Nini maana ya ‘Kilimo cha PDF’?

Wazee wa PDF husema hivii...

Shamba Eka 1 unaotesha miche 1000 ya Mitikiti maji. Baada ya miezi 5 unaanza kuvuna kila mche mmoja matikiti 4 utakayouza kila 1 @ 1000 bei ya shambani. Hapo utauza matikiti 4000 mara 1000 utapata shilingi 4,000,000 kila mchumo mmoja.

Sasa lima ekari 10 ambapo utapata milioni 40 kila ukivuna mchumo mmoja.

Mwisho wa PDF wanakuambia, kilimo kina hela, kilimo ni fursa
 
Kwani uongo kilimo kina lipa
Mimi hapa nalima nyanya naweza kulipa mwanajeshi 3 mshahara
 
Jichanganye sasa ulime uone balaa lake 😂
 
Na Kuna watu wao na PDF hakuna utofauti, utamkuta anakupa details as if yeye ndio mhusika wa kilimo fulani.

Mara ooh zabibu pale Dodoma zinalipa sana.
Hua najiuliza kwan wao hawataki hzo hela.
 
Na Kuna watu wao na PDF hakuna utofauti, utamkuta anakupa details as if yeye ndio mhusika wa kilimo fulani.

Mara ooh zabibu pale Dodoma zinalipa sana.
Hua najiuliza kwan wao hawataki hzo hela.
Wangekuwa wanasema
Changamoto ya zao husika
Uzoefu wao wakulima hilo zao
Na ushahidi waku justify wao nao wamepima zao hilo labda hapo tusingekuwa na kilimo cha pdf
 
😄 🤣 🤣🤣🤣. Ila kilimo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…