Nini maoni yako kuhusu goli walilofungwa Yanga vs As Bamako?

Kwa kweli mm sijui vzr sheria za mpira ila kwa lile goli la jana hapana Kwa kweli n kama kuna kitu kilikuwa hakipo sawa mpaka muda mpira unapigwa , ninacho jua n Yanga tuna goli 1 hao Bamako wana 0.
Kama uchawi hivi,changa lamacho flani hivi.iliniuma sana
 
Kwa kweli mm sijui vzr sheria za mpira ila kwa lile goli la jana hapana Kwa kweli n kama kuna kitu kilikuwa hakipo sawa mpaka muda mpira unapigwa , ninacho jua n Yanga tuna goli 1 hao Bamako wana 0.
Kumbe wee mwananchi....sasa jamani hapo sii mlitakiwa mkabe mpaka filimbi ya mwisho
 
Hilo ni goli kama magoli Mengine.

Magoli ya vichwa hayajaanza kufungwa leo..

Madrid wakiwa na Ramos na Pepe na walikuwa wanafungwa magoli ya vichwa.

Chelsea ya kina John Terry, Michael Essien, Gary Cahill , Ballack, yaani maroboti wote wanaoweza kupiga vichwa na walikuwa wanafungwa magoli ya vichwa.

Yes ni goli kama magoli mengine, Mistake and a goal is scored. Ili goli la kichwa lifungwe lazima kuwe na poor marking au mkabaji azidiwe kwenye kuwania mpira.

Kwani zimepigwa kona ngapi na faulo ndogo ngapi siku ya hiyo mechi?...

This is football.
mwishowe kinachokumbukwa score ni 1-1
 
Ukiangalia wakati kona inapigwa ni mtu mmoja pekee ndo alikuwa kafanya "man marking". Wengine wote walikuwa wanatazama mpira.View attachment 2531254
Sio kwamba wanatazama mpira tuu. Hapo yanga wanafanya zonal marking. So kuna mambo kadha ya kuzingatia.
Kwanza kabisa katika zonal marking in corners unajipanga kwenye nafasi na sio lengo kukabana mtu na mtu klorokwin tamu. Unajipanga kwenye maeno ambayo unadhani mpira utadondoka.

Pili upangaji wa wachezaji unategemea sana aina ya kona inayopigwa; je ni inswinger (inayoelekea goli) au out swinger (inayolikimbia goli).

Jambo lengine lakuangalia ni kiwe na mistarri miwili, first line and second line. Mara nyingi mstari wa kwanza unakuwa umesimama kwenye mstari wa eneo la goli. Kwenye hiyo picha utaona kwamba mstari huo haujapangika vizuri, umemeguka.

Tatizo kubwa la zonal marking kwenye kona ni kwamba mpinzani anaywrukia mpira anakuwa na manufaa ya spidi dhidi ya beki kwa kuwa beki anaanza kugombania mpira akiwa katika stationary position.

Zipo timu nyingi ambao wameweza kujilinda kwa kutumia zonal marking kwa ufanisi mkubwa ikiwemo man city ya pep.
 
Wachezaji waliongozwa na hisia za ushindi wakasahau kufanya matking
 
Asante kwa analysis nzuri.
 
Swali zuri. Benchi la ufundi Lina kazi Kufundisha timu kucheza Kona na Faulo maana Yanga hawafungiki Kwa move.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…