Nini siri ya usalama wa Zanzibar?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Wakati wimbi la utekaji likiwa limeshika kasi Tanganyika, hali ni tofauti kwa jirani yake, Zanzibar.

Zanzibar kumetulia . Zanzibar hakuna utekaji.

Nini siri ya Zanzibar kuendelea kuwa katika amani hata kipindi ambacho jirani yake, Tanganyika, inakabiliwa na maswaiaba ya watu kutekwa na hata wengine kuokotwa wamekufa baada ya kutekwa?
 
Watekaji wa Zanzibar wanaitwa "mazombie". Inadaiwa wamehamishiwa bara wote ili kulinda kiti cha ndugu yao aendelee kuchota hela. Ndiyo maana Zanzibar kuko shwari.
Zanzibar yuko Mwinyi, ukileta ujinga umekwisha hataki mchezo kwenye majukumu yake!!
 
Watatekanaje wakati Kwa mara ya kwanza wametoa maRais wawili mmoja wa Jamhuri na mwingine wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar?

Wanasema charity begins home
 

Siyo huko ndiko kuna lile chimbuko la mazombie mahsusi nyakati za uchaguzi wa rais?

Kwani uchaguzi wa rais umeshafika?
 
Kwani ssh ni Rais Zanzibar? Kule Si Wana Serikali na Rais wao?
 
hata wazanzibari wanasema Rais wao ni Mbara
Hao nao waache maneno yao! Kwani anayoyafanya Mwinyi huko Zanzibar ni kwa manufaa ya Watanganyika au Wazanzibar?

Isitoshe, Mwinyi ana sifa zote za kuitwa Mzanzibar. Nafikiri alizaliwa Zanzibar.
 
Chura mla watu yupo kazini
 
Mkuu hilo kwa sasa ni taifa teule, ukiligusa tu inakula kwako.
 
Sababu ya Zanzibar kuwa salama na mambo ya kutekana ni kutokana na kuwa na rais ambaye anajitambua siyo huko bara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…