DOKEZO Nini kinaendelea Kampuni ya Mapembelo Cargo? Tunalalamika kila siku mizigo yetu tuliyoagiza haifiki

DOKEZO Nini kinaendelea Kampuni ya Mapembelo Cargo? Tunalalamika kila siku mizigo yetu tuliyoagiza haifiki

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
Kuna sintofahamu inaendelea kuhusu Kampuni ya Mapembelo Cargo ambayo najihusisha na usafishaji wa mizigo, wamekuwa kimya sana kuhusu mizigo ya wateja wao.

Kuna Wafanyabiashara na Watu wengine ambao waliagiza mizigo kwa mambo binafsi, huu ni mwezi wa nne hawajapata mizigo yao kutoka China. Mimi nina miezi miwili nafuatilia mizigo yangu ambayo niliambiwa imeshafika tangu Oktoba 2024.

Ukiwasiliana nao wanakwambia “Wiki hii mzigo utatoka kulikuwa na changamoto Bandarini”, baada ya hapo wanapotea unaona kimya.

Hali hiyo inatuumiza sisi Wafanyabiashara, hawatupi majibu ya kueleweka na hatujui hatma ya mizigo yetu, mwisho wake mitaji inapotea kwa kuwa hakuna tunachoingiza.

Tunaomba Mamlaka husika ziingilie tujue nini kinaendeleaa. As we speak nasikia wamefilisika, sasa je, mizigo ya Wafanyabiashara inakuwaje? Si waseme ukweli kuliko kutupotezea muda.
JJ (1).png

JJ (2).png

JJ (3).png

JJ (4).png

JJ (5).png

JJ (6).png

JJ (7).png

JJ (8).png
 
Nikuhakikishie tu bandarini hamna changamoto kubwa tena,angalao ndani ya siku 7 meli inashusha hivyo suala la bandarini si kweli.

Loose Cargo imekumbwa na fitna nyingi na viboko vya Customs(vilivyo halali) hivyo kampuni nyingi zinaelekea shimoni.

Ni ushauri wangu kwa wafanyabiashara ,badala ya kutumia hizi kampuni tumieni groupage.Hii inapunguza gharama na mnakuwa na taarifa sahihi za mzigo wenu.Lakini pia inapunguza gharama sana.CBM moja haitazidi usd 350.
 
Onhoo pole kwa uliyeagiza miti krismass umebakiza siku chache biashara yako isubiri mwakani mwezi kama huu
 
Nikuhakikishie tu bandarini hamna changamoto kubwa tena,angalao ndani ya siku 7 meli inashusha hivyo suala la bandarini si kweli.
Loose Cargo imekumbwa na fitna nyingi na viboko vya Customs(vilivyo halali) hivyo kampuni nyingi zinaelekea shimoni.

Ni ushauri wangu kwa wafanyabiashara ,badala ya kutumia hizi kampuni tumieni groupage.Hii inapunguza gharama na mnakuwa na taarifa sahihi za mzigo wenu.Lakini pia inapunguza gharama sana.CBM moja haitazidi usd 350.
Grouppage inakuwaje mkuu
 
Inasemekana hiyo kampuni imefilisiaka na wamegawana hizo bidhaa zenu.peleni sana.msirndelee kutumia hii kampuni imekuwa ya kutapeli.
 
Labda wanasubiri uhakiki wa wahanga wa ghorofa Kariakoo wasije kutoa mzigo kwa mtu asiyestahili. Si unajua kila kitu fursa siku hizi!!!
 
Tatizo Huwa tunafuata urahisi wa bei ndio matokeo yake hayo
 
Naona hata Tosh wanastrugle kudeliver on time nowadays. Kuna fitina pale bandari itakuwq ya makusudi, na tutegemee kukutana na kampuni mpya kubwa mwaka 2025
 
Mapembelo wamefilisika..sio huku tuu hata kwenye route za magari walizokuwa wanafanya nchini.
 
Ukitoa Silent Ocean hao wengine changamoto sana. Sisi watu weusi hatuna consistency kwenye ubora wa kazi.
 
Back
Top Bottom