Nini kinaikumba Japan? Mwakani India inaipiku na kuwa Taifa la tatu lenye uchumi mkubwa Ulimwenguni

Nini kinaikumba Japan? Mwakani India inaipiku na kuwa Taifa la tatu lenye uchumi mkubwa Ulimwenguni

Nadhani suala kubwa hapa ni population ya India inazidi kuwa kubwa huku population ya Japan ikiendelea kuporomoka.

India ni taifa lenye idadi kubwa ya watu duniani ukichagiza na maendeleo ya science na technology ni suala la muda tu kabla Japan haijatupwa nje ya kumi bora.

Nchi kama Brazil zinaweza kuipiku Japan muda si mrefu sana.
Population ni suala mojawapo ila sio suala kubwa,
Masuala makubwa ni deflation na banking crisis zilizoikumba Japan.
 
Japani ilipitwa na China 2010 na kutoleqa nafasi ya pili, kumbuka Japani imekaa nafasi ya pili kwa miaka 40.

Sasa mwakani tena inatolewa nafasi ya 3 hivyo kuangukia nafasi ya 4 ambayo nayo huenda ikaja kuotelewa tena.

Ninacho kiona Japani ni kufuata mkumbo wa USA, mfano India kwa sasa anapata mafuta kwa bei chee sana kutoka Urusi, Ilihali Japani yeye akiwa ameungana na Marekani kuiweka Urusi vikwazo amnavyo vinaithori sana Japani.
View attachment 3160033
Unaweza kupigwa na India utajiri lakini watu wako wakawa matajiri kuliko wahindi
 
Uchumi wa Japan haujaanguka ila Uchumi wa China na India imekua unakua sana sababu ya kubadili siasa na kufanya uchumi kukua haraka kuelekea kwenye usawa na uwezo wao ambao ni mkubwa Sasa ila ulikua umelala.
Sama majitu yameamka
 
The high the population, the high the economy. India ina population kubwa ambayo ni more productive ikilinganishwa na Japan iliyojaa wazee na vijana wachache.
Sio kweli,
Nigeria, Bangladesh, Pakistan na Ethiopia hazina uchumi mkubwa wakati zina population kubwa.
Ujerumani, South Korea, UK, Ufaransa, Spain, Canada, Netherlands na Switzerland zina uchumi mkubwa zikiwa na population ndogo.
 
Hii tabia ya kufuata mkumbo wa Marekani kumeiponza Ujerumani ,sasa hivi uchumi wa Ujerumani unapumlia mashine na unakaribia kuanguka.
Yaani viongozi wa Ujerumani ni wasenge sana yaani wanashauliwa na Marekani wasinunue gesi na mafuta ya Urusi yenye bei ndogo alafu yeye ana anawauzia gesi yenye bei kubwa mara 4 ya ile ya Urusi.

Huu usenge nchi nyingi ziliukataa,kuanzia Uturuki , Indonesia,India,China hata Italy ambaye ni kibaraka mwenzao aliukataa huo usenge.
Umechanganyikiwa na ushabiki uchwara.
 
- Sababu za japan kushuka kiuchumi ipo Ki demographia zaidi, ina idadi kubwa ya Wazee ambao ni tegemezi japo pia wanatumia sana Robotics kwenye uzalishaji
Uchumi wa Japan haujashuka bali haukuendelea kukua sana kuanzia miaka ya 1990, sababu kubwa ni deflation na banking crisis, demographics ni nyongeza tu.
 
Pia Japan imejaa wazee! Mambo ya uzazi wa mpango usio na mpango umejibu.
Mbaya zaidi, Japanese wanajiona watu maalumu hawana utamaduni wa kukaribisha wageni - ni wabaguzi.
Wanazo kazi za watu wachini (weusi) wahamiaji wanase ni 4D, yaani Dirty, Dangerous, hizo D2 nimesahau.

Waombe Muungano na nchi za Afrika kuondoa tatizo la population.
 
Umechanganyikiwa na ushabiki uchwara.
Ww ndo unaendekeza ushabiki uchwara kwa kutokubali ukweli mchungu hasa unapo wahusu wamagharibi unao waona kama miungu wako.
Kwa hiyo ni uongo kuwa uchumi wa Ujerumani kwa sasa unapitia kwenye myumbo?
Kwa hiyo ni uongo kuwa mamia ya viwanda nchini Ujerumani havijafungwa kwa sababu gharama za uzalishaji kuwa juu hivyo kushindwa kuendana na ushindani wa soko la dunia?
Kwani ni uongo kuwa kwa sasa Ujerumani kuna mfumko mkubwa wa bei?
Kwani ni uongo kuwa serikali ya Shoz imeanguka na kulazimika kuitisha uchaguzi wa mapema?
 
Ww ndo unaendekeza ushabiki uchwara kwa kutokubali ukweli mchungu hasa unapo wahusu wamagharibi unao waona kama miungu wako.
Kwa hiyo ni uongo kuwa uchumi wa Ujerumani kwa sasa unapitia kwenye myumbo?
Kwa hiyo ni uongo kuwa mamia ya viwanda nchini Ujerumani havijafungwa kwa sababu gharama za uzalishaji kuwa juu hivyo kushindwa kuendana na ushindani wa soko la dunia?
Kwani ni uongo kuwa kwa sasa Ujerumani kuna mfumko mkubwa wa bei?
Kwani ni uongo kuwa serikali ya Shoz imeanguka na kulazimika kuitisha uchaguzi wa mapema?
Na haya yote yametokea kwa sababu Ujerumani imefuata "mkumbo" wa Marekani??
 
