Nini kilibadalisha Msimamo wa Tanzania kuhusu Palestina!

Nini kilibadalisha Msimamo wa Tanzania kuhusu Palestina!

MAKULUGA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2011
Posts
7,828
Reaction score
10,527
Salamu,

Dunia inaenda kasi sana! Tulipokuwa wadogo tukifuatilia na kufundishwa harakati za ukombozi Afrika na dunia, tulijifunza (lau kidogo) uhuru na haki ya Wapelestina. Tulisoma kuhusu Yassir Arrafat na Palestine Liberation Army (PLO). Wakati huo, kama ilivyokuwa kwa POLISARIO cha Sahara Magharibi, Tanzania ilikuwa inaunga mkono PLO dhidi ya Israel.

Kumbuka wakati huo tulikuwa hatufungamani na upande wowote! Leo hii, siasa zetu kuelekea mzozo wa Mashariki ya Kati hazieleweki! Nafikiri sasa ndio hatufungamani na upande wowote! Kulitokea nini, au ulikuwa ni msimamo wa Mwalimu Nyerere? Hivi vuguvugu la POLISARIO lilishaje?

Leo hii nipo mtu mzima, lakini nipo nyuma kwa siasa za dunia kuliko nilipokuwa shule ya msingi! Sijui nini kimenikumba! Na nini kimelikumba taifa!
 
Sasa hivi tuko kwenye uhusiano/diplomasia ya uchumi, hatufungamani na yoyote yule. Kwa maana ya adui wa nchi A hawezi kuwa adui yetu pia. Sisi tutaangalia maslahi yetu kama nchi kwa nchi hiyo bila kujali uhasama wa pande zake. Ndio maana leo hii Tanzania ina mahusiano na Morocco, ambao wanaishikilia sehemu ya nchi ya Sahara Magharibi.

Na hata alipokuja kiongozi wa nchi ya Sahara kwenye mkutano wa CCM juzi, nadhani alielezwa msimamo wa Tanzania, akarudi kwao kimya kimya.

Vilevile, hali iko hivyo kwa Israel na Palestine. Sisi wote hao ni marafiki zero kidiplomasia kulingana na manufaa tunayoyapata kama nchi kutoka pande zote.
 
Nadhani baada ya Palestine kuyageuka makubaliano ya Oslo ya 1993. yaliyotaka makao yao makuu yawe East Jerusalem na Israel makao makuu yao makuu yawe West Jerusalem . Wao wakataka Jerusalem yote iwe Makao makuu ya Palestine
 
Nadhani baada ya Palestine kuyageuka makubaliano ya Oslo ya 1993. yaliyotaka makao yao makuu yawe East Jerusalem na Israel makao makuu yao makuu yawe West Jerusalem . Wao wakataka Jerusalem yote iwe Makao makuu ya Palestine
yale makubaliano yangefanya pande zote ziheshimiane na kuishi kama majirani, ila misimamo mikali ya kiarabu inayochochewa kidini ndio imewatetea shida wapalestina, sikuzote akili mbovu za viongozi huleta maumivu kwa wananchi waa kawaida.
 
Back
Top Bottom