Nini maana ya kusamehe...?

... Hii afya inaitwa afya ya Utu!! ..Lol! tofauti na ile ya mwili.... Ni afya muhimu !
Hii ni ya utu, akili na mwili...lol
Ntarudi nikawsome kama mli conclude UTU ni nini!
 
Kwahiyo hata kama ni mwizi unajifanya kama vile sio mwizi kisa umemsamehe???

Aiwezekani kwako kumsamehe mwizi hata kama ujui kama atendelea na tabia hiyo? Kusamehe akugarantee mtu kuacha tabia yake!
 

Ni kweli hasira, vinyongo na visasi vinadororesha afya aisee...

Lakini bado na sisitiza 'kusamehe ni mchakato'...angalau kwa baadhi ya watu na kukingana na kosa na mahusiano ya wahusika
 
Hata urafiki ni mahusiano...na naongelea mahusiano ya aina yote...kimapenzi..kirafiki..kindugu n.k
Swali...kumsamehe mtu kunahusiana vipi na utayari wako kurudia mahusiano yenu ya mwanzo???

Kusamehe kwenye mahusiano ya kawaida hakuna mambo mengi,suala ni moja tu kusamehe.Kwenye mahusiano ya kimapenzi ni tofauti.Kwenye mahusiano ya kimapenzi kusamehe na kurudisha uhusiano ni vitu viwili tofauti.Unaweza ukamsamehe na mkaendelea kupiga stori lakin msiwe wapenzi tena.Mtu anaweza kuonesha nia ya kutaka asamehewe lakini akawa hajaonesha kutaka kuwa mapenzini tena!
 
Tatizo watu wanapoambiwa kusamehe ni dawa hawaelewi!Fahamuni kuwa unapoacha kumsamehe unakuwa na hasira pamoja na kinyongo.Hizi ni hisia hasi zina madhara ya kihisia na kimwili,hasira husababisha kifua kubana na kusababisha damu isipite kwenye mishipa inavyotakikana.Kinyongo humfanya mtu kutojisikia vyema na kuwa na kisirani muda mwingi.
 
Ni kweli hasira, vinyongo na visasi vinadororesha afya aisee...

Lakini bado na sisitiza 'kusamehe ni mchakato'...angalau kwa baadhi ya watu na kukingana na kosa na mahusiano ya wahusika

Kusamehe ni mchakato... binafsi naafiki ..! Kwani kweli kuna matukio mengine..Lohh ..huwezi kuamka asubuhi na kujikuta umeweza ku late go for good! Lakini pia kuna baadhi ya victims ...hawaoni sababu ya msingi ya kusamehe ..au wanalifanya ni jambo jepesi lisilo na umuhimu sana!

..Hapo ndio mtu kama huyo anapoelimishwa kwa dhati kuwa kutosamehi kunaharibu kinga ya mwili wakati mwingine kuliko hata vimelea vya maradhi.. hapo anaweza ..tikisa...kichwa na kuuliza mara ya pili ..what did you say? maana anaanza kumaka!!
 

Lizzy mpenz sijui kwa nini nimeijenga imani juu ya Msamaha wa kusahau na kurudi kama mwanzo! Huwezinambia nimekusamehe halafu haturudiani kuwa pamoja!!! Kwangu ni umekubali YAISHE kuwa huna kinyongo na mimi lakini unayakumbuka niliyokukosea
 

The Boss hii nimeipenda ingawa ningeomba unifafanulie zaidi kwani katika hii post yako tuko ukurasa mmoja BUT kulet it go unakokuzungumzia wewe na mimi ni tofauti! Nahisi kuwa wewe unazungumzia kulet it go but usirudie uhusiano mlokuwa nao mwanzo ambayo kwangu mimi bado huja-let it go but umehold it freely!
 
Hii kitu ni subjective sana, inategemea natukio, kuna wakosaji wanalazimisha wasamehewe kwa nguvu bila utayari wa mtendwa.
Kama ndugu na rafiki obvious ukimsamehe along the road kila kitu kitarudi kama mwanzo.
Kwenye mahusiano inategemea na kosa pis impact ya kusamehe au kutokusamehe.

Jibu siyo moja hapa kwa kweli
 

umeona ee? afadhali umenisoma mstari kwa mstari...

... Ni kutokuwa na hata tone moja la hisia hasi za chuki, hasira, kinyongo, shaka nk kwa muhusika!!

