Leo nimeangalia wimbo wa Diamond uitwao Baila...nikamwangalia video queen wake, nikagundua ndio yule wa kwenye wimbo wa If ya Davido. Dada huyu ametusua careerwise maana hao ni wasanii wakubwa Afrika. (Na ameshafanya kazi na wasanii kadhaa huko dunia ya kwanza)
View attachment 863885
Nqobile Danseur, Video Queen in Davido's If and Diamond's Baila among her many features
Nikaanza kuwaza kazi yao inaongeza value gani kwenye nyimbo? Zaidi ya kuwaona kwenye hizi nyimbo je, wanatufanya tuzipende kwa ajili yao? Kama Diamond angekaa tu kwenye kiti na kuimba tusingeupenda wimbo? Angekosa views milioni 5 alizonazo?
Sasa nataka kuwauliza wanaume na hata wanawake mtakaopenda kujibu; Je umewahi kupenda wimbo fulani kwa sababu ya urembo, uzuri, madoido ama mapozi ya video queen? Mnadhani video queens wanaongeza value kwenye nyimbo?