Nini hasa maana ya utu?

Nini hasa maana ya utu?

Niuzungumzie “utu” kama ambavyo wenzetu wanauita “dignity”

Mkuu nimeipenda post yako yote but I am interested hapo ulipo-translate utu kama "dignity". Hapo nyumba Mkuu Paulss ali-translate utu kama "humanity" Sasa ili ku-clear any doubt, which is which? Au "dignity" na "humanity" is the same thing?
 
Mkuu nimeipenda post yako yote but I am interested hapo ulipo-translate utu kama "dignity". Hapo nyumba Mkuu Paulss ali-translate utu kama "humanity" Sasa ili ku-clear any doubt, which is which? Au "dignity" na "humanity" is the same thing?
Teh teh teeeh
Yaani wewe umekaapembeni unatupambanisha tu mkuu,
Lakini natumai umepata mwanga utu ni nini
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu Gaijin, naomba nisikujibu moja kwa moja ila niulize swali ili litujengee uelewa mpana zaidi

Kwa nini sheria zipo? Je si ili kulinda "utu" wa wananchi/wanajamii wa nchi/jamii husika?


hebu tusaidiane mtazamo hapo kwanza ndiyo tuone tunachukua njia gani katika kuamini hili

At the same time, kuna watu kama Kant on "Morality and Dignity" ana-define kazi kubwa ya morality kama ku-foster dignity. Kama "dignity" ni utu kama ulivyo-translate, does it also mean that morality inasaidia kulinda utu? Najua Gaijin ataniuliza na morality ni nini? lol.
 
At the same time, kuna watu kama Kant on "Morality and Dignity" ana-define kazi kubwa ya morality kama ku-foster dignity. Kama "dignity" ni utu kama ulivyo-translate, does it also mean that morality inasaidia kulinda utu? Najua Gaijin ataniuliza na morality ni nini? lol.

You got that one right......who defines morals? lolz

What is your thoughts on "Might makes right"?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Ibara ya 9 ya Katiba juu ya kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea inasema kuwa "....Mamlaka ya Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha- (a) kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu zinaheshimiwa na kuthaminiwa;.." Kwa hiyo utu unaweza ukawa ni haki?

Pia ibara ya 12 (2) inachohusu usawa wa binadamu inasema "Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake." Hakuna definition ya utu kwenye hicho kkifungu na katiba nzima

Lakini Ibara ya 25(1) iinaelezea wajibu wa kushiriki kazini kwa kusema "Kazi pekee ndiyo huzaa utajiri wa mali katika jamii, ndilo chimbuko la ustawi wa wananchi na kipimo cha utu." Kwa hiyo wajibu wa kushiriki kazini ni kipimo cha utu? Kwa maana wale ambao hawatimizi huo wajibu hawana utu au kama hushirikishwi kazi then utakuwa unanyimwa wajibu wako?
 
Mkuu nimeipenda post yako yote but I am interested hapo ulipo-translate utu kama "dignity". Hapo nyumba Mkuu Paulss ali-translate utu kama "humanity" Sasa ili ku-clear any doubt, which is which? Au "dignity" na "humanity" is the same thing?

Mkuu naamini na Paulss hatujatofautiana ila ku-supplement kujazia vema....sijui ni mapungufu ya maneno kwa lugha yangu au la ndiyo maana nilipenda kuleta upande wa pili wa neno la kingereza linalotumika kama "utu" hapa kwetu

Ila ukisoma definition niliyotumia ya Mette Lebech inatumia maneno yote mawili, naomba niirudie hapa


Mette Lebech anaesema Dignity is the quality of worth (status/values) and honour (respect) intrinsic to every person which establishes the basic boundaries of humanity

Kwa hiyo ili kwenda kwa undani naomba nikupe tafsiri mbili mbili kutoka kwa watu wengine wanavyotafsiri haya maneno mawili then utapata mwanga wa kuelewa kwa undani

Humanity
NIkimsoma Simon Rees kwa undani ananiambia kuwa humanity ina-describe abilities and characteristics of human beings in whole which defines our civil rights and social causes - yaani akiwa na maana ya how one is to be treated by or to treat others


Kwa tafsiri hii naweza kusema kuwa humanity, in its totallity, are those chemistry which makes us "humans"

Kwa upande wa Dignity

Dignity:
Social Care Institute for Excellence wanasema Dignity is a state, quality or manner worthy of esteem or respect; and (by extension) self respect……….. it is a kind of system or setting which supports and promotes, and does not undermine a person's self respect regardless of any difference.

