Nini kinakwamisha Simba na Yanga kushirikiana kimataifa?

Nini kinakwamisha Simba na Yanga kushirikiana kimataifa?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Moja ya mambo yanayokwamisha sana mpira wetu ni ushindani na uhasama wa Simba na Yanga unaopelekea vilabu hivi siyo tu kushindwa kushirikiana katika mashindano ya kimataifa bali wakati mwingine hadi kuhujumiana na kufanyiana fitna.

Juzi juzi nilipokuwa naangalia tuzo za CAF niliona jinsi wenzetu wanavyojivunia sana mchezaji au timu yao iwe klabu au ya taifa inapofanikiwa na kupewa matuzo. Pamoja na kwamba nchi nyingi zina timu zenye upinzani wa jadi, sina uhakika kama huwa wanadhihakiana pale mmoja anapofanikiwa katika jambo lake.

Najua katika uhalisia wa utani wa jadi wengine wanasema ni tunu ya taifa inayoendelea kuimarisha umoja wetu, wengine wanasema inasaidia kunogesha mpira na maisha yetu. Inawezekana yote haya yana ukweli fulani.

Binafsi naona bila ushirikiano fulani wa kimkakati kati ya vilabu hivi itakuwa ngumu sana moja ya vilabu hivi kutoboa kimataifa maana unaweza sogea kidogo halafu mwenzio atakukwamisha tu, halafu unamuona yuleee pale jukwaani anashangilia anguko lako. Huu uhasama na utani wa jadi unacheza katika mstari mwembamba wa chuki na wivu kwa upande mmoja na utani kwa upande mwingine.

Unadhani nini kifanyike kutengeneza mkakati wa kushirikiana au kama hauwezi kumsaidia mwenzio basi angalau usimuwekee vigingi katika njia yake?
 
Moja ya mambo yanayokwamisha sana mpira wetu ni ushindani na uhasama wa Simba na Yanga unaopelekea vilabu hivi siyo tu kushindwa kushirikiana katika mashindano ya kimataifa bali wakati mwingine hadi kuhujumiana na kufanyiana fitna.

Juzi juzi nilipokuwa naangalia tuzo za CAF niliona jinsi wenzetu wanavyojivunia sana mchezaji au timu yao iwe klabu au ya taifa inapofanikiwa na kupewa matuzo. Pamoja na kwamba nchi nyingi zina timu zenye upinzani wa jadi, sina uhakika kama huwa wanadhihakiana pale mmoja anapofanikiwa katika jambo lake.

Najua katika uhalisia wa utani wa jadi wengine wanasema ni tunu ya taifa inayoendelea kuimarisha umoja wetu, wengine wanasema inasaidia kunogesha mpira na maisha yetu.

Binafsi naona bila ushirikiano fulani wa kimkakati kati ya vilabu hivi itakuwa ngumu sana moja ya vilabu hivi kutoboa kimataifa maana unaweza sogea kidogo halafu mwenzio atakukwamisha tu, halafu unamuona yuleee pale jukwaani anashangilia anguko lako. Huu uhasama na utani wa jadi unacheza katika mstari mwembamba wa chuki na wivu kwa upande mmoja na utani kwa upande mwingine.

Unadhani nini kifanyike kutengeneza mkakati wa kushirikiana au kama hauwezi kumsaidia mwenzio basi angalau usimuwekee vigingi katika njia yake?
Mbona wanashiriki tena vyema kimataifa,timu2 hadi sasa,upewenini tena,tena zenye matumaini lukuki🏃
 
Hao unaoita wenzenu ulijuaje ni timu tofauti?
Daah, swali zuri ila gumu saana 🤔

Ila kwa kutambua kuwa suala hili bado linahitaji utafiti zaidi, kuna sehemu hapo nimeandika "sina uhakika kama huwa wanadhihakiana pale mmoja anapofanikiwa katika jambo lake"
 
Mkuu huko Misri derby yao ni nzito kuliko hata Simba na Yanga.
 
Ni KUSHIRIKIANA sio kushiriki. Ukweli mchungu asilimia kubwa ya washabiki WA mpira ni watu wasio na uelewa mpana. Mfano timu ambayo haijaiwahi kufika robo fainali kuicheka timu inayoishia robo. Wengi wanatumia NGUVU ya kujenga hoja Kwa ubishi na ujuaji. Pia Viongozi kama Manara hawafai hebu fikiri Hadi kufikia kuhost timu pinzani kutoka nje, kuvaa jezi zao na kuwashangilia. Timu hizi zimeanzishwa miongo kibao hatajawahi kushuhudia chuki kiasi hiki. Utani unaruhusiwa hata WA mabango ni utani lakini sio kupokea wageni na kuwapa mbinu ya kufunga Taifa lako.
 
