Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,713
- 6,121
Habari za wakati huu,
Ni matumaini yangu kwamba unaendelea vyema na maisha yako ukiendelea kuzifikia ndoto zako.Katika safari yangu ya ujasiriamali na biashara ambayo ina umri wa zaidi ya miaka 20 ni mefanya aina nyingi sana za biashara. Nimefanya biashara ya maduka ya nguo,maduka ya chakula, Biashara ya bar na hata biashara ya jiko la chipsi n.k.utoaji wa huduma mbalimbali,maduka ya spea za magari,pikipiki hata nimefanya biashara katika sekta ya elimu na hata udalali wa nyumba na mashamba.
Najua unaweza kushangaa inakuwaje nimefanya biashara za aina nyingi hivi?Well katika maisha kuna hatua na katika kila hatua unajikuta unakumbana na hustles ambazo zinakufanya uingie katika aina fulani ya biashara kwa muda mfupi au muda mrefu. Najua siko mwenyewe ambaye ninafanya biashara za aina tofauti ila najua kuna watu ambao kabisa hawajawahi hata kujaribu kufanya biashara. Swali la kujiliza ni JE nikitu gani kinakufanya na wewe usianzisha kabiashara kako hata kama ni kadogo?Je ni Mtaji?Je ni wazo la biashara huna?Je ni muda?Je ni uwezo wako wa kiakili ni mdogo?Je ni fursa hauzioni?Ni kitu gani kinakuzuia kufanya biashara?
Kila mtu anazo sababu zinazomfanya asianzisha biashara.Ila leo nataka nikwambie ni kwa nini ni muhimu uanzisha kabiashara kako.Hata kama ni kadogo.Siku hizi kuanzisha biashara ni rahisi sana.Kuendesha na kusimamia biashara ni rahisi sana.Unapokaa bila kuwa na Biashara unapishana na FURSA ambazo utakuja kuzikumbuka.
Jaribu kufikiri kampuni kama za FACEBOOK(META),GOOGLE(ALPHABET),TWITTER,TIKTOK na kampuni nyingine kama hizo halafu ujiulize iwapo zina tofauti yeyote.Hizi zote ni kampuni za TEHAMA ambazo kiuhalisia zinadeal na Taarifa tu.Ni kampuni ambazo ni kubwa sana na zinaingiza mabilioni ya PESA.Swali ni JE unafikiri uanzishwaje wake ulikuwa mgumu au mrahisi?
Ukizitazama hizi kampuni unaweza kufikiri kuzianzisha ilikuwa kazi ngumi il ilikuwa kazi rahisi sana.Ilifanywa na mtu mmoja au wawili ambao waliamini katika wazo lao na kutenga muda na rasilimali zao kulipa wazo lao nguvu.Baada ya hapo sote tunajua kilichotokea.
Biashara yoyote inaanza na wazo na kuliamini wazo lako.Mawazo ya biashara yako mengi na yote yanaweza kukuingizia kipato tena cha kutosha kabisa. Swali la kujiuliza ni Je unaliamini wazo lako?Hapo ndipo ambapo wengi wetu hukwama. Kwani sisi wenyewe tunakuwa hatuamini katika wazo na uwezo wetu na matokeo yake ni kwamba tunapokutana na changamoto yoyote ni rahisi kufikiri kwamba tumefikia Mwisho kumbe bado ni mwanzo tu.
Wazo lolote la biashara ni lazima ulifanyie "Validation" Hii unaweza kufanya kwa kuangalia wengine wanafanya nini katika eneo hilo au unaweza kulipeleka sokoni kwa baadhu ya wateja ili uone iwapo litawafaa na unaweza.Kumbuka usipolifanyia wazo lako validation ni vigumu sana wewe kuelewa kwa kina aina ya biashara na changamoto zake.
Katika mjadala huu nimechokoza kidogo tu kuhusu kile kinachotuzuia kuanzisha biashara na namna ambavyo tunaweza kuvuka changamoto.Hata hivyo naamini kwamba yako mengi ambayo yanawazuia watu wasianzishe biashara. Karibuni tujadili kwa pamoja Juu ya yale ambayo yanatuzuia kuanzisha biashara na namna ambavyo tunaweza kuyashinda na kuibua mawazo na fursa mpya.