Royal College of Nursing wanasema Dignity is concerned with how people feel, think and behave/act in relation to the worth or value of themselves and others. To treat someone with dignity is to treat them as being of worth, in a way that is respectful of them as individuals


Labda itasaidia kutupa mwongozo wa kuchanganua haya maneno mawili


But in my personal opinion naweza kusema kuwa Humanity has to do with "our whole being" and Dignity has to do with "how that whole being is treated by your own self or others"........ i stand to be corrected
 
  • Thanks
Reactions: EMT
EMT, post

Kwa mujibu wa katiba, haki na utu kwa pamoja zinahitaji kulindwa na dola na sio utu pekee


EMT,

Kwa hiyo ukitaka kumtizama mtu ana utu kiasi gani utizame anafanya kazi kiasi gani? lol
 
Sheria inayozuwia ndoa za watu wa jinsia moja inalinda utu wa nani? ....

Wewe. Usitake hii thread ifungwe kwa mara ya pili. lolz

"Naye Katibu wa Baraza la Maaskofu nchini (TEC), Padri Antony Makunde, alisema "....Uingereza wasitumie umaskini wa Waafrika kulazimisha suala hilo. Wakitaka kutupa msaada watupe, lakini si kwa masharti hayo ya kuunyanyasa utu wetu wa Afrika ili tukubaliane na utamaduni wao." Alisema ni heri Waafrika wakaendelea kuwa maskini na kulinda utu na heshima waliyonayo lakini si kutaka kudhalilishwa kwa ajili ya misaada iliyojaa laana ya ushoga na usagaji.

Source: Viongozi wa dini waionya serikali na ushoga

Mwingine anasema: "Inaonekana kama vile Uingereza na nchi nyingine tajiri bado zinaamini kwamba nchi za Kiafrika ni nchi zinazoongozwa na watu ambao uroho na tamaa yao ya misaada vinaweza kuwafanya wakubali lolote lile hata likiwa baya kwa mila, desturi, imani, utamaduni na utu wa watu wao……Umaskini hauimanishi maskini kukubali kuuza roho, utu na imani yake kwa ajili ya kupewa misaada."

Source: Tukubali ushoga au tuachane na misaada

Kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa Chuo cha Mtakatifu Augustino (SAUT), Dk. Kitima, "..ushoga ni vitendo vya uovu na ukinuiwa na Serikali ni kuwaudhi wananchi wake, na kwamba kauli ya Waziri Cameron wa Uingereza ni sawa na kauli ya kutaka kuua utu wa watu…. Ushoga unaharibu utu wa mtu. Kukubali ushoga ni sawa na kuua vizazi vijavyo…"

Source: Chuo Kikuu cha SAUT chamuasa Kikwete kuhusu "Misaada na ushoga" | Fikra Pevu | Kisima cha busara!

Pia Bakwata imeahidi kuendelea kuunga mkono Serikali kwa misimamo yake ya kukataa kusaidiwa kwa masharti yasiyojali wala kuheshimu utu na thamani ya Mtanzania, kwa sababu ina lengo zuri la kuutetea utaifa.

Akizungumza katika Baraza la Idd el Hajj katika Msikiti wa Masjid Al Farouq, Kinondoni, Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema, heri kuwa tayari kufa kwa njaa kutokana na umasikini, kuliko kupewa misaada ya maendeleo kwa masharti ya kudhalilishwa utu.

Source: HabariLeo | Bakwata- Bora kufa njaa kuliko kukubali ushoga


Ukisoma huko kwenye red inalinda kutonyanyasika kwa "utu wetu wa Afrika", kutokuuliwa au kutoharibiwa kwa utu wa watu, kuheshimu utu, kutokudhalilishwa, nk. Do the above shed some lights? lol. kazi ipo.
 
EMT Pal thank you for this Insightful and USEFUL thread na kunishtua pia… It has Great Discussions in it.

