Nini kimemkuta Ommy Dimpoz?

Christopher Wallace

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2015
Posts
1,479
Reaction score
3,788
Wanaukumbi kwema,

Leo naombeni mnijuze nini kimemkuta mwanamuziki Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz ambaye kuna kipindi tuliaminishwa kuwa atakuja kumzidi kama sio kumfunika na kumpoteza kabisa Diamond.

Ikumbukwe Ommy Dimpoz alianza vizuri kwa kutoa vibao matata kama Nainai, Baadae, Tupogo na Ndangushima. Baada ya hapo ametoa nyimbo zilizoshindwa kutamba kabisa...mfano mzuri ni Wanjera. Kwasasa dimpoz amepotea na kafunikwa na vijana wadogo akina Rayvan na Harmonize, Je ni nini kimemsibu staa huyu aliyekuwa anafananishwa na Diamond kwa uwezo wake Kimuziki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…