Nini kimeikumba Mtibwa Sugar!

mrubwavwasy

Senior Member
Joined
Apr 14, 2021
Posts
138
Reaction score
229
Nmekuwa mpenzi na shabiki wa Mtibwa miaka 4 iliyopita, Enzi za akina Mzamiru, Mtibwa inapiga soka safi na pia kuibua vipaji bora kabisa.

Ila nmefuatilia takriban mechi 10 zilizopita, Mtibwa si ile nnayoifahamu, wachezaji hawajitumi na pia wengi siyo type ya Mtibwa nnayoifahamu, wanacheza kama timu ya daraja la kwanza.

Kwa hichi kiwango wanachoonyesha nasikitika kusema kuwa Mtibwa bye bye ligi kuu!
 
Usishangae timu nzima iyo wachezaji wake ni wa kushikwa mkono.
 
Timu haina mwalimu wa maana kwa sasa! Wamrudishe Meck Mexime, jamaa anaijua vema Mtibwa sugar! Na Jamali Baysal aongeze bajeti kwa ajili ya timu sambamba na kutafuta wadhamini wengine wakubusti uchumi wa timu! Mungu aisaidie Mtibwa isishuke daraja!
 
Lazima washuke kidogo alafu watajipanga wataanza upya kupanda tena,Mtibwa ilidumu top 5 kwa muda mrefu na wametikisa timu kongwe zote kwenye ligi yetu hii.
 
bora ishuke daraja maana imekuwa ndio inaharibu soka la tanzania Kwa kutuletea wachezaji wengi wafupi vindurutu kazi kuwapiga misumari wenzao. tunataka wachezaji wenye malengo ya mbali sio kutamani simba na yanga tuu
 
Timu nzima inasajili wazanzibar , wazanzibar wanapata wapi uwezo wa kucheza ligi ngumu kama VPL, ni wa kubahatisha sana sasa wao mtibwa kikosi kizima. Huwezi kuwa na timu imara kwa kusajili wala urojo.
 
bora ishuke daraja maana imekuwa ndio inaharibu soka la tanzania Kwa kutuletea wachezaji wengi wafupi vindurutu kazi kuwapiga misumari wenzao. tunataka wachezaji wenye malengo ya mbali sio kutamani simba na yanga tuu
Huyo scout wa mtibwa anayescout wachezaji wa futi mbili sijui wanamlipa Shillingi ngapi ?

Hao wachezaji futi mbili mtibwa wanatoa wapi ?
 
Huyo scout wa mtibwa anayescout wachezaji wa futi mbili sijui wanamlipa Shillingi ngapi ?

Hao wachezaji futi mbili mtibwa wanatoa wapi ?
Type za kina Kibwana, Kichuya, Aisee! Nilimcheki Hassan Kessy Jana alivyopewa mwili na Chama, dah!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…