Nini Simba ifanye kuvuka group stage ya CAF CL

Nini Simba ifanye kuvuka group stage ya CAF CL

Kila la heri AS Vita, National Al Ahly na El Mereikh

Pigeni huyu Paka Fc arudi kwao, maana amesajili Genge la wahuni na kuzindua jezi ziso na maana

Piga hao Simba mpaka waache tabia zao za misemo yao mara Do or Die, tiki taka mpaka kwa mpaka, War in Dar, Next Level....

Tumewachoka sioni jipya watakalofanya warudi wajipange tu
Tulia tuwatafutie nafasi ya Viti Maalum
 
Tulia tuwatafutie nafasi ya Viti Maalum
Yanga ni kama wale wakinadada wa Covid-19 wa Bawacha.
Alafu Simba ndo mzee Ndungai, anapambana wanamama(Yanga)waingie Bungeni(klabu bingwa)
Simba- Ndungai.
Yanga- Bawacha.
Bunge- Mashindano ya klabu bingwa.
 
Ijumaa hii Simba ataanza kampeni yake ya kutinga robo fainali ya CAF CL kwa kumenyana na AS Vita Club ya DRC katika uwanja wa mashujaa pale Kinshasa. Pambano la mwisho uwanjani hapo alipoteza kwa 5–0 lakini mambo mengi yamebadilika katika vikosi vya timu zote mbili. Vita Club waliuza wachezaji wao hatari kama Francis Kazadi Kasengu, Fabrice Ngoma, Jean Jacques Makusu Mundele, Tuisila Kisinda n.k.

Simba wachezaji wa kikosi cha kwanza walioondoka ni wawili tu Emmanuel Okwi na kiungo mkabaji mghana lakini wakasajiliwa Tadeo Lwanga, Luís José Micquisson, Benard Morrison, Larry Bwalya, na Joash Achieng. Hawa wamedhihirika kuongeza ubora wa Simba. Pia wamemuongeza beki mzimbabwe Peter Muduhwa na striker mnaija Junior Lokosa. Hawa ubora wao haujafahamika bado ndani ya Simba.

Simba ya safari hii inaubora na uwezo wa kupata sare ama ushindi DRC na Sudan ikiwa watakuwa na utayari na ari ya kufanya hivyo. Lakini pia wanahitaji kufanya hivyo ili kujihakikishia nafasi mbili za juu. Msimu wa 2018-19 Simba licha ya kushinda mechi zake zote za nyumbani na kupata alama 9 bado ilihitaji wengine wamfanyie kazi na kweli Al Ahly alimfanyia kazi pale Algeria kwa kuwabana mbavu Saoura na kutoka nao sare.

Ilikuwa ni faida kwa Simba kwani kama Saoura angeshinda basi angemaliza na alama 10 na kufuzu huku Simba akibaki. Pia hao hao Saoura walimfanyia Simba kazi pale Kinshasa kwa kutoa sare ya 2-2 dhidi ya Vita club kwani Vita angeshinda basi angemaliza na alama 9 sawa na Simba lakini angemzidi Simba kwenye head-to-head, Vita alikuwa na magoli 6-2 hivyo angefuzu na kumwacha Simba.

Msimu huu hatuna uhakika kama El merrikh anaweza kufanya kazi hiyo pia hata hawa vita hatufahamu kama wanaweza kumzuia El merrickh (haijulikani yupi kati yao ni bora na anaubora kiasi gani) hivyo ni muhimu Simba akapata alama ugenini ili walau amalize na alama 13 yaani ashinde na kupata sare dhidi ya Vita na El merrikh (alama 4), kisha ashinde zote za nyumbani (alama 9).

Kwa kuzingatia ubora walionao na kutokuwepo mashabiki kwenye nchi hizo basi hili linawezekana kabisa. Hata hivyo wanapaswa kufahamu kuwa watajaribiwa sana kwa baadhi ya wachezaji kukutwa na covid-19 fake. Wawe na utayari wa mapambano.
Mkuu, target ya alama 13 ni nzuri sana lakini nadhani hata alama 10 zinaivusha kwenda hatua inayofuata.
Kwa ''nature'' ya haya mashindano, ni lazima wengine wakufanyie kazi.
Simba ikishinda mechi zote 3 za nyumbani na sare 1 yoyote ya ugenini (Alama 10), automatically atakua ananufaika na matokeo ya wapinzani wake (wanamfanyia kazi mwenye point 10).

Mambo ya kuzingatia kwa timu ya Simba kwa maoni yangu ni kama ifuatavyo:

1. Ili kuongeza morali ni lazima tupate pointi yoyote kwenye mchezo wa kwanza. (Never underestimate the power of starting big).

2. Tupunguze makosa yanayopelekea adhabu za mipira iliyokufa (kona na faulo), lakini pia tufanyie kazi ku-clear dead-balls zinazoelekezwa kwetu. (Mabeki wote wajitahidi kucheza kama Onyango katika hili).

3. Tuongeze ufanisi na aggressiveness kwenye kutumia nafasi za kufunga. Katika hatua hii wapinzani hawatakua wanakuruhusu utengeneze nafasi nyingi. Chache tunazopata tusizitapanye. Hapa Bwalya apigiwe sana kelele kwenye hili.

Vinginevyo nadhani tuna timu nzuri na tunaweza kufanya jambo na kuvuka hatua hii.
 
Mkuu maoni yako ni mazuri, shida ni mechanism ya namna tutavukaje! Kikosi cha Simba bila Onyango pale kati tayari kimeshaonekana kuleta wasiwasi hasa ukizingatia beki mwingine muhimu Erasto Nyoni nae haijulikani afya yake kama ataweza kucheza!
Kwa kocha anapaswa kushugulikia sana kwenye kujenga defence na tuwe na mfumo mzuri wa kujilinda.
Hata mechi ya juzi na Azam kilichotuponza ni defence na pia middle bado hazijaivana vizuri, nashauri kama vipi Mkude arudishwe pale kati!
Wachezaji wote wajengewe saikolojia nzuri ya ukabaji, watambue kuwa kila tunapopoteza mpira maana yake tunaanza kukaba sisi, na tukabe kwa kasi ili kuvuruga mbinu za wapinzani wetu. Timu ikiwa bora kwenye ukabaji huwa ni vigumu kupoteza mchezo hata ikiwa ugenini!
 
Back
Top Bottom