika?
Jiunge nasi katika Mjadala utakaojadili Chimbuko la Matumizi Mabaya ya Madaraka, ungana nasi leo Juni 6, 2024 Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2:00 Usiku kupitia #XSpaces ya JamiiForums
Link ya Mjadala jamii.app/JFMadaraka
=======
Mjadala umeanza kwa muongoza mjadala, Ipyana Gwaselya kumkaribisha Tito Magoti baada ya kuufungua.
Tito Magoti(Mtetezi wa haki za Kibinadamu): Mada ni pana, nitaangazia kwa upande niliouchagua, matumizi mabaya ya madaraka kwa viongozi wa Umma. Kumekuwa na matumizi mabaya ya madaraka kwa muda mrefu kwasababu ya kukosekana uwajibikaji. Imeonekana na kawaida kukiuka miiko ya maadili bila kuwajibishwa na mhusika akaendelea na uongozi.
Tuna mifumo butu, bunge ni kama halipo, hatuoni chachu ya Bunge kusimamia uwajibikaji hata tukitazama ripoti za CAG.
Utamaduni huu umekuwa kama sehemu ya utamaduni wa uongozi wetu(matumizi mabaya ya madaraka).
Ipyana Gwaselya: Kuna viongozi waliwahi kutuhumiwa kwa matumizi ya madaraka nchini na Je waliwajibishwa inavyopaswa?
Eugine Kabendera: Nawapongeza Jamii kwa kuendesha mijadala hii. Nawakumbuka haraka haraka Basil Mramba na mwenzake ambao walipewa adhabu ya kufagia lakini hatujawahi kuona hukumu kama ya jana aliyefungwa miaka 7 kwa kutapeli milioni nne za Ridhwani Kikwete.
Napenda nimguse leo Paul Makonda, hali aliyokuwa nayo miaka 10 iliyopita na leo ni vitu viwili tofauti, unaweza ukajiuliza huyu mtu ana biashara gani!
Chimbuko
Namna na jinsi viongozi hawa wanavyopatikana. Binadamu tuna tamaa hatukatai lakini sheria na hukumu zake ziko vipi? Kama adhabu ni kwenda kufagia Palestina! Sheria zimekuwa bubu na butu.
Viongozi lazima wawe na shughuli za kufanya.
Ipyana Gwaselya: Sheria za Tanzania zina Nguvu ya kupambana na matumizi mabaya ya madaraka
Thomas: Mimi naweza kusema Sheria za kuwafuatilia wanaofanya Madudu zipo ili Changamoto ni pale ambapo hatua zikichukuliwa Wananchi hawapati Taarifa
Kila Mwaka tuna tukio la Ripoti za CAG na huwa anasema kwenye Ripoti iliyopita ni mambo mangapi yalishughulikiwa. Shida hatufanyi 'publication' ya hatua zilizochukuliwa
Mara nyingi hatua tunaona zinachukuliwa kwa Viongozi wa nafasi za Uteuzi kwasababu Ajira ya Mtumishi wa Umma kuna process ndefu ya kumuondoa
Ili kuweka public trust, hatua zozote zikichukuliwa visisubiri ripoti ya CAG ya mwakani.
Abdul Nondo: Matumizi mabaya ya madaraka ni kutumia cheo vibaya kuumiza watu kukidhi matakwa yake. Hautoi huduma, fedha za kutoa huduma unazitumia kwa maslahi binafsi.
Tatizo kubwa ninaloliona kama chanzo cha Matumizi mabaya ya Madaraka ni kutokuwa na Mifumo Imara ya Utaasisi kama Katiba Imara, Tamaduni Imara na Sheria imara. Viongozi wanatumia utashi wao badala ya kutumia Utaratibu
Sheria zetu zina mianya mingi zinazofanya viongozi kuongoza kwa utashi wao.
Huwezi kuzungumza matumizi mabaya bila kuongelea upatikaji wa viongozi. Kiongozi wa kumteua mtu kwasababu tu ni kada, ndugu. Hawi royal kwa wananchi bali kwa aliyemteua.
