Nini maana ya Moshi mweusi kwenye pikipiki?

Nini maana ya Moshi mweusi kwenye pikipiki?

lindunduru

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2015
Posts
392
Reaction score
553
nina pikipiki honda NX 650 Inatoa moshi mweusi wakati hard acceleration.nini sababu? Nini suluhu la hilo tatizo?
 
nina pikipiki honda NX 650 Inatoa moshi mweusi wakati hard acceleration.nini sababu? Nini suluhu la hilo tatizo?
Mosh mweusi hauna shida sana ila ungekuwa wa bluu au mweupe hapo ningekushauri cha kufanyaa ingawa hata huo mweusi ukizid sana itabidi wakuchekie rings .
 
nina pikipiki honda NX 650 Inatoa moshi mweusi wakati hard acceleration.nini sababu? Nini suluhu la hilo tatizo?
Mafuta yanapoingia ndani ya injini (combustion chamber) hayawezi kuungua mpaka yawe yamechanganywa vizuri na hewa ya oxygen. Kiwango cha hewa kinachotakiwa kinategemea na ukubwa wa injini yenyewe. Sasa injini yoyote ya petroli inapotoa moshi mweusi ni dalili kuwa haichomi mafuta vizuri kwa sababu ya kuwepo kwa hewa pungufu kuliko mafuta. Kuna sehemu ya mafuta hutoka nje ya eksozi bila kuwa yameungua. Hakuna madhara makubwa kwa injini yako ila utakuwa unapoteza mafuta mengi bure na vile vile kudhuru mazingiria kwa sababu sehemu ya huo moshi mweusi ni Carbon Monoxide. Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha hali hii itokee.

Kama Injini yako inatumia kabyureta, basi tafuta fundi akuchekia kabureta yako. Huwa kuna boya ambalo huenda sasa hivi lina kitundu kidogo kinachofanya boya lizame ndani ya mafuta na kusababisha kabyereta ishindwe kuzuia mafuta ya ziada na hivyo kuruhusu mafuta mengi yapite. Vile vile inawezekana jet inayopitisha mafuta imeshapanuka kupita kiasi. Kuna sababu nyingi sana zinazoweza kufanya kabureta isifanye kazi vizuri. Sababu nyingine huenda ni kwamba air fliter yako sasa hivi imeziba hairuhusu hewa ya kutosha kuingoia ndani ya injini.

Kama injini yako inatumia Electronic Fuel Injection (EFI) basi pia kuna sababu nyingi sana ingawa kubwa itakuwa ni kuwa ama Oxygen sensor yako imekufa au Air Filter imeziba au Injector nozzle zimepanuka hivyo zinahitaji kubadilishwa. Vile vile inawezekana engine control Unit yako imeharibika, ingawa hii ni nadra sana
 
Mafuta yanapoingia ndani ya injini (combustion chamber) hayawezi kuungua mpaka yawe yamechanganywa vizuri na hewa ya oxygen. Kiwango cha hewa kinachotakiwa kinategemea na ukubwa wa injini yenyewe. Sasa injini yoyote ya petroli inapotoa moshi mweusi ni dalili kuwa haichomi mafuta vizuri kwa sababu ya kuwepo kwa hewa pungufu kuliko mafuta. Kuna sehemu ya mafuta hutoka nje ya eksozi bila kuwa yameungua. Hakuna madhara makubwa kwa injini yako ila utakuwa unapoteza mafuta mengi bure na vile vile kudhuru mazingiria kwa sababu sehemu ya huo moshi mweusi ni Carbon Monoxide. Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha hali hii itokee.

Kama Injini yako inatumia kabyureta, basi tafuta fundi akuchekia kabureta yako. Huwa kuna boya ambalo huenda sasa hivi lina kitundu kidogo kinachofanya boya lizame ndani ya mafuta na kusababisha kabyereta ishindwe kuzuia mafuta ya ziada na hivyo kuruhusu mafuta mengi yapite. Vile vile inawezekana jet inayopitisha mafuta imeshapanuka kupita kiasi. Kuna sababu nyingi sana zinazoweza kufanya kabureta isifanye kazi vizuri. Sababu nyingine huenda ni kwamba air fliter yako sasa hivi imeziba hairuhusu hewa ya kutosha kuingoia ndani ya injini.

Kama injini yako inatumia Electronic Fuel Injection (EFI) basi pia kuna sababu nyingi sana ingawa kubwa itakuwa ni kuwa ama Oxygen sensor yako imekufa au Air Filter imeziba au Injector nozzle zimepanuka hivyo zinahitaji kubadilishwa. Vile vile inawezekana engine control Unit yako imeharibika, ingawa hii ni nadra sana
umeniponya hapo.nimebana jet tatizo limeisha.Asante
 
Back
Top Bottom