Nimesoma Commets za humu ndani of which most are really really IMPRESSIVE!! Nimependa the fact kuwa as much as woote mmeongelea the same thing "Utu" imefanya kila mmoja aelezee toka angle yake… which kind of makes it really really interesting and Entertaining to an interested Mind. And prove as a fact kua "Utu" is a broad term, which must be understood from the context of what one is defining and from which community/society drawn.

The definition of "Utu" I would say differs from Society to Society… Sometimes it would even from members of the same society for it is such a conceptual term. Mara nyingi Utu unazungumziwa in the same lines as "Ubinadamu" na ubinadam consist of the facts and acts considered as humane in ones eye or society Or oneself…..

Kwa kutolea Mfano ambao upo so Valid na una many Schools of thoughts and various debates…. Ni hili suala zima la Ushoga. Hawa Westerners miaka sio Mingi saana hapo nyuma a gay person was considered as kutokua na "Utu" dhidi yake mwenyewe na jamii kwa kuenda kinyume cha Maumbile wakati wa faragha (kuenda nyuma ya maumbile is another discussion/debate pia as in what determines kua ni nyuma ya Maumbile) BUT tunaona with time the situation has evolved sasa hivi mpaka wanatetewa by all means kua they have the right to be gay na ni kwamba it is acceptable and has to be acceptable!

Where as tunaona jamii yetu ya hapa Tanzania ilivomaka kuhusiana na suala zima la Ushoga… Alternatively known as u-Cameroon sasa. Inaonekana kabisa hicho kitendo sio "utu" na hao watu kama wamelaniwa vile.

Hivo basi I would say "Utu" lies in the lines of defining what is right and what is wrong in close relation with what is considered as one's right in a certain or particular context as subjected with one(s) around...
 
You got that one right......who defines morals? lolz

What is your thoughts on "Might makes right"?

Nafikiri tuna-define morality kulingana na experiences and beliefs zetu. Hizo experiences na beliefs zinakuwa shaped au influenced na jamii tunayoishi, our religious and/or spiritual path, nk. Lakini at the end of the day, we all define our own morals. Of course, wapo watakaosema kuwa Mungu/Allah ndiye anaye-define morality, lakini this may ignore the fact that those who argue such have chosen their own faith and therefore have chosen to accept God's definition of what is moral.

But kama kuna mgongano kati ya morals za watu wawili, who gets to decide who "wins"? If, by adhering to your moral code, you violate someone else's right to live their life as they see fit, have you overstepped your bounds?
 
Gaijin
Utu wa binadamu, kuwa its against the nature
Kumbuka si kila sheria inalinda utu na si kila utu unatamkwa na sheria

Well said mkuu....tumeshakuwa hadi na sheria za kunyonga (which i declare it is against humanity) mpaka ilipofika mahali kelele za watu kupigania "utu"/"ubindamu na haki ya binadamu kuishi, ndipo inafahamika kuwa ni kosa na sheria hizo sasa zinafutwa

Nimependa pale uliposema utu hauna reference/source na ndiyo maana nikasema Utu "is human emblem", that totality of who we are na haya mengine kama sheria ni kupigania kuhakikisha hakuna mtu mwingine anaathiri utu wa mtu mwingine na pia mtu haathiri utu wake na ndiyo maana ukitaka kujinyonga leo utashtakiwa na Jamhuri (hahaaaa, hapa itakuwa ngumu "kumesa")
 
Nafikiri tuna-define morality kulingana na experiences and beliefs zetu. Hizo experiences na beliefs zinakuwa shaped au influenced na jamii tunayoishi, our religious and/or spiritual path, nk. Lakini at the end of the day, we all define our own morals. Of course, wapo watakaosema kuwa Mungu/Allah ndiye anaye-define morality, lakini this may ignore the fact that those who argue such have chosen their own faith and therefore have chosen to accept God's definition of what is moral.

But kama kuna mgongano kati ya morals za watu wawili, who gets to decide who "wins"? If, by adhering to your moral code, you violate someone else's right to live their life as they see fit, have you overstepped your bounds?