Na haya yote yametokea kwa sababu Ujerumani imefuata "mkumbo" wa Marekani??
Hayo yote yametokea baada ya Ujerumani kusikiliza tumba za Marekani kuhusu kuachana na nishati ya bei rahisi kutoka Urusi badala yake akaenda kununua nishati ya bei kubwa sana kutoka Marekani.
 
Hayo yote yametokea baada ya Ujerumani kusikiliza tumba za Marekani kuhusu kuachana na nishati ya bei rahisi kutoka Urusi badala yake akaenda kununua nishati ya bei kubwa sana kutoka Marekani.
Acha ukasuku,
Nusu ya nishati ya ujerumani ni kutokana na renewable sources(upepo, solar na maji), makaa ya mawe yanafuatia na wananuna kila mahali duniani, Norway ndio supplier mkubwa zaidi wa gas Ujerumani.
 
Acha ukasuku,
Nusu ya nishati ya ujerumani ni kutokana na renewable sources(upepo, solar na maji), makaa ya mawe yanafuatia na wananuna kila mahali duniani, Norway ndio supplier mkubwa zaidi wa gas Ujerumani.
Sasa kama wana siasa wa wenye Ujerumani yao wana sema kuwa kina endelea ni kutokana na ombwe la gesi ya Urusi ,ww mlala hoi kutoka mbagala unabisha nn?
Kabla ya vita ya Ukraine kuanza %40 ya nishati iliyo kuwa inatumika Ujerumani ilikuwa inatoka Urusi.
 
Badala ya kujiuliza Japan kimewakumba Nini, unaweza vile vile waweza jiuliza India wana Siri gani ya maana hiyo nafasi aliyopo India kwa hivi sasa alikuwa UK nae kapigwa kibega na India
Nadhani demographic factors zinambeba zaidi India, ambazo ndio hizo hizo zinazomuangusha Japan
Umechangia kiuchumi ndugu. Wasiosoma uchumi hawataelewa hata kidogo
 
Nchi zilizokuwa zinategemea sana export za viwandani hali ni tete baada ya ujio wa China. Ujerumani na Japan sekta yao ya magari inaenda shimoni baada ya EVs za China kushika kasi. Kingine ni kuwa hazikuwekeza kwenye digital world. Pia gharama za uzalishaji kwenye hizi nchi zilizoendelea sana ni balaa.
 
Nchi zilizokuwa zinategemea sana export za viwandani hali ni tete baada ya ujio wa China. Ujerumani na Japan sekta yao ya magari inaenda shimoni baada ya EVs za China kushika kasi. Kingine ni kuwa hazikuwekeza kwenye digital world. Pia gharama za uzalishaji kwenye hizi nchi zilizoendelea sana ni balaa.
Kwani wao wanaahindwa kuinda EVs kama za China?

Hiyo sio sababu ya msingi
 
Hii ni kawaida katika cirle ya maisha.
Itafikia kipindi hata nchi za Kiafrika zitakuwa juu sana kiuchumi ikilinganishwa na nchi za Ulaya.
Dunia ipo katika movement/rotation hivyo aliye juu atakuja kushuka na aliye chini atapanda juu.
Kumbuka pia kuna 'reincarnation'
Kuna changamoto kadhaa zinaikabili Japan zinazoweza kuchangia India kuipiku kiuchumi na kuwa taifa la tatu lenye uchumi mkubwa duniani.

1. Idadi ya Watu Kupungua na Kuzeeka
Japan inakumbwa na tatizo la idadi ya watu kupungua kwa kasi na idadi kubwa ya wazee.
Hali hii inasababisha kupungua kwa nguvu kazi, ambayo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi.

Nchi inakabiliwa na mzigo mkubwa wa gharama za kijamii kama pensheni na huduma za afya kwa wazee.

2. Ukuaji wa Taratibu wa Uchumi
Uchumi wa Japan umekuwa ukikua kwa kasi ndogo kwa miaka kadhaa. Hali hii imetokana na ukosefu wa uvumbuzi mkubwa wa kiuchumi, kiwango cha chini cha matumizi ya ndani, na deni kubwa la serikali.

3. Kushuka kwa Nguvu ya Viwanda
Ingawa Japan imekuwa kitovu cha teknolojia na magari, ushindani kutoka nchi kama Korea Kusini, China, na hata India unafanya nafasi yake kupungua katika soko la kimataifa.

4. Mabadiliko ya Kidunia
India inafaidika na idadi kubwa ya watu vijana, ukuaji wa sekta ya teknolojia ya habari, na soko kubwa la ndani.
Ukuaji huu wa kasi unaiweka India katika nafasi nzuri ya kuipiku Japan.

5. Tofauti Kati ya Japan na India
- Japan: Inategemea sana mauzo ya bidhaa za hali ya juu kama magari na vifaa vya elektroniki. Lakini soko la ndani linaendelea kudumaa.

- India: Ina uchumi unaokua kwa kasi kutokana na viwanda, huduma za teknolojia ya habari, na soko kubwa la watumiaji.

Hivyo, ikiwa hali itaendelea kama ilivyo, India itaipita Japan kiuchumi mwakani, hatua inayoweza kuimarisha ushawishi wake kimataifa.

Ova
 
Back
Top Bottom