Hakuna cha bahati, wala clouds kuvimba
-Msanii unatakiwa uingie studio utoe ngoma kali, utoe video kali, vipate airtime (na uzuri tu vituo ni vingi saana tvs na radios) kama mwanamuziki mchanga ndio ikutambulishe kama ilivyo basi nenda kwa mo music, na kama tayari umetoboa basi ikuongezee mashsbiki n.k ....
-Tofauti na kutoa ngoma, awe na interval nzuri ya jinsi ya kuachia ngoma zake ili awe kwenye media muda woote, na kuhakikisha anapush zipokelewe na kupata airtime ya kutosha
-Msanii anatakiwa kuwa na mahusiano mazuri na wasanii wenzake na wadau wa burudani. Hapa ndio mwanzo wa kupata support ya promo ya kazi zako, kupeana maujanja, ushauri na kupata shows ambazo ndio chanzo kikuu cha mapato ya wasanii wetu
-Msanii anatakiwa ajibrand, lazima afanye vitu vya kumuweka awe kama chumvi kwenye mboga, mitandaoni usimtafute kwa tochi, awe gumzo, watu wamuelewe zaidi ya kusikiliza tu nyimbo zake ili hata akija kukwambia bila mil 15 sifanyi show promoter ajiongeze
HUYO NDIO MSANII, SIO UNAISHIA KUSEMA NINA KIPAJI TU UNATAKA KIPAJI KIJIUZE UNASAHAU BONGO STAR SEARCH NA TUSKER PROJECT FAME VIJANA NI WAKALI WANATOKA KILA MWAKA ILA HAIELEWEKI WANAKWENDA WAPI.. GAME IS FAIR ENOUGH KAMA UTAENDANA NALO..