...dahhhh, mimi bado sijafikia kupunguza hayo....



jamani, mwenzenu kidonda changu bado kibichi...
nipeni muda basi...labda nitaweza sahau na kumsamehe!



bht, ....nayazingatia maneno yako,....
hebu nisaidie nduguyo hizo process za kusamehe nami
nijiskie 'comfortable' aisee....dahhh, hapana...acha kwanza!


nafikiri point yangu ni sio 'kutegemea the worst'
bali kutokuwa 'suprised' yakitokea

...aiseee? unaweza tabiri heartbreak itavyokuumiza? umejaliwa 'roho ngumu' bro!


Umenikumbusha ile unasema "Ahaaa fulani bana namuamini sana hawezi kunifanyia jambo lolote baya"

...dahhhh,
hivi hukuweza vumilia mpaka umenikumbushia machungu?
haya ndio maneno nilokuwa nabishania na ndugu zangu, akiwemo mama yangu kabla sijatendwa.



...mwj1, ndio kusema kwako wewe kuna nafasi kubwa ya 'baby come back' sababu msamaha wako hauna masharti, au nimekusoma vibaya?
 


Mie kwa maoni yangu kama mko kwenye mapenzi na mwenzio akakukosea na kosa lake lilimfanya yule aliyekosewa awe tayari kuvunja uhusiano wa kimapenzi kati yao basi anapokuomba samahani na kuomba muendelee na penzi lenu inapendeza zaidi kama utamtamkia kwamba umemsamehe na kumpa nafasi nyingine ya kuendelea na penzi lenu. Sioni kama ni sawa kumtakia mkosaji kwamba nimekusamehe kosa lako na wakati huo huo unashikilia uamuzi wako wa kwamba penzi lenu limefikia tamati, kusema kweli mkosaji katka hali kama hii haamini kabisa kwamba samahani yake ilipokolewa na hivyo ataendelea kuwa na donge lake kwa muda mrefu ujao na huku akiamini kabisa kwamba samahani aliyoiomba haikukubaliwa.

 
Last edited by a moderator:


...mwj1, ndio kusema kwako wewe kuna nafasi kubwa ya 'baby come back' sababu msamaha wako hauna masharti, au nimekusoma vibaya?

....Mbu kama sijakwambia YAMEKWISHA, you are still in my heart baby.
 
Reactions: Mbu
Kusamehe inamaanisha kutokumbuka ya nyuma.
Loading...
Little X aksante- kutokumbuka ya nyuma.... Je unapokatisha mahusiano baada ya kusamehe ni kweli kuwa hutoyakumbuka yakotokezea hadi ukakatisha mapenzi yenu?
 
Hapo umesema kitu muhimu sana.
Kusamehe ni kukubali 'kujaribu' kumuachilia mtu kwa kosa alilotenda. Unaweza kumuachilia wakati akiwepo/uhusiano ukiendelea ama mkiwa hampo pamoja.kusamehe ni process ndefu na ngumu kutegemeana na kosa lililofanyika. Kila kitu kina bei,ndo maana nazjaz akikosewa akatolewa for a shopping spree in dubai,hata kama ulimkata mguu nadhani atakusamehe. Mwisho wa process ya kusamehe ni kusahau kabisa. Kumalizika kwa process kutategemea sana msamehewaji, kwa matendo na maneno. Kama kila siku unarudia kosa,ama vitu vinavyokumbushia kosa,then huwezi kusameheka. Kosa linaweka kovu,utasamehewa ila halitasahaulika unless hautoneshi kile kidonda for a very long time.ngoja niwakumbushe story hii: kuna mtoto kijana alikua na tabia ya kuumiza watu/hasira sana. Akawekewa sehemu ya fence ya mbao na misumari. Akaambiwa every time unakasirika/kosea kagongelee msumari mmoja pale.ukiapologise unauchomoa. Baada ya muda,alioneshwa ile fence,ilivyojaa matundu japo misumari haipo tena.sasa imagine kama umegongelea misumari hadi fence ikaisha na unarudia places,kha! Makovu hayatapona! Kusamehewa kunamtegemea zaidi msamehewaji,japo kuacha kumsamehe mtu ni kuchagua kuwa victim. Nimekusamehe,bt it might never be the same again (maybe aftr 30 yrs,when my teeth starts falling?lol)
Kwahiyo hata kama ni mwizi unajifanya kama vile sio mwizi kisa umemsamehe???

Aiwezekani kwako kumsamehe mwizi hata kama ujui kama atendelea na tabia hiyo? Kusamehe akugarantee mtu kuacha tabia yake!
 
Na unaposema 'hauna masharti' maana yake ni kua hata lile kosa lililotufikisha hapa laweza kurudiwa tena? Unajua msamaha ni kama parole, hahaha sema with humans haina deadline. Unaambiwa 'u ar on 2yrs parole' ukikosea tena unawekwa selo!

