Nini maana ya KUDADEKI? Sio tusi?

Njilembera

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2008
Posts
1,496
Reaction score
609
Wana JF, Mimi Nina asili ya Bara, na maneno yanayotamkwa Kwa mkazo na hasa yenye kuanzia herufi 'ku' zinanipa hisia kuwa ni aina Fulani ya kutukana.

kwenye matangazo ya biashara ya Tigo Facebook, ninapata shida sana ninapomsikia Yule Mzee akadakia neno 'kudadeki', linaonekana ni neno baya, tusi walau Kwa matamshi. Hisia hizi zimeimarika zaidi pale ninapohusisha maneno ya utangulizi wa Yule Babu, kwamba uzee mwisho ni Msata, mijini ni ' honey' ambayo yanamaanisha uhusiano wa watu wazi a na jinsi a nyingine.


Ningefurahi kuondolewa wasiwasi huu! Je lakini, hakuna laughs nyingine ambayo ingefikisha Ujumbe huo huo?
 


Hapo RED, itakuwa kwako kila kitu ni tusi aisee; kula, kulala, kuimba, kusoma, kucheza, kuruka, kulima, kuomba, kusali, kutazama, kutembea, kunywa, kuandika etc etc.

Hebu angalia tena ulikuwa unamaanisha nini, otherwise umekurupuka.
 
kuna ka ukweli lakini,jamaa amesema "ku" inayotiliwa mkazo,hata lile lingine "ku--mbegesi" na lenyewe ku yake inatiliwa mkazo
 
neno la kihuni mbadala wa neno lingine la kihuni ku...mbegesi. halina heshma yeyote ingawa ni misisitizo ya kihuni
 
kudadadek ni maneno yasiyo na maana mfano wake ni afanalek shabbash ni mfano ha gash(kiingereza) hayana maana ila hupata maana kihsi pind mtu anapotamka akiwa katika hali gani kuelezea hisia zake kuwa amefikia kiwango cha mwisho mfano umemuudhi au ameona kitu kilicho mvutia eg kito dem mkali au gari nyumba nk ingawa mda mwingne hutumika kama vionjo
 

Nakubaliana nawe kwa asilimia zaidi ya themanini.
 
Hakika mkuu Skype kwanza nikupongeze kwa ujasiri wa kutamka hayo maneno....na nibakie tu kuona muendelezo wa mada jadiliwa.

Nikushukuru pia napenda kusisitiza kuwa hapa tupo ktk kujifunza zaidi mkuu wangu si kama kule kwenye ulingo wa siasa, la hasha. Na endapo utatamka maneno hayo kwa kumlenga mtu kwa hakika kutakua na kisa ama mkasa wala si bure.
 
Last edited by a moderator:
mcubic naomba nikuongezee maneno haya na wataalam watachangia zaidi kua ni kwa nini yanatumika kama ifuatavyo:

1. Yule pundamilia ni mzuri kishenzi.

2. Mcubic ni mshenzi wa lugha.

3. Yule demu ni mkali kinyama.

4. Jamaa yuko nondo!

Ukiangalia hapo juu kuna maneno kama mshenzi, kishenzi, mkali, kinyama na nondo yametumika kumaanisha dhana tofauti kabisa na maana za msingi za maneno hayo.
 
Last edited by a moderator:
Ukweli ni kwamba haya maneno ni matus mfano;kumamake,kudadadeki.Kama utakuwa na ulewa fulani utaweza kupata kirefu cha neno "kumamake'',chukua japo dakika 3 ufikirie utapata jibu.
 
Ukweli ni kwamba haya maneno ni matus mfano;kumamake,kudadadeki.Kama utakuwa na ulewa fulani utaweza kupata kirefu cha neno "kumamake'',chukua japo dakika 3 ufikirie utapata jibu.

JITABOY mambo vipi mkuu? Unaizungumziaje na hii kauli hapa chini?:

Masalakulangwa ni mshenzi wa Hesabu kinyama.
 
Last edited by a moderator:
JITABOY mambo vipi mkuu? Unaizungumziaje na hii kauli hapa chini?:

Masalakulangwa ni mshenzi wa Hesabu kinyama.

neno mshenzi tayari lina maana tofaut na kudadeki ambalo naweza sema ni neno la kufikirika.
mfano wa maneno yenye maana kama huyu kijana ni nyoko usimchezee katika mambo flani maneno tayari yana maana ila watumiaji wa lugha huweza kuyatumia maneno hayo na wakelewana vile wanavyotaka wao waelewane ila huo sio usahihi wake.
ndio maana lugha hz kuepusha mgongano wa kimaana huzungumzwa tu. kwa rika au kundi la watu fulani ambao wamekubali kuelewana.
siku hizi, mtu anatukanwa ndo anasifiwa wazungumzaji hupendezewa na mdundo wa sauti (tone of the voice) na mambo yakaenda
 
Last edited by a moderator:

Mkuu nadhani nimekuelewa sasa.
 
kulalae, kubabae, kulaleki, kubababeki, kudadake, kudadadeki mi nadhani ni kama damn! kwa kizungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…