Nini kifanyike kufufua Tanzania International Petroleum Refinery (Tiper)?

Nini kifanyike kufufua Tanzania International Petroleum Refinery (Tiper)?

mwanamichakato

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,090
Uagizaji mafuta toka nje unaigharimu nchi yetu mabilioni ya fedha kila mwaka hivyo kudidimiza thamani ya fedha yetu na uchumi Kwa ujumla.

TIPER-Tanzania International Petroleum Refinery ni kampuni ilioundwa mahsusi Kwa ajili ya kusafisha mafuta ghafi. Mitambo ya thamani kubwa ilinunuliwa na kusimikwa pamoja na storage terminals Za kutosha pale Kigamboni.

Tumebinafsisha..Serikali imebakiwa na nadhani 30%..Nini kinafanyika?Nini kifayike?
 
Ubinafsishaji uliua icho kiwanda. Imagine dingi yangu ananiambia alianza kazi miaka ya 70 anatumia gesi mimi leo japo nina kazi jiko la gesi nalitumia huku nawaza isiishe fasta maana kujaza gesi ni gharama.
 
Mh. Mwanamichakato, sijui nikuite ni mzalendo, ama umekuwa na mawazo ya kizalendo.

Ni kweli tukiwa na petroleum refinery industry yetu, hakika tutapunguza sehumu kubwa sana ya gharama za uagizaji wa petroli, dizeli, oil pamoja na bidhaa mbali mbali zitokanazo na usafishaji wa crude oil petroleum.

Hebu tujiulize hasa sisi wa gen. wa miaka ya 50s, 60s, ni kwa nini TIPER iliuliwa?

Wengine wanasema ati ni sababu TIPER wakati inajengwa, idadi ya WaTanzania ilikuwa na ndogo, wengine wakasema ati technology ilishapitwa na wakati.
Hizo zote zilikuwa ni sababu za kuhalalisha upigaji tu.

Tunapo waambia nchi hii, TANZANIA upigaji ulianza zamani na sasa imekuwa kansa sugu, huwa hamuelewi.

Ni jambo jema sasa kuianzisha TIPER mpya sasa tukilenga na usafishaji wa mafuta (crude oil petroleum toka Uganda kwa Bomba linalojengwa sasa, ni kweli tutapunguza ama tutashusha bei za bidhaa za petroleum.

Je, viongozi wetu waliona hili? Wanayo mawazo haya ya kizalendo? Je, nao wanamawazo hayo hayo ya kipigaji?

Ndugu Mwanamichakato, nakuomba fanya re-search kidogo tu juu ya mampuni yenye kibali cha kuagiza bidhaa za petroleum toka nje, je, hakuna mikono mingi ya viongozi wetu wengi kwenye makampuni hayo?

Mwl. Nyerere (RIP) alisema, mtu akila nyama ya mtu hawezi kuacha. Je, na hawa viongozi wetu walishakula nyama ya mtu, ni kweli watakumbuka wazo hili la kujenga TIPER nyingine?

Siku hizi wao wanaita kulamba ASALI, je wataacha? Siku hizi kuna wazo la kusema tunawakaribisha wawekezaji, (wakoloni mamboleo) , je, hata hilo wazo wanalo?

Huenda tutapata ukinzani mkubwa toka nje, hasa wale watuuziao bidhaa za petroleum, hivi ni kweli?

Kama sivyo, ama ndivyo, tutawasaidiaje hawa viongozi wetu?
 
Mipango miji mmeshindwa ndo mtaweza kujisamamia na kuendesha miradi yenye kuhitaji akili kubwa.Botha alikuwa sahihi kabisa kuwaondoa watu weusi kwenye mipango ya maendeleo ya SA.
 
Hebu tajeni haswa sababu za hiyo Refinery kufa....wekeni na ushahidi...
Sababu hata 4 tu...

Mada nzito kama hii siyo mnaijibu kiuwepesi kama mabishano ya mpira....

Baada ya hapo ndipo uje ushauri wa kukifufua....
 
Uagizaji mafuta toka nje unaigharimu nchi yetu mabilioni ya fedha kila mwaka hivyo kudidimiza thamani ya fedha yetu na uchumi Kwa ujumla.

TIPER-Tanzania International Petroleum Refinery ni kampuni ilioundwa mahsusi Kwa ajili ya kusafisha mafuta ghafi. Mitambo ya thamani kubwa ilinunuliwa na kusimikwa pamoja na storage terminals Za kutosha pale Kigamboni.

Tumebinafsisha..Serikali imebakiwa na nadhani 30%..Nini kinafanyika?Nini kifayike?
Eneo hilo la kiwanda apewe buludoza alitumie kuponya watu kama pale Tanganyika Pekazi.
 
Kosa kubwa nchi za Afrika zilifanya ni kuamini fikra za wakoloni. Kubinafsisha kila kilichokuwa na maslahi ya wachache.
 
Kosa kubwa nchi za Afrika zilifanya ni kuamini fikra za wakoloni. Kubinafsisha kila kilichokuwa na maslahi ya wachache.
Mkoloni kaondoka Miaka zaidi ya 60 iliyopita ila leo viongozi 53 wote wameitwa kwa Mkoloni Mpya Mchina, Beijing.
 
Ndiyo hayo mashirika yanayotakiwa kuuzwa ikiwa yanaendeshwa kwa hasara!
 
Na ubabaishaji wetu huu wote tuifufue tipper ili iweje? Nani aiendeshe? Tumeshindwa kuendesha karibu kila kitu, vyote vimekufa; tufufue tipper kwa manufaa ya nani? Tumekalia ufisadi, wizi, uzembe, majungu; hakuna kitu hata kimoja tunachofanya kwa ufanisi: huo uendeshaji kwa ufanisi wa tipper tutauiba toka wapi?
 
Tiper ingekuwa na manufaa kama mafuta yangekuwa yanachimwa nchini. Kuagiza mafuta ghafi na kuyasafishia nchini ni bora kuagiza mafuta safi moja kwa moja.

Ni sawa na ilivyo kwa bidhaa nyingine kwa sasa; it is by far cheaper kuagiza bidhaa yoyote toka nje (China for example) kuliko iliyotengenezwa nchini. Cost of production Tz ni kubwa sana! Hoja ingekuwa kupunguza gharama za uzalishaji.
 
Uagizaji mafuta toka nje unaigharimu nchi yetu mabilioni ya fedha kila mwaka hivyo kudidimiza thamani ya fedha yetu na uchumi Kwa ujumla.

TIPER-Tanzania International Petroleum Refinery ni kampuni ilioundwa mahsusi Kwa ajili ya kusafisha mafuta ghafi. Mitambo ya thamani kubwa ilinunuliwa na kusimikwa pamoja na storage terminals Za kutosha pale Kigamboni.

Tumebinafsisha..Serikali imebakiwa na nadhani 30%..Nini kinafanyika?Nini kifayike?
Well, waulize PSRC , ZITTO watakusaidia, or else chukua sababu za kufa kw mashirika zigeuze ziwe strength.

1. Kama sasa hvi mashirika yanaongozwa na mapro-pesa na madaktari na yanakufa , tuweke akinanni?
 
Back
Top Bottom