Hiyo ipo kote duniani
Mashabiki wa man u hawawezi ku support Liverpool
Barcelona hawezi support Madrid
Arsenal hawezi ku support spurs
Galatasaray hawezi support fehnabache
 
Daah, swali zuri ila gumu saana [emoji848]

Ila kwa kutambua kuwa suala hili bado linahitaji utafiti zaidi, kuna sehemu hapo nimeandika "sina uhakika kama huwa wanadhihakiana pale mmoja anapofanikiwa katika jambo lake"
Ukweli ni kwamba wenzetu mataifa mengine, linapokuja suala LA utaifa, uhasama na upinzani wanauweka kando, wanaungana kuwa kitu ki1.
 
Moja ya mambo yanayokwamisha sana mpira wetu ni ushindani na uhasama wa Simba na Yanga unaopelekea vilabu hivi siyo tu kushindwa kushirikiana katika mashindano ya kimataifa bali wakati mwingine hadi kuhujumiana na kufanyiana fitna.

Juzi juzi nilipokuwa naangalia tuzo za CAF niliona jinsi wenzetu wanavyojivunia sana mchezaji au timu yao iwe klabu au ya taifa inapofanikiwa na kupewa matuzo. Pamoja na kwamba nchi nyingi zina timu zenye upinzani wa jadi, sina uhakika kama huwa wanadhihakiana pale mmoja anapofanikiwa katika jambo lake.

Najua katika uhalisia wa utani wa jadi wengine wanasema ni tunu ya taifa inayoendelea kuimarisha umoja wetu, wengine wanasema inasaidia kunogesha mpira na maisha yetu. Inawezekana yote haya yana ukweli fulani.

Binafsi naona bila ushirikiano fulani wa kimkakati kati ya vilabu hivi itakuwa ngumu sana moja ya vilabu hivi kutoboa kimataifa maana unaweza sogea kidogo halafu mwenzio atakukwamisha tu, halafu unamuona yuleee pale jukwaani anashangilia anguko lako. Huu uhasama na utani wa jadi unacheza katika mstari mwembamba wa chuki na wivu kwa upande mmoja na utani kwa upande mwingine.

Unadhani nini kifanyike kutengeneza mkakati wa kushirikiana au kama hauwezi kumsaidia mwenzio basi angalau usimuwekee vigingi katika njia yake?
Tubaki hivi hivi tunaanzaje kuweka ushirikiano na wachawi wanaoturogea wachezaji wetu.
 
Ali kamwe alisema Uzalendo ni taifa stars tu kungine hakuna hyooooo
 
Moja ya mambo yanayokwamisha sana mpira wetu ni ushindani na uhasama wa Simba na Yanga unaopelekea vilabu hivi siyo tu kushindwa kushirikiana katika mashindano ya kimataifa bali wakati mwingine hadi kuhujumiana na kufanyiana fitna.

Juzi juzi nilipokuwa naangalia tuzo za CAF niliona jinsi wenzetu wanavyojivunia sana mchezaji au timu yao iwe klabu au ya taifa inapofanikiwa na kupewa matuzo. Pamoja na kwamba nchi nyingi zina timu zenye upinzani wa jadi, sina uhakika kama huwa wanadhihakiana pale mmoja anapofanikiwa katika jambo lake.

Najua katika uhalisia wa utani wa jadi wengine wanasema ni tunu ya taifa inayoendelea kuimarisha umoja wetu, wengine wanasema inasaidia kunogesha mpira na maisha yetu. Inawezekana yote haya yana ukweli fulani.

Binafsi naona bila ushirikiano fulani wa kimkakati kati ya vilabu hivi itakuwa ngumu sana moja ya vilabu hivi kutoboa kimataifa maana unaweza sogea kidogo halafu mwenzio atakukwamisha tu, halafu unamuona yuleee pale jukwaani anashangilia anguko lako. Huu uhasama na utani wa jadi unacheza katika mstari mwembamba wa chuki na wivu kwa upande mmoja na utani kwa upande mwingine.

Unadhani nini kifanyike kutengeneza mkakati wa kushirikiana au kama hauwezi kumsaidia mwenzio basi angalau usimuwekee vigingi katika njia yake?
Kwasababu yanga wanaenda kuwapokea wageni airport yaani vita yetu na yanga haiwezi kwisha kwa ujinga ule mliorufanyia.
 
Simba iliwahi kuwapa ushirikiano Yanga mwaka 1998 kwa kuwaazimisha (baada ya Yanga kuomba) wachezaji kadhaa, pamoja na Simba kukejeliwa na hao watani zake mwaka 1993.

Kwa jinsi Yanga walivyo na roho mbaya sidhani kama wao wangekuwa tayari kuwaazimisha Simba wachezaji.
 
Back
Top Bottom