Polisi anapofanya Mauaji kwa Raia kunatakiwa kuwe na Chombo tofauti na Polisi wenyewe ambacho kitafanya Uchunguzi na kuleta Uwajibikaji kwa wahusika
Katiba Imara ndio itakayofanya Viongozi walioko Madaraka wajione kwamba wao ni Agent na kumpa Madaraka Mwananchi
Tusipotambua Power ya Mwananchi hawa Viongozi wataendelea kuwa hivi walivyo
Kamala Dickson: Kuna mambo ambayo ni Mtambuka. Mfano kwenye kipindi fulani kuanzia kwa JK Taasisi zilikuwa na Uhai na unaona hata Watu ambao imezalisha kwa ajili ya Uwajibikaji
Ukiangalia Vyombo vya Habari kipindi hicho unaona kulikuwa na Jicho la Uwajibikaji ambao ulitokana na Watendaji kuanzia Mwandishi mpaka kwa Mlaji
Tumeona Wakurugenzi fulani ambao baada ya CAG kutoa Ripoti wamehamishwa Vituo badala ya kuchukuliwa hatua. Kama Wewe umeteuliwa na unataka kumuwajibusha mwenzio ambaye naye ameteuliwa halafu kahamishwa Kituo inakuwa ngumu kumchukulia hatua.
Tito Magoti: Sheria zetu zipo lakini zinajitegemeza kwa Viongozi wa Kisiasa hasa Rais, Uwajibikaji nao umetegemea neno la Rais, akitia neno utaona Mawaziri na kila Mtu anahangaika kuonesha kwamba anafuatilia
Niambie ni Polisi gani ambaye anaweza kwenda kumkamata Mkuu wa Wilaya au Kiongozi yeyote Mwanadamizi wa Serikali?
Lakini Mimi nikiandika hapa hata Tweet nitachukuliwa kwasababu Sheria zetu zinabagua na Usawa mbele ya Sheria ulishakufa muda mrefu kwenye Nchi yetu.
Tunasikia skendo mbalimbali Mikoani kwamba huyu kaiba hiki au kafanya hivi lakini watasubiria mpaka Waziri Mkuu aende kutembelea hilo eneo
Watu wanapakatwa na kurudishwa Ofisini utadhani hawajawahi kufanya Matukio yoyote. Nani asiyejua kwamba Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliwahi kuvamia Kituo cha Habari akiwa na Silaha, pia ameshatoa kauli nyingi mbaya mbaya dhidi ya Watu lakini leo hii amerudi Ofisini
Tulihitaji uthibitisho gani kujua kwamba huyu Mtu hafai kushika Madaraka.
Niambie ni skendo gani kubwa ambayo ilishughulikiwa mpaka ikaacha historia. Mwenzangu amesema hapa Watu walifanya makosa halafu wakapewa adhabu ya kwenda kufagia Hospital ya Palestina, haya ni Maigizo
Askari walimuua Mwanafunzi wa NIT, Akwilina halafu wakaenda wakafungua kesi ila Mwendesha Mashtaka anakuja anaifuta kwamba hana nia ya kuendelea na hiyo kesi.
Kuna Polisi wana kesi kule Mtwara ila inazungushwa tu ila ifike mahali Watu tusahau. Tunaishi kama vile tupo Gheto.
Onesmo Mushi: Kuna kitu huwa tunakiangalia vibaya nacho ni tafsiri ya Madaraka, inaaminika wenye nguvu katika Nchi ndio wanaokuwa na nafasi ya kuiweka Serikali madarakani wakati kwa uhalisia ni Wananchi ndio wanaoiweka madarakani.
Kwa bahati mbaya Wananchi tumeruhusu viongozi na Taasisi zao kuchukua madaraka na maamuzi yetu, pia sisi Wananchi, tumeruhusu Serikali ituongoze kwa imani na siyo kwa kuchambua sera za kiongozi.
Eugene Kabendera: Umma wa Watanzania hauwezi kuufananisha na Umma wa Jamii nyingine kama vile ilivyo nchi kadhaa, sisi ni Watu wa kuvumilia na kumuachia Mungu, tunatakiwa kutoka huko na kuzungumza
Mfano mtu anaweza kukukanyaga kwenye Daladala na ukavumilia, unafika unapokwenda ndio unazungumza, unatakiwa kusema kuanzia mapema kuwa unaumia