Kimsingi wenye nguvu ndio wanao define morals za jamii husika

Tukiangalia kwenye suala hilo la ushoga kwa mfano au suala la malezi ya watoto. Waafrika tunajinsi yetu ya kulea watoto, lakini Westerners kwa vile wana nguvu wanakuwa na haki ya kutufasiria morals za malez ni zipi na ndipo tunapoanza kubadili namna ya ulezi wetu.

Inaonekana kuwa ni hivyo hivyo kwenye utu.
 
Well said mkuu....tumeshakuwa hadi na sheria za kunyonga (which i declare it is against humanity) mpaka ilipofika mahali kelele za watu kupigania "utu"/"ubindamu na haki ya binadamu kuishi, ndipo inafahamika kuwa ni kosa na sheria hizo sasa zinafutwa


Kwa hiyo hapa mkuu unataka kusema zamani tulipotnga hizo sheria utu wetu ulikuwa chini, na sasa tumenyanyua viwango vya utu wetu na tumeamua kujirekebisha?

Before long tutasema tulipozuwia ndoa za jinsia moja ilikuwa ni kinyume na humanity kwa sabau wale pia wana haki ya kutambulika kisheria kama binaadamu wengine wanavyotambulika.
 
utu ni jambo liko binded na vitu mbali mbali katika jamii
  • jamii zina tamaduni zake na zinaweza kutofautiana . wagogo wana tofauti na wahehe
  • jamiii zina dini a nyingine hazina
  • Jamii zina miiko na madili
Hayo na mengine mengine ndio yana shape utu wa mtu kuwa defined na yanatofautiana
  • Mtikilia aliwahi kunukuliwa kuwa mzoga wa mwalimu nyerere uligharimu taifa pesa nyingi. Ni kweli kitu kilichokufa kintwa mzoga lakini hapo inawezekana alikosa utu kwakuchagua hilo neno sio tu kwa nyerere bali binadamu yeyote.
  • Waafrika sehemu mbali mbali walikuwa na tamaduni kuwakeketa wanawake lakini waafrika hao hao tamaduni nyingi hazitambui ushoga na ndoa za jinsia moja. Lakini ukenda sweeden na ulaya bado ni utu kwa mwanaume kuwa shoga na si utu wa mwanamke kukeketwa.
  • Kuna dini zina miiko aina ya chakula. kwa hiyo kipimo cha utu kwa kigezo cha dini au imani inaweza kuonekana kwa mtu fulani hana utu n wingine akajiona haimundolei utu kwa kula mjusi, chura etc.
Kazi ipo kwenye kutafuta universal definition ya utu.
 
Kwa hiyo hapa mkuu unataka kusema zamani tulipotnga hizo sheria utu wetu ulikuwa chini, na sasa tumenyanyua viwango vya utu wetu na tumeamua kujirekebisha?

Before long tutasema tulipozuwia ndoa za jinsia moja ilikuwa ni kinyume na humanity kwa sabau wale pia wana haki ya kutambulika kisheria kama binaadamu wengine wanavyotambulika.

Absolutely....ukimsoma mkuu EMT hapo juu anazungumzia kuwa kukua kwa "Utu"

Ukiniuliza mimi nitasema sio "kukua kwa Utu" ila "Kukua kwa Ufahamu wetu juu ya Utu wetu"....

Kwa nini nasema hivi? Hapa nitarudi kwa Mkuu Paulss anaposema "utu" wetu ni natural thing....Ulikuwepo na upo na utazidi kuwepo maadam mwanadamu anaendelea ku-exist, sema tu tatizo ni kuwa kuna mahali "TUNAPIGA UTASHI WETU KUFULI" na kuutupa utu wetu "hata mavumbini"
 
Absolutely....ukimsoma mkuu EMT hapo juu anazungumzia kuwa kukua kwa "Utu"

Ukiniuliza mimi nitasema sio "kukua kwa Utu" ila "Kukua kwa Ufahamu wetu juu ya Utu wetu"....

Kwa nini nasema hivi? Hapa nitarudi kwa Mkuu Paulss anaposema "utu" wetu ni natural thing....Ulikuwepo na upo na utazidi kuwepo maadam mwanadamu anaendelea ku-exist, sema tu tatizo ni kuwa kuna mahali "TUNAPIGA UTASHI WETU KUFULI" na kuutupa utu wetu "hata mavumbini"

Kwa maana hiyo hakuna "utu wa Kiafrika" wala "utu wa Kimagharibi".

