Nini Maana ya Hisa.

Nini Maana ya Hisa.

Kontelo

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2013
Posts
572
Reaction score
161
Habari zenu wanajamvi.

Nimefanikiwa kusoma au kuendelea kuiona au kusikia hii kitu inayoitwa Hisa. Na mara nyingi ninasikia hasa kwenye shughuli za kibenki na biashara zingine kubwa kubwa.

Naomba msaada wa kupata elimu kuhusu Hisa ili nipate uelewa na nifaham nawezaje kuwa mdau ktk shughuli za Hisa zinavyoendelea hivi sasa.

Nawasilisha
 
Hisa ama jina jingine share ni kipande chenye thamani fulani...kama hela ilivyo kuna shs.10.20.50 na kadhalika....sio kila company inaweza ku issue share lazima iwe ime listiwa katika stock exchange husika...kwa mfano hapa Tz tuna DSE(DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE).Nchi nyingne zilizoendelea kama Marekani zina stock exchange zaid ya 500 kama NSE .

KWA TANZANIA kampuni baadh nazojua zinazo issue share ni kama CRDB .PRECION AIR..NMB TCC.KCB..ETC...Wanaopata faida kwenye hizi hisa ni watu walio invest mihela kibao.sio ununue share za laki moja utegemee utapga bingo...kila kampuni huwa inatangaza kila baada ya mwaka faida au hasara iliyopata hivyo huwa wana announce dividend shareholders watakakazopewa...kama una hisa chache co ajabu uambuliye 10000 kwa mwaka mzima.
 
Mdau Nimechafukwa, maelezo yako yana kasoro. Kila kamapuni iliyosajiliwa rasmi (hata kama ni ya kuuza vitunguu reja reja) inakuwa na hisa. Isipokuwa kuna aina mbili za kampuni. Kuna kampuni binafisi (private company) na kampuni ya umma (public company). Kampuni binafsi ni zile ambazo hazikuorodheshwa kwenye soko lolote la hisa.

Kisheria (kwa Sheria ya Makampuni ya Tanzania) hizi zanatakiwa ziwe na wamiliki (wanahisa) kati ya wawili (2) mpaka hamsini (50). Kampuni ya umma, kwa upande mwingine, lazima iwe imeorodhesha hisa zake katika soko la hisa. Kwa hapa Tanzania tunalo soko moja (Dar es Salaam Stock Exchange - DSE). Kampuni ya umma haina kikomo cha wamiliki (wanahisa) bali kuna masharti mengi yanayoongoza uendeshwaji wake kuliko kampuni binafsi. Hata wewe ukitaka kuanzisha kampuni ya kuuza maandazi unaweza.

Mtafute mtaalamu akutengenezee hati inayoitwa "Memorandum and Articles of Association" halafu uipeleke BRELA (Business Registration and Licensing Agency). Baada ya kutimiza masharti fulani fulani na kulipa ada ya usajili utakuwa na kampuni ambayo wewe na watu wa familia yako au washirika wako mtakuwa ndiyo wenye hisa. Haya ni maelezo ya jumla. Ni somo pana mno kulieleza kinagaubaga hapa.
 
hisa ama jina jingne share ni kipande chenye dhamani fulan...kama hela ilivyo kuna shs.10.20.50 na kadhalika....sio kila company inaweza ku issue share lazima iwe ime listiwa katika stck exchange husika...kwa mfano hapa Tz tuna DSE(DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE)..nchi nyingne zlizoendelea kama marekan zna stock exchange zaid ya 500 kama NSE ..KWA TANZANIA kampuni baadh nazojua znazoissue share ni kama CRDB .PRECION AIR..NMB TCC.KCB..ETC...Wanaopata faida kwenye hiz hisa ni watu walio invest mihela kibao..co ununue share za laki moja utegemee utapga bingo...kila kampuni huwa inatangaza kla baada ya mwaka faida au hasara iliyopata hivyo huwa wana announce dividend shareholders watakakazopewa...kama una hisa chache co ajabu uambuliye 10000 kwa mwaka mzima....

Mkuu asante sana kwa ufafanuzi...
 
Mdau Nimechafukwa, maelezo yako yana kasoro. Kila kamapuni iliyosajiliwa rasmi (hata kama ni ya kuuza vitunguu reja reja) inakuwa na hisa. Isipokuwa kuna haina mbili za kampuni. Kuna kampuni binafisi (private company) na kampuni ya umma (public company). Kampuni binafsi ni zile ambazo hazikuorodheshwa kwenye soko lolote la hisa. Kisheria (kwa Sheria ya Makampuni ya Tanzania) hizi zanatakiwa ziwe na wamiliki (wanahisa) kati ya wawili (2) mpaka hamsini (50). Kampuni ya umma, kwa upande mwingine, lazima iwe imeorodhesha hisa zake katika soko la hisa. Kwa hapa Tanzania tunalo soko moja (Dar es Salaam Stock Exchange - DSE). Kampuni ya umma haina kikomo cha wamiliki (wanahisa) bali kuna masharti mengi yanayoongoza uendeshwaji wake kuliko kampuni binafsi. Hata wewe ukitaka kuanzisha kampuni ya kuuza maandazi unaweza. Mtafute mtaalamu akutengenezee hati inayoitwa "Memorandum and Articles of Association" halafu uipeleke BRELA (Business Registration and Licensing Agency). Baada ya kutimiza masharti fulani fulani na kulipa ada ya usajili utakuwa na kampuni ambayo wewe na watu wa familia yako au washirika wako mtakuwa ndiyo wenye hisa. Haya ni maelezo ya jumla. Ni somo pana mno kulieleza kinagaubaga hapa.

namm nimechafukwa na maelezo hapo uliposema haina, sio haina ni aina
 
Kwa maana rahisi hisa ni mgawanyo wa thamani ya kampuni.kwa makampuni ya uma,thamani ya kampuni hugawanywa kwenye vipande vidogo(hisa)ambavyo huuzwa kwenye stock exchange.wamiliki ama wanunuzi wa hisa huhesabiwa kama sehemu ya kampuni husika na hupata gawio mwisho wa mwaka(dividend)kutokana na faida ya kampuni husika.(japo sio makampuni yote hulipa gawio).wamiliki wa hisa huitwa wanahisa(shareholders)

Kwa upande wa makampuni binafsi ambayo kisheria yanaruhusiwa kuwa na watu kuanzia wawili hadi hamsini,hawayauzi hisa zao kwenye soko la hisa..wanachofanya hugawana hisa kutokana na jinsi kila mmoja anavyochangia mtaji kwenye kampuni....hawa wanaweza wakawa mtu na mkewe wakaanzisha kampuni na kuamua kuwa na 50% ya hisa kila mmoja.
 
Mkuu Kontelo tembelea na tovuti ya jamaa wa dhamana ya uwekezaji unaweza ukajifunza kitu fulani. Angalia hii link hapa Utt home page
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom