Nini hasa kilitokea mpaka UDE UDE na rafiki yake wakauawa na polisi TANGA?

Bigbootylover

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
2,847
Reaction score
1,828
Habari zenyu wakuu, juzi juzi hapa zilisambaa habari kuhusu huyu jamaa wakuitwa UDEUDE, msanii na mtunzi wa nyimbo kadhaa za mastaa hapa bongo kwamba alipigwa risasi, akiwa na msanii mwenzake na wote wakapoteza maisha kwa tuhuma za ujambazi huko TANGA, kwanza naomba kujuzwa kama ni kweli na pia nijue hasa nini kilitokea! Yaani inamaana mastaa wetu wanaishi maisha mazuri huku wakifanya mambo mabaya nyuma ya pazia? Tafadhali naomba kujuzwa
 
sio majambazi kwa tafsiri iliyozoeleka, walikuwa wakifungua spare za ndinga flani ndipo watu wakawashtukia wakawaunganishia, sasa si unajua mkulu alishatoa agizo majambazi wauliwe nao wakauliwa kwa staili hiyo
Hebu wairasmishe sanaa aisee, inafikiaje mwandishi wa heat songs anakuwa mwizi wa spares
 
inamaana sharobaro record ni jambazi duuh!
 
Masharo wengi dar ni wezi wa vifaa vya magari kuna cku nimewakosa pale baraka plaza mikocheni......narudi kwenye gari nae ndio anamaliza kufungua mlango wa gari yangu kuna mwenzake akamstua wakakimbialia kwenye gari yao n kuondoka fasta....mana wangefanikiwa kuiba ingekua kilio kwangu
 
hasa masharo wa kino na migo hawana kazi maalumu, kama sio mapunda wezi wa vifaa
 
Wee unataka tujadili majambazi ndiyo maana Dr Magufuli haaliki ikulu
 
Tunasikia stori za upende mmoja tu kwa vile Marehemu hawezi kuongea. Ukweli wanaujua Polisi. Lakini cha kunishangaza inakuwaje kibaka wa tairi la gari hana zana yoyote apigwe risasi? Kuna watu inabidi wawajibike hapa!
 
Tunasikia stori za upende mmoja tu kwa vile Marehemu hawezi kuongea. Ukweli wanaujua Polisi. Lakini cha kunishangaza inakuwaje kibaka wa tairi la gari hana zana yoyote apigwe risasi? Kuna watu inabidi wawajibike hapa!
Mkuu wanasema waliwakimbiza mpk ilipofika sehemu ambapo ikishindikana wao kukimbia, walipoona hivyo wakachomoa bunduki wakaanza kujibizana na askari ndo ikatokea 2 men down
 
Kwa kweli risasi zinaua iwe kihalali au kiharamu. Na maagizo yanapotolewa na wakubwa ni lazima sote tuyaelewe na kuyazingatia!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…