Nini husababisha wivu katika Mapenzi


Asante sana mkuu
Na ule wivu uliozudi je una madhara gani?? Make kuna watu wivu ni too much
 
Hahahaahhahahaahahahahaha lol kumbe
Ndio mkuu. Ila mimi nna wivu pia kwa manzi angu ila sio kwamba nadhani anachepuka no, yani sometimes nikiwa nae alafu akawa anaongea na mtu hata ndugu yake au maza ake nakuwa na kawivu fulani yani nataka attention yake yote iwe kwangu yani akiwa na mimi dunia yake isimame na mimi nisimamishe yangu iwe ni mimi na yeye tu
 
Asilimia 90 ya wanawake wa sasa hawapendi wanaume wenye wivu hii inatokana na ukweli kwamba wanajijua tabia zao......Duniani hakuna mwanaume asiye na wivu Mtaishia kwenye majaba watu washachoka!
 
Asante sana mkuu
Na ule wivu uliozudi je una madhara gani?? Make kuna watu wivu ni too much
Chukua mfano unammulika mwenzio machoni na touch maumivu atakavyo sikia ni kutokana na mwanga ulivyo mkali na mwanga mkali unasababiswa na betri zilivyo na nguvu

Sasa hapa nakuchambulia

MWANGA ni kile kinachokuja moyoni baada ya kuona kile unachokipenda au unaempenda kina dalili ya kuchukuliwa

MACHO ni moyo ambao unaumia unapomulikwa na mwanga na maumivu ya macho yanatokana na ukali wa wanga

BETRI ni uzuri wa kile unachokiona mbele yako kulinganisha na wewe ambacho kinatishia kuchukua kile ukipendacho

Sasa combination ya MWANGA, MACHO na BETRI ndio muundo sahihi wa wivu hakuna binadamu ambaye hana wivu ila tunatofautiana ukubwa wa wivu tu
Siku zote tatizo la wivu kupitiliza ni kupelekea magongwa ya moyo hasa BP so Mwanga ukiwa mkali ndivyo macho yanazidi kuumia
 
Huo sasa ndio ubinafsi anaousema mshana
 
Huo sasa ndio ubinafsi anaousema mshana
Sijui kama ndio wenyewe ila nimesema sometimes sio muda wote.. Sijui hiyo variation in degree ya hiyo kitu inasababishwa na nini!

Ila wivu upo tu asee. Na sio kweli kwamba mwizi akihisi anaibiwa ndio anakuwa na wivi. Hata kama hauibi unapenda kweli wivu lazima uhusike. Kataa kubali ila ndio ivo
 
me huwa nawashangaa sana wanaume wenzangu wanaokua na wivu kwa wapenzi wao...unakuta lingine kubwa zima na ndevu zake linajiliza eti kisa galfriend kalikimbia...ni utaahira.
 
Wivu upo sawa lkn wako umezidi mpka kwa ndugu zake!!!!
 
Upendo ni lazima uambatane na wivu... Ata Mungu wetu ana wivu kwetu kwa sababu anatupenda...! (Kutoka 20:5, 34:14)

Wivu utakaopitiliza ndo unakua matatizo... Either huyo mtu hajiamini au ana matatizo ya akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…