...mwj1, ndio kusema kwako wewe kuna nafasi kubwa ya 'baby come back' sababu msamaha wako hauna masharti, au nimekusoma vibaya?
 
Reactions: Mbu
Fighter..MJ1..BAK..King'asti...
Nashindwa kukubaliana na nyie kuhusu kumsamehe mtu na kurudi mlipotoka as if nothing happened.

Jana baada ya kutoka hapa nlikua nafikiria kwanini natofautiana na Boss kwenye swala la ''kutegemea kutendwa'' wakati najua inawezekana , alafu nikafikiria kwanini nyie mnaposema ''ukisamehe unafuta makosa na kurudi mlipokua '' nashindwa kuungana na nyie.
Nikagundua kwamba tatizo ni capability...mtu akishafanya kitu mara moja najua what he/she is capable of. Hivyo UWEZEKANO wa mpenzi wangu kucheat, rafiki yangu kunisingizia/pakazia mambo ya uongo, ndugu yangu kuniibia n.k havinisumbui kwasababu hiyo ndio hali halisi...kwamba chochote chaweza tokea.Kinachonisumbua ni kujua kwa uhakika kwamba those people are CAPABLE OF COMMITTING THOSE ACTS. Kwahiyo mpenzi aliyecheat hatonipa amani ndani ya mahusiano yetu, rafiki mbea/mwongo sitomwamini na mambo yangu na ndugu mwizi sitomwamini na mali zangu.
Nikirudi kwenye ishu ya Boss...watu wanaingia kwenye mahusiano wakijua uwezekano wa kusalitiwa upo ila kinachowapa amani ni imani kwamba yule aliyemchagua hawezi kunicheat. Unachagua kumwamini na hapo ndo unapoanza kutegemea mazuri kutoka kwake badala ya mabaya. Bila hiyo imani kuna watu ambao wangeona mahusiano hayana maana (mimi mmoja wapo) kwasababu ni sawa na mtu kudumbukia mtoni huku akijua fika atazama.

So, YES the possibility is there and we all know it, but capability rises the possibility.
 
Reactions: Mbu
Kwahiyo hata kama ni mwizi unajifanya kama vile sio mwizi kisa umemsamehe???

Aiwezekani kwako kumsamehe mwizi hata kama ujui kama atendelea na tabia hiyo? Kusamehe akugarantee mtu kuacha tabia yake!


Rudia kusoma nilichoandika...
Nimesema kwamba naweza kumsamehe ila siwezi kujifanya kwamba sio mwizi...hivyo ntakua mwangalifu kama bado ntakua karibu nae.Tofauti na wewe ulivyosuggest...kwamba ukisamehe unasahau na kurudi mlipotoka...meaning unasahau kwamba fulani ni mwizi!!
 

...jamani jamani jamani.....!

kaka mimi bado sijakuelewa bana.
unamaanisha kwa wale wanaoachana hawajasameheana?

aisee mimi mwenzenu ndio nilipokwama hapa, nioneeni huruma!!!
yaani msamaha maana yake nirudiane na mwenzangu, otherwise sijamsamehe?
hebu nifafanulie bana, maana nipo kwenye exact situation...natakiwa nisamehe na kumrudia

SIWEZI AISEE!



Mwanajamiione hebu nionee huruma bana,.....
huo msamnaha wa masharti bana.... kumsamehe mtu haina maana kurudiana bana....plssssss!
au nakuelewa vibaya?.....kiukweli nimechanganyikiwa na hizi post zenu wanajamiiforums....

mke/mume baada ya abusive relationship (psychological/physical or both) kamtelekeza mume/mke zaidi ya mwaka mmoja...kila mtu akaendelea na maisha yake...kwakuwa upande ulodhulumiwa umeamua kudai/kutoa talaka kipatikane cheti cha RITA, mtuhumiwa anaomba msamaha ati mrudiane... na asiporudiana nae bado hajamsamehe? hapana...

...mbu nipo kwenye situation hii. Potelea mbali kama msamaha wangu hautaeleweka, kurudiana nae sitaki!
 
To forgive is to reflect on the following;

If only u can reflect on what u've been through together, on the things she went through for u, the things he went through for u, on the things only two of you know about eachother, all the pains u've conquered together, the victories u've won, the ridicules, the miracles, the promises... U know what's important to u... You will fight to stay together.
 
Mbu calm down...
Inabidi kila mtu awe na abaki na maana yake binafsi ya kusamehe maana kwa kufuata kanuni za kina MJ inaonekana wengi wetu hatujasamehe. Yani zaidi ya kaazi kweli kweli kutakiwa kurudisha mahusiano ya mwanzo bila kujali kilichotokea kisa tu umekubali/penda/taka kutoa msamaha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…