Na jee ikiwa jambo moja litakubalika kuwa ni la ki-utu sehemu moja basi likubalike sehemu nyengine kuwa ni utu pia?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Kimsingi wenye nguvu ndio wanao define morals za jamii husika .

Mkuu umewahi kusikia ule msemo "They play in Europe, we dance in Africa" au "The one who pays the piper is the one who choose the song"?

Hapa pia ndipo inapokuja ile dhana ya "Kazi na Utu" nikiwa na maanisha "Utu na uwezo wa kujitegemea"..... Kama huna uwezo na maamuzi ya kujitegemea na ukategemea kwa mwingine kwa vyovyote yeye atakulipa na utapiga anachotaka hata kama hutaki.............Hhahaaaa, halafu kwa jeuri utawasikia wanasema "UPENDE, USIPENDE" na ukibwabwaja wanakuangalia tu halafu wanakugeuzia mgongo wanajidai wameondoka na kukuacha huku wakijisemea "Ahhaaaaa, Umekataa leo na nguo zako, utakubali kesho ukiwa uchi"
 
Mtazamaji,


Msimamo wangu mkuu uko karibu sana na huu wa kwako.

Kwa vile katiba yetu haisemi utu ni upi, inanipa mimi nafasi ya kufasiri utu nitakavyo mie (according to the things which have influenced me) na kukupa wewe nafasi ya kufasiri utakavyo wewe pia.

Chukulia suala la kuoa wake wengi. Baadhi ndani ya Tanzania wanaweza kuchukulia kuwa kuoa wake wengi ni ukosefu wa utu kwa wanawake wanaowekwa uke wenza wakati wengine wanaona ni haki yao ya msingi.

Cathode Ray amezungumzia hukumu za vifo kuwa tunaanza kuzifuta kwa sababu tumeona zinakiuka utu, lakini kuna dini zinazolazimisha hukumu ya kifo kwa baadhi ya makosa kwa hiyo kwao wao wanadhani kufuta hukumu ya kifo ni kumkosea utu aliyetendewa kosa na mhalifu.
 
Utu wa shoga jee haupaswi kuheshimiwa? lolz

Mkuu kazi ndiyo heshima, ndiyo thamani ya utu wako japo katika definition ya utu tunasema mtu habaguliwi kwa msingi wowote (hata kama hana kazi) but if we are back in relality, (KA MFANO RAHISI TU) HUNA KAZI, HUNA KIPATO THEN HUNA FEDHA YA KUNUNUA NGUO NA UTATEMBEA HUKO BARABARANI KALIO WAZI....Umedhalilisha ule utu wako

Mkuu Cathode Rays huko ambako sija-quote haina maana kuwa nime-ignore but I concur with you. Sasa huyu Gaijin kaleta swali la kizushi. lol. Kama umeona hizo links nilizoweka hapo juu, Watanzania wanapinga ushoga in the strongest terms kuwa ni kinyume na utu wetu. Pia tumeghusia suala la kazi kama kipimo cha utu. Nakubaliana na wewe kuwa kama huna kipato means huna fedha za nguo means utatembea barabarani uchi means utadhalilisha utu wako.

Sasa kuna sehemu nimem-quote Jenerali Ulimwengu huko nyuma ambapo anasema kwamba "No self-respecting African man would let another man pay for his and his wife's and his children's upkeep. Indeed, a man who allows that to happen would be considered as having been married by the provider man, call them economic homos." Ina maana hapa mwanaume atakuwa amepoteza utu wake kwa mwanaume mwingine kuwa provider wa familia yake?

If so, kwa vile, tunasema kuruhusu ushoga ni kudhalilisha utu wetu, kwa sisi Watanzania kuendelea kutembeza bakuli huko nje kuomba misaada si sawa na kukosa kipato which means hatuna fedha za kujinunulia nguo, which means tuko barabarani kalio wazi which means tunalalidhisha huo huo utu wetu tunaoutetea dhidi ya ushoga? Kama alivyosema Ulimwengu, "Rejecting the one, reject the other too"? Kama hatutakataa vyote ni utu gani tunautetea dhidi ya ushoga?
 
Back
Top Bottom