Somo la Hisabati kama linavyofahamika ktk shule za msingi si somo gumu, lakini ni somo ambalo ili mwanafunzi alifauru ni lazima alipende. Kwa wanfunzi kupenda somo kunajengwa na sababu nyingi. Nitazitaja chache tu
1. Mwl anayemfundisha mtoto katka madarasa ya awali(darasa la I, II na III). Awe mwenye competent teaching skills.
2. Mazingira ya kujifunzia (vitabu na mazoezi yanayosimamiwa kwa karibu...exercises with close supervision)
3. Walimu wenye ari na moyo wa kuwaelewesha wanafunzi katk madarasa yanayofuata nk.
Mtoto anaanza kupenda hesabu au kuzichukia akiwa katika madarasa ya 3 na 4, katka madarasa haya akiwa na walimu wazuri wenye ari na moyo wa kufundisha watazingatia hayo nilotaja hapo juu na mwanafunzi ataendelea kupenda somo la hesabu. Lakini suala la kufikiri kuwa mwanafunzi atapenda hesabu akiwa secondari ni kujidanganya. Madarasa ya 5 6 na 7 na hatimaye secondari ni matokeo ya msingi uliotengenezwa ktk shule ya msingi; ndio maana mtoto aliyekuwa anafanya vizur hesabu shule ya msingi ataendelea kupenda hesabu akifanikiwa kufundishwa na mwl mwenye ari na moyo wa kuelewesha ktk shule ya secondari na kuendelea!