Nini maana ya coolant na inter cooler kwenye gari?

mtu kauliza maana ya coolant na intercooler kwenye gar. peoples wamekuja na maneno million

ilikuwa inatosha kusema, coolant ni kimiminika ambacho heating rate yako inachelewa tofauti na maji ya kawaida.
intercooler- internal cooling system. then maswali yaanzie hapo.
 
Ni kweli na uendelee kushangaa lakini nimepata elimu na nimeelimishwa so nilichokuwa Naitaji nimeipata na nashukuru kwa wale wenye positive mind kwa ushirikiano walionipa nami mtaweza kuwaelewesha wenzangu wenye shida kama nliyokuwa nayo mimi
 
Huwa wanafundisha ndiyo na aina za gari ata kama hautaendesha au miliki..mifumo mingi ya gari inafanana..ukiachana na hzo tofauti chache za kwamba hii ina turbo hii haina ..hii ina 4wheels hii ina AWD...sasa nmeshangaa ata coolant huijui..
Lakini haya mambo ya kujifanya mjuaji wa kila kitu na kuwaonawanaouliza wasivyovijua ni wajinga si utamaduni mzuri je unautoaje ujinga wangu kwa kunikejeli bila kunielimisha
 
Lakini haya mambo ya kujifanya mjuaji wa kila kitu na kuwaonawanaouliza wasivyovijua ni wajinga si utamaduni mzuri je unautoaje ujinga wangu kwa kunikejeli bila kunielimisha
Mkuu nmekukejeli wapi..? Mbona nmekuiliza tu kistaarabu..nilidhani nmekupa mwanga wa kuona umuhimu wa kwenda darasani..samahani lakini kama nmekukwaza.
 
Sawa mkuu naomba kujua aina za ivyo vimiminiko ambavyo havipati joto kwa haraka?
 
Mjumbe nakushukuru kwa maelezo mazuri, japo ningependa kumwongezea kitu kuhusu Coolant.

1. Coolant siyo maji ya kawaida kwenye gari kama watu wengi wadhaniavyo, ni mchanganyiko wa maji fulani "deionized water" ambayo uchanganywa na aither Ethylene Graycol au wakati mwingine Glycerine na mchanganyo unatakiwa uwe 50/50. Unashauriwa usizidishe kipimo walau cha 30/70 kama umeshindwa kabisa.

-Baada yakuchanganya unaweza kutumia reflectometer kupima kama umepata mchanganyiko sawa.

2. Coolant huwa ina kitu kinaitwa freezing and boiling point, na hapa ndipo tofauti ya coolant na maji ya bomba utofautiana. Kawaida maji uchemka pale yanapopata joto la 100 degree na uganda yakifika 0, sasa coolant imeongezewa additives ambazo uipa uwezo wakuweza kuhimili joto la mpaka zaidi ya degree 100 hivyo uweza kuilinda injini isichemke, pia kwenye mazingira ya baridi coolant imepewa uwezo wa kwenda hafi kwenye negative degree na bado isigande, tofauti na maji ya kawaida ambapo yangekuwa yashaganda.

Kazi yake nini?

Kazi ya Coolant nikusafirisha joto ambalo utokana na mzunguko kwenye injini kuelekea kwenye rejeta, likishapozwa urudishwa kwenye injini kwa ajiri ya kuipoza.

Kwanini usitumie maji ya bomba?
Maji ya bomba yakipata moto yanachemka kama yakupikia ugali, yakipoa uzaa mvuke ambao ukichanganyika na hewa+chuma, baada ya muda kutu huanza kujenga ndani ya rejeta, matokeo yake njia zote uliwa na kutu, rejeta itaziba na itaanza kutoboka na kumwaga maji. Pia gari itakuwa inachemsha sana.

Kwa ufupi ukitumia coolant unazua mambo yafuatayo: freezing, boil-over, cavitation, liner pitting, erosion, corrosion, elastomer gasket degradation, na scaling.(nimekosa kiswahili but unaweza kuuagoogle moja moja).

Pitia kiambatanisho hiki kwa msaada.
 

Attachments

Kaka namm naomba kujua macopolo maana yake ninn maana nimeona scania nyingi san zimeandikwa makopolo
 
Shukrana kaka mungu akuzidishie maarifa,nilipokua naona macopolo nikawa nahis labda kuna kitu kimezidishwa kaka
 
Boss maji ya bomba haishauriwi kabisa. Kama unatumia pia, tafuta raduator flush uflush then uweke premix coolant utakuwa safe, siyo ghari na kama gari lako halivuji itakupeleka mpaka usahau.
 
Huwa wanafundisha ndiyo na aina za gari ata kama hautaendesha au miliki..mifumo mingi ya gari inafanana..ukiachana na hzo tofauti chache za kwamba hii ina turbo hii haina ..hii ina 4wheels hii ina AWD...sasa nmeshangaa ata coolant huijui..

Huyu muuliza swali hakwenda darasani kabisa, anaulIza anajibiwa na bado anauliza same questions.
 
Huyu muuliza swali hakwenda darasani kabisa, anaulIza anajibiwa na bado anauliza same questions.
Mkuu nashukuru na ww kuliona..mm nililiona hilo baada tu ya kusoma kichwa cha uzi..bt ndo hvyo anasema mm nmemuattack...
 
Nichumu Nibebike AC sio kwa ajil ya kupooza maana wengi wakisikia ac wanajua ni kuleta hali ya ubarid tu kwa ndan NO AC ni kwa ajili ya hali ya hewa kama unataka joto utalipata kama baridi utapata hiyo ndo maana ya air condition


Intercooler .....fins flani hivi zipo kwa ajili ya kupooza hewa inayotoka kwenye turbo baada ya turbo kuwa imevuta hewa nje .....kwa vile turbo inaendeshwa na exhaust gas ambayo ni ya moto hivo na yenyew itapata moto kusababisha hata hewa ambayo itapita pale na yenyew kupata moto hivo kusababisha hewa kupoteza zile molecules ...hewa bard ina molecules nying kuliko ya moto kwa ujazo mmoja


inshort intercooler ipo kama radiator ila hewa inapita mule ndan na kupoozwa kabla ya kuingia kwa engine
 
AC sio kwa ajil ya kupooza maana wengi wakisikia ac wanajua ni kuleta hali ya ubarid tu kwa ndan NO AC ni kwa ajili ya hali ya hewa kama unataka joto utalipata kama baridi utapata hiyo ndo maana ya air condition
Safi ila hiyo unayozungumzia wewe siku hizi inaitwa HVAC yani heat, ventilation and AC...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…