Nini inaweza kuwa shida kwenye hii engine naona inavuja oil

Nini inaweza kuwa shida kwenye hii engine naona inavuja oil

Leo mchana nimefungua bonet nikakuta kama oil ina leak kwenye gari(vvti-cc 2360)2AZ engine sijui nn shida hapo hadi nadata gari ina miaka 2 toka itoke jep ikiwa na 96,000 milage ushauri tafadhali
Kuvuja oil kwenye engine Mara nyingi ni Matatizo ya seal,
Kwa hiyo position ya picha nila Shaka Ni top cover seal
Nunua original funga imeisha.
 
Gari imechakaa kabisa halafu unaambiwa kuwa ni 96,000km!Beforward ni wezi.
 
Mkuu mbona unakuza tatizo?

Hiyo ni seal ya top cover na inaonekana hapo clearly kabisa.

Cylinder head inapokatikia asingeweza kupiga picha.

Mkuu JituMirabaMinne ,

Namimi yaweza kuwa ni the same issue, top cover seal? Nilifanya oil service. Nimetembea almost 3,000 Km, na sasa dipstick inasoma oil imo nusu! Oil imevujia sana all over the cover.

IMG_20241130_180228.jpg

IMG_20241130_180142.jpg

IMG_20241130_180910.jpg



Pia, pale zinapoingia AC pipes panaonekana kuvuja hivi (not oil). 👇🏾👇🏾
IMG_20241130_180340.jpg
 
Mkuu JituMirabaMinne ,

Namimi yaweza kuwa ni the same issue, top cover seal? Nilifanya oil service. Nimetembea almost 3,000 Km, na sasa dipstick inasoma oil imo nusu! Oil imevujia sana all over the cover.

View attachment 3168314
View attachment 3168316
View attachment 3168318


Pia, pale zinapoingia AC pipes panaonekana kuvuja hivi (not oil). 👇🏾👇🏾
View attachment 3168322

stephot , naomba maoni yako hapa mkuu. Niko wilaya mkoani (remote area), mafundi huku ni mtihani.

Nimekuta hiyo hali juzi.
 
Jipunguzie vitu vya kuweka kichwani,
Kaz kama iyo peleka kwa wataalam wakusaidie.
Hii mambo ya kupiga pic af ukataka msaada utajikuta unaharibu zaidi

Ni km mtu unaumwa tumbo afu unataka msaada wakat tumbo linaweza uma kutokana na sababu kibao utashauriwa dawa ya minyoo kumbe una apendex
 
Jipunguzie vitu vya kuweka kichwani,
Kaz kama iyo peleka kwa wataalam wakusaidie.
Hii mambo ya kupiga pic af ukataka msaada utajikuta unaharibu zaidi

Ni km mtu unaumwa tumbo afu unataka msaada wakat tumbo linaweza uma kutokana na sababu kibao utashauriwa dawa ya minyoo kumbe una apendex
Nonsense! Kama hauna any idea ya suala husika, kaa kimya. Siyo lazima useme/uandike. Save your energy!

Mimi siyo mjinga kuja kwanza hapa jf ili kupata ABCs kabla sijaenda kwa hawa mafundi wa huku nilipo. Nilipo hakuna watalaamu, kuna mafundi.

FYI, JF imenisaidia mambo mengi sana positively zaidi ya 100%.
 
Kichuguu , naomba maoni yako mkuu.
Oil hiyo inavuja kutoka kwenye cylinder head ndiyo maana ifunika cylnder head yote. Ni vigumu kukupa diagnosis kamili bila kuikagua injini wakati inaunguruma. Hata hivyo hizo injini za VVT-i zina oil control valves ama moja au mbili juu ya cylinder head, moja ikiwa kulia na nyingine kushoto. Wasiwasi wangu ni kuwa o-rings za hizo oil control valves hizo zimekauka hivyo hazibani sawasawa na kuasababisha oil ivuje juu ya cylinder. Ama sivyo valve zenyewe ndizo zimekufa zinarudisha oil nyuma na kuivujisha kwenye cylnder head.

Kagua hizo valves ikiwezekana ubadilishe valve nzima siyo o-rings tu. Picha ulizoweka hazionyeshi sawasawa kwe vile zimechukuliwa upande mmoja tu wa injini ambapo sijui kama ni kulia au kushoto. Ingekuwa vizuri kama ningeona kutokea pande zote mbili: kulia na kushoto. Sasa hivi shughulika na hizo oil control valves tu, tena upate genuine kwani ukipata aftermarket zinaweza zisilingane sawasawa na tundu la kwenye injini na kusababisha uvujaji uendelee.
 
Oil hiyo inavuja kutoka kwenye cylinder head ndiyo maana ifunika cylnder head yote. Ni vigumu kukupa diagnosis kamili bila kuikagua injini wakati inaunguruma. Hata hivyo hizo injini za VVT-i zina oil control valves ama moja au mbili juu ya cylinder head, moja ikiwa kulia na nyingine kushoto. Wasiwasi wangu ni kuwa o-rings za hizo oil control valves hizo zimekauka hivyo hazibani sawasawa na kuasababisha oil ivuje juu ya cylinder. Ama sivyo valve zenyewe ndizo zimekufa zinarudisha oil nyuma na kuivujisha kwenye cylnder head.

Kagua hizo valves ikiwezekana ubadilishe valve nzima siyo o-rings tu. Picha ulizoweka hazionyeshi sawasawa kwe vile zimechukuliwa upande mmoja tu wa injini ambapo sijui kama ni kulia au kushoto. Ingekuwa vizuri kama ningeona kutokea pande zote mbili: kulia na kushoto. Sasa hivi shughulika na hizo oil control valves tu, tena upate genuine kwani ukipata aftermarket zinaweza zisilingane sawasawa na tundu la kwenye injini na kusababisha uvujaji uendelee.

Shukrani sana mkuu kwa maoni. Nimepata mwanga. Ahsante
 
Back
Top Bottom