Nini faida ya nguo hizi zinazovaliwa na madiwani wetu

nasrimgambo

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2017
Posts
1,902
Reaction score
2,488
Habari,

kuna hii destruri ya madiwani kuvaa nguo aina ya majoho wawapo kwenye vikao vya halmashauri.

Binafsi sioni faida yao kuvaa hivyo kwasababu halmashauri zenyewe changamoto zipo vilevile miaka nenda rudi.

hoja yangu ni kuwa hayo manguo hayana faida kuvaliwa, na laiti yangekuwa na faida, basi tungeona lami hadi vichochoroni, maana yana faida,

ila hayana faida, ndio maana hatuoni lami hadi vichochoroni

kwanini wasivae tu nguo za kawaida kama wezao wa bungeni

nguo zenyewe ni kama hizi.

 
kwangu bora uniform/majoho ya madiwani kuliko wale wagonga mabench kutoka nyumba ya kutunga sheria.
 
Kufuata mkumbo na zaidi sana ni maigizo ya usomi na mfano wa PHD za heshima.
 
Chemsha juice ya Tangawizi kali, kamulia limau kwa mbaali mkuu..
 
Labda wanataka wakijamba harufu ziwe zinaishia kwenye hayo magauni, maana hamna la maana wanalofanya huko halmashauri, ufisadi, usimamizi mbovu wa miradi ndio majukumu ya madiwani wa Tanzania na majungu labda
 
Wahitimu wa fedha na rasilimali watu
 
Ipo siku utakuja kulalamika kua kwanini Polisi wanavaa uniform no kofia wakati vibaka na wezi bado wapo mitaani?

Hakuna nchi iliyomaliza matatizo yake yote.
 
Embu tushoneni la kutembelea tu mtaani na jioni ukiwa zako unapata kinywaji tuone kama itapigwa marufuku. Kofia isisahaulike.
 

Mkuu si hao tu. Kuna wale wa mahakamani, mawakili, wa kwenye mahafali, kwaya nk.
 
Kwani ukitazama akili za madiwani huwa unaona ziko sawa?
Tuanzie hapo
 
Kufuata mkumbo na zaidi sana ni maigizo ya usomi na mfano wa PHD za heshima.
Wakati wengi wao walitoroka masomo primary
Wana mind set ya ajabu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…