Karibuni
Ni matumaini yangu kwamba unaendelea vyema na maisha yako ukiendelea kuzifikia ndoto zako.Katika safari yangu ya ujasiriamali na biashara ambayo ina umri wa zaidi ya miaka 20 ni mefanya aina nyingi sana za biashara. Nimefanya biashara ya maduka ya nguo,maduka ya chakula, Biashara ya bar na hata biashara ya jiko la chipsi n.k.utoaji wa huduma mbalimbali,maduka ya spea za magari,pikipiki hata nimefanya biashara katika sekta ya elimu na hata udalali wa nyumba na mashamba.
Najua unaweza kushangaa inakuwaje nimefanya biashara za aina nyingi hivi?Well katika maisha kuna hatua na katika kila hatua unajikuta unakumbana na hustles ambazo zinakufanya uingie katika aina fulani ya biashara kwa muda mfupi au muda mrefu. Najua siko mwenyewe ambaye ninafanya biashara za aina tofauti ila najua kuna watu ambao kabisa hawajawahi hata kujaribu kufanya biashara. Swali la kujiliza ni JE nikitu gani kinakufanya na wewe usianzisha kabiashara kako hata kama ni kadogo?Je ni Mtaji?Je ni wazo la biashara huna?Je ni muda?Je ni uwezo wako wa kiakili ni mdogo?Je ni fursa hauzioni?Ni kitu gani kinakuzuia kufanya biashara?
Kila mtu anazo sababu zinazomfanya asianzisha biashara.Ila leo nataka nikwambie ni kwa nini ni muhimu uanzisha kabiashara kako.Hata kama ni kadogo.Siku hizi kuanzisha biashara ni rahisi sana.Kuendesha na kusimamia biashara ni rahisi sana.Unapokaa bila kuwa na Biashara unapishana na FURSA ambazo utakuja kuzikumbuka.
Jaribu kufikiri kampuni kama za FACEBOOK(META),GOOGLE(ALPHABET),TWITTER,TIKTOK na kampuni nyingine kama hizo halafu ujiulize iwapo zina tofauti yeyote.Hizi zote ni kampuni za TEHAMA ambazo kiuhalisia zinadeal na Taarifa tu.Ni kampuni ambazo ni kubwa sana na zinaingiza mabilioni ya PESA.Swali ni JE unafikiri uanzishwaje wake ulikuwa mgumu au mrahisi?
Ukizitazama hizi kampuni unaweza kufikiri kuzianzisha ilikuwa kazi ngumi il ilikuwa kazi rahisi sana.Ilifanywa na mtu mmoja au wawili ambao waliamini katika wazo lao na kutenga muda na rasilimali zao kulipa wazo lao nguvu.Baada ya hapo sote tunajua kilichotokea.
Biashara yoyote inaanza na wazo na kuliamini wazo lako.Mawazo ya biashara yako mengi na yote yanaweza kukuingizia kipato tena cha kutosha kabisa. Swali la kujiuliza ni Je unaliamini wazo lako?Hapo ndipo ambapo wengi wetu hukwama. Kwani sisi wenyewe tunakuwa hatuamini katika wazo na uwezo wetu na matokeo yake ni kwamba tunapokutana na changamoto yoyote ni rahisi kufikiri kwamba tumefikia Mwisho kumbe bado ni mwanzo tu.
Wazo lolote la biashara ni lazima ulifanyie "Validation" Hii unaweza kufanya kwa kuangalia wengine wanafanya nini katika eneo hilo au unaweza kulipeleka sokoni kwa baadhu ya wateja ili uone iwapo litawafaa na unaweza.Kumbuka usipolifanyia wazo lako validation ni vigumu sana wewe kuelewa kwa kina aina ya biashara na changamoto zake.
Katika mjadala huu nimechokoza kidogo tu kuhusu kile kinachotuzuia kuanzisha biashara na namna ambavyo tunaweza kuvuka changamoto.Hata hivyo naamini kwamba yako mengi ambayo yanawazuia watu wasianzishe biashara. Karibuni tujadili kwa pamoja Juu ya yale ambayo yanatuzuia kuanzisha biashara na namna ambavyo tunaweza kuyashinda na kuibua mawazo na fursa mpya.
Karibuni