Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,160
- 9,151
Mimi mbwa nimefuga, ili nyumba ailinde,
Kwa jirani nimeiga, anaye kama kipande,
Wabaya akiwaniga, na kuwafanya wakonde,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu.
Cha ajabu huyu wangu, kutwa kucha amelala,
Jua au liwe wingu, njaa hata na chakula,
Kungangania uvungu, na kuleta masihala,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Wamkimbia mwenzangu, na kujaa vamia kwangu,
Wamejua shida yangu, mbwa ashinda uvungu,
Wataka nitia pingu, wachukue mali zangu,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Mbwa nimempa yote, lakini kaniangusha,
Sasa sijui lolote, kweli kanipagawisha,
Natamani ajikate,, thamani yake kashusha,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Kapoteza yangu ndoto, ameniacha gizani,
Angelikuwa mtoto, ningemuuza dukani,
Kaniongeza msoto, na kuninyima amani,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Wajuzi wale mahiri, mnijulishe jamani,
Mwaweza ijua siri, kunitoa matatani,
Ili niitafakari, na kujipa tumaini,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Kwa jirani nimeiga, anaye kama kipande,
Wabaya akiwaniga, na kuwafanya wakonde,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu.
Cha ajabu huyu wangu, kutwa kucha amelala,
Jua au liwe wingu, njaa hata na chakula,
Kungangania uvungu, na kuleta masihala,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Wamkimbia mwenzangu, na kujaa vamia kwangu,
Wamejua shida yangu, mbwa ashinda uvungu,
Wataka nitia pingu, wachukue mali zangu,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Mbwa nimempa yote, lakini kaniangusha,
Sasa sijui lolote, kweli kanipagawisha,
Natamani ajikate,, thamani yake kashusha,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Kapoteza yangu ndoto, ameniacha gizani,
Angelikuwa mtoto, ningemuuza dukani,
Kaniongeza msoto, na kuninyima amani,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?
Wajuzi wale mahiri, mnijulishe jamani,
Mwaweza ijua siri, kunitoa matatani,
Ili niitafakari, na kujipa tumaini,
Nini nitampa mbwa, ailinde nyumba yangu?