Nini maana ya Mahakama kusikiliza kesi Kwa kiswahili na kuandika Mihutasari yake Kwa Kiingereza?

Mpanda nyangobe

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2015
Posts
762
Reaction score
1,688
Nimekuwa mhanga wa kutafsiriwa Mihutasari ya mashitaka iliyoandikwa Kwa lugha ya Kingereza.Mara nyingi Huwa najiuliza maana ya hii kitu Huwa ni Nini...Kwa nini isiandikwe Kwa kiswahili kama ilivyosikilizwa Mahakamani...au lugha ya maandishi ya mahakama ni kingereza hata kama asilimia 99 ya wapeleka kesi hawaijui hiyo lugha Kwa ufasaha..
Huwa sielewi kwa kweli
 
Kabla ya kufika mbali!

Lugha ya Mahama Tanzania ni lugha ya kisheria (legal language) na siyo Kiingereza.

Lugha ya kisheria inaundwa na maneno na misamiati ya Kifaransa, Kilatini na Kiingereza.
 
Mimi sioni kama kuna sababu ya msingi eti! Unaiandika hiyo hukumu kwa lugha ya kigeni ili kumfurahisha nani!
 

Hili swali lipo sambamba na swali la "ni kwanini mwandiko wa madaktari na wataalamu wa afya hausomeki?

Jibu ni moja tu: kuficha siri za kazi Ili Kila mtu asijue yaliyomo na hatimaye kuwategemea wataalamu.

Hata wale wataalamu wa miti shamba, ukihitaji dawa hawezi kukuelekeza ni wapi pa kuchimba bali atakumbia mpe muda akachimbe. Hata ukitaka muongozane hawezi kukubali.
 
Il
Kabla ya kufika mbali!

Lugha ya Mahama Tanzania ni lugha ya kisheria (legal language) na siyo Kiingereza.

Lugha ya kisheria inaundwa na maneno ya Kifaransa, Kilatini na Kiingereza.
Ila cha ajabu hao wafaransa na walatini hawakitumii hicho kingereza ktk lugha yao
 
Ujambazi wa mkoloni bado unaendelea,hii mechi tumelogwa,Rwanda huu ungese haupo kabisa
 
CCM ni wajinga sn, huwezi ukasikia kesi imesikilizwa kwa kifaransa huku ikaandikwa kwa kiingereza
 
Kabla ya kufika mbali!

Lugha ya Mahama Tanzania ni lugha ya kisheria (legal language) na siyo Kiingereza.

Lugha ya kisheria inaundwa na maneno na misamiati ya Kifaransa, Kilatini na Kiingereza.
Acha ujuaji wa kipuuzi!
Hukumu na hati za mashtaka zinaandikwa Kiingereza! Misamiati na jargons zipo kwenye Kila taaluma!
 
Ni ukoloni mambosasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…